Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

WAFANYA BIASHARA ZA MADAWA YA KULEVYA WAZIDI KUKAMATWA


WATU wawili raia wa kigeni wanashikiliwa na polisi mkoani Lindi baada ya kukamatwa wakiwa na kilo 40 za madawa ya kulevya aina ya Heroine yenye thamani ya shilingi bilioni 2.4, tukio lililotokea Februari 7, mwaka huu.

Miongoni mwa watuhumiwa wa madawa ya kulevya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Renatha Mzinga alisema watu hao, Ture Ally (55) raia wa Uganda na Sano Sadick Abobakary (53) wa Guinea Bissau, walikamatwa katika kizuizi cha Nangurukuru wakitokea Msumbiji kuelekea jijini Dar es Salaam.
“Polisi walikuwa wameweka mtego baada ya kupewa taarifa na raia wema, dawa hizo zilikuwa zimehifadhiwa katika paketi 40 zilizokuwa na uzito wa kilo moja kila moja na walikuwa na gari lenye namba za usajili UAU 789 na kesi yao ipo katika Mahakama ya Wilaya ya Lindi.
Wakati huo huo, Februari 12, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, saa 7 usiku, polisi wa kitengo cha madawa ya kulevya, walimkamata msichana aliyetambuliwa kwa jina la Munira Mohamed (32) (pichani) mkazi Mombasa nchini Kenya akiwa na kilo1000 za Heroine.
Binti huyo ambaye bado hajafikishwa mahakamani, alikamatwa akiwa njiani kuelekea Nairobi na Mombasa na Kamanda wa kitengo hicho, Godfrey Nzowa amewataka wananchi kuzidisha ushirikiano kwa kutoa taarifa kuhusu mtu yeyote wanayemhisi kujihusisha na biashara hiyo haramu.
GPL.

MCHUNGAJI ADAKWA NA DWA ZA KULEVYA ZA SH BILION 2 DAR.



Jeshi la Polisi kitengo cha Kupambana na Dawa za kulevya limekamata kilo40 za dawa za kulevya aina ya heroine zenye thamani ya shilingi bilioni2.
Tukio hilo lilitokea juzi eneo la Tegeta nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam ambapo Polisi walifaniikiwa kuwanasa watu wawili wakiwa na dawa hizo ndani ya nyumba inayomilikiwa na mchungaji ambaye wakati huo alikua katika kanisa lake lililopo eneo la Sinza.
Kamanda wa kikosi cha kupambana na dawa za Kulevya Godfrey Nzowa alilithibitishia Gazeti la MTANZANIA kuwa  kuwepo kwa tukio hilo akiomba jina la mchungaji huyo lihifadhiwe kuepusha kuvuruga uchunguzi.
“Ni kweli tukio la aina hiyo lipo  lakini watu kama hawa siwezi kusema moja kwa moja ni Mchungaji  ndio muhusika hadi nipate vithibitisho vya kutosha ikiwa kuendesha kanisa kwani wengi wao wanatumia makanisa kama mwamvuli wa kujificha na kufanya biashara hii,”Alisema Nzowa.
Alisema kwa sasa watu hao wanashikiliwa na Jeshi hilo ambapo wawili kati yao si raia wa hapa nchini wakati upelelezi ukiendelea kabla ya kuweka hadharani ukweli wa mambo.
Ni halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza 
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga