Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

HEBU MUONE LADY JAY DEE ENZI ZA KU RAP


Kweli maisha ni safari ndefu, mkali Jide wa enzi hizoo, kipindi anachana, alikuwa bonge la msela. cheki picha kali nyingine hapo chini.

HAYA SASA, HIZO NDO SIFA ZA MWANAUME ANAEMTAKA JAY DEE


SIFA ZA MWANAUME AMTAKAE LADY JAYDEE KWA SASA Mwanaume mwenye vigezo gani ungependa kuwa nae kwa sasa? JIBU :Anaejali na kuheshimu, mwenye roho ya upendo na huruma, anaeweza ku take care of me financially.Asiechepuka hovyo (Milupo kila kona ),Asiwe
tegemezi.Hata kama sio tajiri lakini asinitegemee.Asiwe mlevi kupindukia wa kulala bar,Wala kulala nje kwa machangu wa Kinondoni au popote pale.Nikikohoa tu awepo hapo Kwa mtazamo wako unaweza kupata Mwamke au Mwanaume asiye na mapungufu?

KUMBE GADNER ALIKUWA MCHAFU KWA WATOTO KIASI CHA KUWASHIKA MAKALIO WHILE MKEWE AKIWA STEJINI. SOMA KISA KIZIMA HAPA

 
Wiki hii Lady Jaydee amewapa nafasi mashabiki wake kumuuliza maswali naye kuyajibu kupitia akaunti yake ya Instagram. Ameulizwa maswali mengi, na miongoni mwa maswali hayo ni la kuhusu ndoa yake na mtangazaji wa Radio E-FM Gadner G. Habash.
Haya ni maswali na majibu kama alivyopost Instagram.

“Tunasikia umeachana na mume ni kweli au uzushi?

JIBU : Hatuja achana niliamua kumuacha

Kwanini umeachana/umemuacha mume?

JIBU : Nimemuacha kutokana na kuwa
Ndoa inatakiwa iwe na maelewano, furaha, amani na upendo. .. ila kwa bahati mbaya vyote hivyo havikuwepo , sikuwa tayari kuendelea kuishi kwa maumivu huku niki pretend ili kuiridhisha jamii. Huoni kama umejishushia heshma kuachana na mume? JIBU : Sioni hivyo, ila naona nilikuwa najishushia heshma zaidi kuishi na mume asie na heshma, anaeweza kutongoza na kushika wanawake makalio wakati mi niko jukwaani naimba.

Kuwapa mademu magari yangu waendeshe na kuyagonga wakati niko safarini . Ukiachilia mbali vipigo.
Kutembea na wahudumu wa restaurant yangu. Ushahidi ninao. …..niliwahi mkuta anawashika mapaja na akakiri kosa. bado kupigana na kuwatusi wateja pia. Kifupi ilikuwa ni ndoa ya mateso.

Baada ya kuachana unategemea kuolewa tena?

JIBU : Ni mapema kujihakikishia uolewaji mwingine, ila haimaanishi kuwa sitopenda tena. Nahitaji kuwa makini zaidi
Kuchagua mtu sahihi wa kumpa moyo wangu.

Kwanini usirudiane na mumeo?

JIBU : Siwezi kurudi nyuma tena, huwa nina misimamo thabiti. Mpk kuamua kuondoka na uvumilivu nilionao mjue ni maji ya shingo. …
When i say never, I mean Never.

Uliwezaje kuishi na mume mlevi namna ile?

JIBU : Nilidhani angebadikika, so nilikuwa natoa nafasi.
Iliposhindikana nikaona isiwe tabu, kila mtu na aubebe mzigo wake. Ukizingatia ananizidi umri miaka mingi, alitakiwa yeye anielekeze zaidi kuliko mimi kumuelekeza maisha mtu mzima.

Uliwezaje kuondoka?

JIBU : Nilipoamua kuwa na iwe basi, Nilitoka bila kubeba kitu.
Nikasafiri kwenda USA, nikakaa huko mwezi mzima ku refresh na kujipima km kweli ntaweza ku move on?
Niliporudi Tanzania sikukanyaga tena nyumbani, mpk muda huu nnapo type na ku post haya majibu.
Kwa ki fupi ni kuwa nili ondoka bila kuaga, sikuona sababu ya kuaga.

Asanteni jamani, nafikiri nimejibu yote.”

GARDER WA JAY DEE ABAMBWA AKILA UJANA NA KABINTI KINGINE.....

Mtangazaji Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteni’ akila ujana na binti (jina halikupatikana mara moja) mrembo bwawani (swimming poOl).

JAHAZI linazidi kwenda mrama! Wakati shauri lao la kugawana mali likidaiwa kufikishwa mahakamani, picha mpya imenaswa ikionesha dhahiri kwamba Mtangazaji Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteni’ ameamua kusonga mbele na maisha yake na kusahau kabisa kama alikuwa na mke aitwaye Judith Daines Wambura Mbibo ‘Jide’, Amani linakupa mchapo kamili.
PICHA IPOJE?
Picha hiyo ambayo inamuashia ‘endiketa’ Jide kuashiria kwamba, Gardner amejiweka pembeni na kuwa bize na ‘starehe’ zake, inamuonesha mtangazaji huyo akiwa ‘ziro distensi’ na kabinti kabichiii (jina halikupatikana mara moja) katika bwawa la kuogelea (swimming pol) huku wakiwa wamening’iniza miguu kwenye maji.
PICHA ILIVYOVUJA
Kwa mujibu wa chanzo makini, picha hiyo iliibwa katika simu ya binti huyo aliyekuwa na Gardner kisha kuisambaza katika mitandao ya kijamii bila yeye mwenyewe kujua.
“Yule dada aliyekuwa na Gardner aliibiwa picha hiyo na shosti yake katika simu yake ndipo akaisambaza mitandaoni,” kilisema chanzo hicho.
NI WAPI?
Mara baada ya mapaparazi wetu kunasa picha hizo, kabla ya kumtafuta Gardner ili kujua ukweli, walianza kusaka eneo ambalo wawili hao walikuwa wakiponda raha zao ambapo jitihada hizo zilikosa majibu ya moja kwa moja.
“Hii ilikuwa ni Mikocheni, Escape One siku hiyo kaka mkubwa alikuwa akifanya yake si unajua tena ameshaona liwalo na liwe,” kilisema chanzo cha kwanza.
ETI NI KIGAMBONI
Chanzo kingine kilichozungumza na mapaparazi wetu kilipishana na mwenzake kwa kudai kuwa wawili hao walikuwa katika ufukwe wa Southern Sun Kigamboni wakijiachia kwa raha zao.
“Mimi kuna kuna mtu kanihakikishia kabisa hii ilikuwa ni Kigamboni, walikuwa wakiponda raha tena Gardner siku hiyo inaonekana alikuwa ameonja kidogo si unajua tena kaka mkubwa na mambo yetu yale, Jide hana chake tena pale,” kilinyetisha chanzo kingine.
Gardner akiwa na Lady Jaydee.
NDIYO ZAKE?
Wakati mapaparazi wetu wakiendelea kuchimba data kuhusiana na mtangazaji huyo ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika Kipindi cha Jahazi cha Redio Clouds FM, chanzo kingine kilipenyeza madai kuwa, Gardner kwa sasa ndiyo zake kujiachia na ‘totoz’ tofauti.
“Aaah…kwani nyinyi hamjui? Jiongezeni bwana, Gardner kwa sasa ameshaondoa mawazo kabisa kwa Jide na badala yake anajipoza tu kwa totoz,” kilisema chanzo.
MAKABRASHA YA LIBRARY
Katika makabrasha yaliyopo katika kumbukumbu za Magazeti Pendwa, Gardner aliwahi kunaswa na kabinti kengine katika Fukwe za Coco jijini Dar wakiwa wamegandana kama kumbikumbi.
GARDNER ASAKWA
Mapaparazi wetu juzikati walimfuata Gardner katika Ofisi za EFM zilizopo Mikocheni jijini Dar ambako mtangazaji huyo anafanya kazi kwa sasa, mtu wa mapokezi alidai hajafika.
ATUMIWA UJUMBE
Jitihada za kumpata kwenye simu zilipogonga mwamba, mapaparazi wetu walimtumia ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) kumsomea mashitaka yake na kama ni kweli ameamua kumpotezea mazima Jide.
Gardner hakujibu mapema, baadaye alipigiwa simu, akapokea na kuambiwa ajibu mashitaka yake kama alivyotumiwa katika SMS. Alijibu kuwa yeye ana marafiki wengi hivyo si kila atakayeonekana naye basi ni mpenzi wake. Msikie:
“Hivi kila mdada nitakayeonekana naye atakuwa ni wifi jamani? Mi nina marafiki wa jinsi zote, sina la kusema.”
UKWELI NI NINI?
Mapaparazi wetu walizidi kumtafuta Gardner kujua ukweli wa picha hiyo na eneo walilopigia lakini hakupokea tena hivyo ukweli anaujua mwenyewe.
TUJIKUMBUSHE
Gardner na Jide waliofunga ndoa Mei 14, 2005 na kutobarikiwa kupata mtoto, Agosti mwaka huu walidaiwa kumwagana.

LADY JAY DEE "SASA NI WAKATI WANGU"


Baada ya tetesi kuwa ameachana na mumewe, mwanamuziki Judith Wambura maarufu Lady Jaydee amesema leo anajitokeza kwa mara ya kwanza mbele ya mashabiki wake kwani wakati wa kufanya hivyo umewadia.
Mwimbaji huyo wa wimbo “Yahaya” anayemiliki tuzo 30 za muziki, amejigamba kuwa hivi sasa yupo bize na kazi, kwani anatarajia kuachia wimbo matata alioupa jina la “Forever” ambao utaambatana na uzinduzi wa video yake Novemba 28.
“Sina habari na mtu na nitaendelea kuwa komando, kilichopo watu wasubiri kuona nitawapa nini maana leo ndiyo naachia wimbo huu, nina mengi ya kuzungumza nao pale nitakapotambulisha kibao hicho, watege tu masikio yao,” alisema Lady Jaydee.
Alisema anataraji kwamba wimbo huo mpya utapendwa na mashabiki wake ikiwa ni moja ya mikakati yake kabambe ya kuwafikia washabiki kwa ukaribu zaidi.
“Watarajie burudani waliyoizoea, nitaachia wimbo wangu leo Jumatatu na video yake nitaizindua Ijumaa na mashabiki watakaohudhuria utambulisho huu watapata bahati ya kuiona video ya “Forever” kwa mara ya kwanza,” alisema Jaydee.
Jaydee aliyepata kutamba na vibao kadhaa kwa kipindi cha takriban miaka 14, amesema wimbo huo amemshirikisha mwanamuziki wa regge, Dabo ambaye pia ni mdogo wake.
“Ni wimbo wa mapenz ambao utabamba, kazi hii imetengenezwa na prodyuza yuleyule Man Water wa Combination Sounds,” alisema.
Alisema pamoja na muziki, ataendelea kuisadia jamii kama ambavyo amekuwa akifanya kila siku na mazingira yakiendelea kuruhusu. “Mahitaji ya jamii ni mengi ila kila kinachowezekana basi Lady Jaydee atafanya kama msaada wa madawati nilioutoa Shinyanga.”
Hata hivyo, nyota huyo hakutaka kuzizungumzia tetesi zilizoenea kuwa ameachana na mumewe.
Lady Jaydee amewahi kutamba na vibao kadhaa huku akiwa na albamu tano ikiwamo, Machozi (2000), Binti (2003), Moto (2005), Shukrani (2007) na The Best of Lady Jaydee (2012).

GARDNER AMBURUZA LADY JAY DEE KORTINI.


Prizenta aliyetua Radio E-FM hivi karibuni akitokea Radio Times FM, Gardner G Habash ‘Kapteini’ anadaiwa kumpandisha kortini mkewe, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ kisa kikisemekana ni mgawanyo wa mali hivyo anataka haki yake baada ya kuwepo kwa madai mazito ya ndoa yao kuvunjika.
Mke wa Gardner G Habash, Judith Wambura Mbibo, ‘Lady Jaydee’ akipozi.
Kwa mujibu wa madai hayo, inasemekana kwamba Gardner amekimbilia mahakamani akidai apewe talaka na waweze kugawana mali walizochuma wote ili kila mmoja achukue hamsini zake.
Chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa familia hiyo kililiambia gazeti hili kwamba, siku chache baada ya kutengana na huku hali ikizidi kuwa mbaya, mtangazaji huyo alichukua hatua ya kutafuta msaada kwa wanasheria.
“Msinitaje jina ila ninachowaambia ni kwamba Gardner tayari ameshampata mwanasheria anataka kumshitaki Jaydee.
“Anachohitaji ni kugawana mali zao, kila mtu afanye maisha yake na ukiangalia tu Gardner hana mpango tena wa kuendelea na maisha ya ndoa na Jaydee ila Jide yeye bado ana matumaini ya kurudiana wawe pamoja na hasa kinachomuuma ni kugawana mali.
Prizenta aliyetua Radio E-FM hivi karibuni Gardner G Habash ‘Kapteini’ Lady Jaydee
“Yaani Gardner ameshafanya kila aina ya jitihada ya kutaka waachane kiroho safi lakini Jaydee anaonekana kutokubaliana na wazo hilo kwani anaogopa ule usemi kwamba mwanamke mjinga huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:“Ishu ya kugawana mali ya Gardner na Jide ndiyo habari ya mjini na ili jamaa apate chake ameona heri atafute mkono wa sheria.”
Chanzo hicho kiliendelea kumwaga ‘ubuyu’ kwamba, kitendo cha Jaydee kutangaza kubadili mwelekeo wa mali zake akianza kwa kubadili jina la ule mgahawa wake kutoka lile la Nyumbani Lounge na kuuita M.O.G ndicho kimemshtua Gardner na watu wake wa karibu.
Kilendelea kudai kwamba, pia ishu ya Jaydee kubadili jina la Bendi ya Machozi na kuiita Lady Jaydee and the Band, nayo imemchochea Gardner na kuamua kukimbilia mahakamani. Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti hili lilimtafuta Gardner ili aweke wazi madai ya kutaka kumburuza mahakamani mkewe huyo na haya ndiyo majibu yake mafupi: “Kaka kusema kweli hiyo ishu nashindwa kuizungumzia maana hata sijui wewe umeipata wapi dah.”
Gardner na Jaydee ambao walifunga ndoa mwaka 2005, wamekuwa wakidaiwa kuwa hawapo pamoja tena huku majukumu ya mtangazaji huyo ambaye alikuwa meneja wa mwanamuziki huyo yakichukuliwa na ndugu wa Jide ambaye ni msanii wa Bongo Fleva aitwaye Wakazi.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga