Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

WAKATI DIMPOZ NA DIAMOND WAKIZUZUKA NA "MAHABA NIUE" ALLY KIBA ANAJIFUA KU POFERM LIVE ZANZIBAR


Wote wa nyumbani Kigoma, ijui kinawasibu nini watu wangu hawa, any way, Ally Kiba yupo Zenzi anajifua ku perform live kwenye tamasha la sauti za busara, wacha wale wazuzuke na Map3nzi yeye kazi zaidi. Angali Picha zaidi hapa chini.















ALI KIBA MBIONI KUFANYA COLLABO NA CHRISS BROWN


Tanzania unao muongoza msanii kutoka
Tanzania ALI KIBA msanii ambae yupo chini
ya uongozi wa Kampuni za SAMSUNG.... Kwa
taarifa zilizopo katika mtandao wa VIP Beats
nchini marekani zinaeleza kua tarehe 24
mwezi wa 11 mwaka 2014 uongozi wa msanii
Chris Brown ulipokea maombi ya muungano
wa wasanii wawili kufanya wimbo wa
pamoja kati ya msanii
Ali kiba na Chris Brown maombi hayo
yaliambatanishwa na Softcopy zilizobeba
nyimbo tatu za msanii Ali kiba ikiwemo
SINGLE BOY, MWANA pamoja na wimbo
aliofanya katika project ya ONE 8. Uongozi
wa Chris Brown umethibitisha kupokea
taarifa za maombi hayo na umeonesha
kupenda sauti ya msanii Ali kiba na kutoa
tamko kua wapo tayari kusimamia kazi ya
pamoja itakayofanywa na wasanii hawa.
Upande wa msanii Chris Brown amesema
hana tatizo yupo tayari kushirikiana na
msanii Ali kiba kwani alipata nafasi ya
kutazama project ya One 8 na ameona
kiwango cha msanii Ali kiba kinaridhisha
Japokua anahitaji marekebisho madogo
sana.BBC SWAHILI Tunampongeza msanii
Ali kiba kwa juhudi zake tunamtakia kila
lakheri katika kazi hii, kuipata habari hii
kamili tembelea mtandao wa VIP Beats,
Channel 0 au unaweza kuipata katika
American Spring news.

ALI KIBA AKIRI KUWA NA BEEF NA DIAMOND PLATINUMZ, AFUNGUKA.


Hatimaye staa wa Bongofleva Ali Kiba amekiri kuwa yuko katika bifu na mwanamuziki mwenzie Diamond Platnumz kwa zaidi ya miaka mitatu sasa.
Kauli hiyo ya Ali Kiba inapingana na ile ya hivi karibuni iliyowahi kutolewa na Mwenyekiti wa Kamati za bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe alisisitiza kuwa wanamuziki hao hawana tofauti zozote na kwamba ni watu tu ndio wanakuza suala hilo.
Hata hivyo, juzi Ali Kiba aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli kuna ugomvi baina yao, huku akisisitiza kwamba tofauti yao ilianza mwaka 2012. Wakati Ali Kiba akifunguka kuhusu bifu hilo hali imekuwa tofauti kwa Diamond ambapo amekaririwa mara kadhaa kuwa hana tofauti yeyote na mwanamuzi huyo ambaye wanatoka mkoa mmoja wa Kigoma na kuunganisha Kundi la Kigoma All Stars. Akizungumza wakati akijibu maswali mbalimbali katika mahojiano maalumu, mwanamuziki huyo pia alielezea mambo mengi kuhusu muziki wake na hii ni sehemu ya mahojiano hayo;
Swali: Nini chanzo cha bifu lako na Diamond?
Ali Kiba: Hakuna kiini kwa sababu nadhani hayo mimi aaah.…Kiukweli haya tuliyamalizaga muda mrefu …Labda watu wahisi kwamba kipindi kile alichonifuta katika wimbo wake (alisema bila kufafanua jina la wimbo) na yeye alivyosema kwamba nimemfuta katika wimbo wangu ‘Single Boy’, mimi sijawahi kurekodi na Diamond katika wimbo wangu hata mmoja na huo niliimba na Lady Jaydee.
Yeye ndiye aliyesema kwamba nilimfuta katika wimbo ule, ila ukweli ni kwamba hatukuwahi kuingia pamoja studio, nilimshauri tufanye wimbo mwingine lakini siyo ule kwa sababu nimeshaimba na Lady Jay Dee.
Swali: Umeshawahi kuwa karibu na Diamond?
Ali Kiba: Hapana yeye ndiyo alishawahi kuwa na ukaribu na mimi.
Swali: Unaweza kufanya kolabo na Diamond?
Ali Kiba: Ngoja nikwambie ukweli, sidhani kama ninaweza kuja kufanya kolabo na Diamond, ila nikipata wimbo ambao nadhani kwamba anastahili kuwapo, kiukweli nitamshirikisha lakini kama hastahili haitawezekana.
Kwa sababu kila wimbo unajielezea, kwa mfano kama mtu anataka kufanya Zouk akimtafuta Stara Thomas itawezekana kwani hayo ndiyo mambo yake, kwa hiyo kama nikitaka kufanya naye wimbo ambao nitaona kwamba unafaa nitamfuata na nitamweleza.


Swali: Utofauti kati yako na Diamond ni upi?
Ali Kiba: Mimi naimba muziki mzuri na nina ‘hit song’, naye Diamond anaimba ‘hit song’, unaposema mimi sina hit song wakati mimi nina nyimbo nyingi kushinda yeye unakuwa unakosea, tangu nimeanza kuimba ni nyimbo mbili tu hazijawahi kuwa hit ikiwamo ‘My Everything’ na ‘Mali Yangu’ lakini nyingine zote zilivuma tangu nianze kufanya muziki.
Swali: Inasemekana katika Tamasha la TigoMusic kuna hirizi zilionekana Uwanja wa Leaders na wewe na Diamond mnatuhumiwa kuhusika, unalizungumziaje?
Ali Kiba: Yaani Mungu mmoja sina imani hiyo kabisa na mimi naamini Mungu na mambo ya hirizi na mimi ni tofauti. Nadhani watu wanasema hivyo kwa sababu wanadhani kwamba kuna bifu. Binafsi sina bifu na msanii yeyote labda kama wanaweza kuwa na bifu na mimi binafsi simchukii msanii yeyote na sina bifu na yeyote.
Swali: Video yako ya Mwana imezungumziwa na mashabiki kuwa haikuwa na uhalisia. Pia ilikuwa ya kawaida sana, wewe binafsi unalichukuliaje?
Ali Kiba: Video ilivyokuwa ndivyo ilipangwa iwe kwa sababu kila mtu alikuwa amejenga picha itakuwaje kwa hiyo ililazimika kufanya vile kwa kuwa watu walishapanga mpaka gharama kwa kuwa nilikaa muda mrefu pasipo kufanya. Ningefanya kitu ambacho watu walikifikiria kiukweli ingekuwa karaha, nilichozingatia mimi ni kuimba vizuri na kuonyesha fikra za wimbo husika.
Swali: Vipi uliandaa ‘skripti’ ya video au aliamua GodFather kuifanya vile ilivyotengenezwa?
Kiba: Tulikuwa na ‘script’ yetu pia waongozaji wa video walikuwa na yao ambayo walitupatia. Hivyo tukakubaliana nao kwa sababu tulitaka kuleta utofauti na kila kitu kikakaa sawa.
Swali: Ni kweli kwamba una mpango wa kufanya kolabo na Chris Brown?
Ali Kiba: Uwezekano wa kufanya upo kwa sababu kila kitu ni mipango kwa hiyo naweza kufanya kolabo na wasanii wa kimataifa na mashabiki watarajie kufanya hivyo.
Swali: Kwa nini haujafanya video ya Kimasomaso na ulisema video ya Mwana ingefanyika Dar es Salaam kwa nini ulitengenezea Afrika Kusini?
Ali Kiba: Video ya ‘Kimasomaso’ ilishindikana kutokana na muda ulikuwa hautoshi, nilijikuta niko katika mambo mengi sana kwani nilikuwa nimeegemea katika video ya Mwana kwa hiyo nilipokuja kugeuka ikawa ni vigumu.
Nilisema kwamba nyingine ningefanya nje ya hapa lakini kwa ‘Mwana’ sijaelewa kwanini nifanye hapa, tofauti na hiyo nyimbo haikuwa na maana ya Dar es Salaam, maana yake ni mwanamke na mwanamume sikuona sababu ya kufanyia hapa jijini.
Ukitumia neno la Dar es Salaam ni kwa sababu ni jiji lenye changamoto kwa hiyo unapozungumzia hilo ina maana kwamba ni Joharnesburg, Nairobi, Kampala, London majiji ambayo yana changamoto mfano video ya Macmuga nilifanyia Marekani.
Source, Mwananchi.

SHETTA AKIRI HANA BIFFU NA ALI KIBA



Msanii ambae tumezoea kuskia akifanya collable takriban kila ngoma ambayo amwahi kutoa, jana amejikuta akipokea maneno machafu kutoka kupitia kwenye mitandao ya kijamii, baada ya baadhi ya blogs kuandika kuwa ana bifu na Alikiba na hawezi kufanya nae collable

Leo hii Shetta ameonyesha kusikitishwa na kitendo hicho na kujitetea kuwa alipigiwa simu na mtanagzaji mmoja na kumuuliza kuhusu collable yake na alikina na ndipo aliposhtuka na kusema yeye hana colable na Alikiba na wala saa hii hana mpango wa kuwa na collable na msanii yoyote wa ndani wala wa nje


"Alikiba mi sina tataizo nae kabisa wala msanii yoyote Tanzania, lakini kitu ambacho nimekiona tangia jana na leo kwenye baadhi ya bogs na habari tofauti tofauti kwamba "angali shettah alichojibu baada ya kuulizwa collable na Alikiba" kwanza nianzie kwenye hiyo story, niliulizwa kwamba kuhusu collable lako na Alikiba, mi nikawa nimeshtuka sababu sina collable na Alikiba na sijafanya yaaani kabisa collable na Alikiba lakini nilichokijibu ni kwamba "Sijafikiria kufanya wimbo na msanii yoyote Tanzania kwa sasa hivi , nikatoa sababu, sababu nimefanya collable nyingi sana hapa ndani, kwahiyo nilichokijibu ni kwamba kiroho safi tu kwamba sifikirii kufanya kazi na msanii wa ndani labda nifanye na international artist kwasababu labda ya kunisongeza zaidi zaidi mbele au nifanye wimbo peke yangu," amesema Shettah

Ofcourse kama inafika time nahitaji kufanya kazi na Alikiba na yeye yupo willing tutafanya wimbo, ameendelea kuongea Shettah, lakini sijawahi kuhit au kutoka katika mziki wngu kwa kumsema mtu vibaya au kujaribu kuzungumza kitu kibaya ili ije iwe story watu wazungumze, kwahiyo nilichokijibu nilikuwa sawa kutokana na swali nililoulizwa, kwahiyo baada ya kuja kugeuka na zile headline zilizoandikwa kwenye blog mbalimbali, watu kuja kunitukana kuzungumza vibaya kwenye social network, kwenye page yangu, imekuwa tatizo, kwangu mimi si kitu kizuri yaani haijakaa vizuri kwa upande wangu.

ALI KIBA, NYOTA INAYORUDI KWA KASI BONGO FLAVA.



Asilimia kubwa ya wapenda burudani Afrika Mashariki kwa sasa wanazungumzia kuhusu ujio wa msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Salehe Kiba, maarufu kama Alikiba.
Baadhi ya watu wamekuwa wakimlinganisha na mwanamuziki nyota kwa sasa Diamond Platnumz, ambaye naye kwa sasa yupo katika nafasi ya juu kimataifa kama ilivyokuwa kwa Alikiba miaka mitatu iliyopita.
Si kwamba ndiyo anaingia katika muziki, kwa watu wanaojua historia ya bongo fleva wanakumbuka kwamba kijana alikuwa tishio, kwani amekuwapo kwenye gemu tangu mwaka 2004 na kufanikiwa kutoa wimbo wake wa kwanza ambao ulimtambulisha uliojulikana kama ‘Cinderella’.
Baada ya kumaliza elimu ya kidato cha sita mwaka 2004, alianza kujituma katika muziki na kufanikiwa kuandika wimbo wake wa kwanza, ‘Maria’. Mwaka huohuo Alikiba alianza kutengeneza albamu yake ya kwanza. Ilipofika mwaka 2005, alipata ofa ya kwenda kuchezea soka la kulipwa nchini Uganda, lakini baadaye aliachana na mpira ili kuendeleza kipaji chake cha muziki.
Mwaka 2007 alifanikiwa kuachia albamu iliyopewa jina la ‘Cinderela’, sambamba na kuachia wimbo huo redioni, ambao ulivuma na kusababisha albam hiyo kuuzika zaidi sokoni. Albamu hiyo ilikuwa ni kati ya albamu bora na iliyouza zaidi mwaka 2007 Afrika Mashariki.
Tangu hapo akaanza kupokea mialiko mingi kutoka Kenya, Rwanda, Uganda na Burundi. Aliifanya Afrika Mashariki kumjua kwa muda mfupi kupitia vibao kadhaa vilivyokuwepo katika albamu hiyo kama MacMuga, Nakshi Mrembo, Njiwa na Mali Yangu.
2008 Alikiba aliachia albamu ya pili ‘Alikiba 4 Real’ na wimbo wa kwanza kuachia ulikuwa ‘Usiniseme’ na wakati huu alikuwa ameshatangaza jina lake Afrika Mashariki na kwingineko.
Albamu hiyo ilimfanya aanze kuaminika zaidi, mwaka huohuo akateuliwa na kushinda tuzo za Kilimanjaro Music Awards kupitia wimbo wake wa Cinderella.
Aliendelea kutafutwa kwa ajili ya kusakata kabumbu ambapo mwaka 2009, alipokea maombi kwa ajili ya kuichezea timu ya African Lyon ya Tanzania lakini alikataa na kuamua kuingia kwenye mitindo ambako hakukumchukulia muda mwingi.
Akutana na R Kelly
Ilipofika mwaka 2010 ndipo alipopata dili la One 8 na kufanikiwa kufanya kazi na wanamuziki wa kimataifa akiwamo R Kelly na wengine saba kutoka Afrika. Alipokutana na R Kelly alimsifu kwamba ana sauti nzuri na ya kipekee, hivyo kupendekeza aanze kuimba katika singo ya pamoja ‘Hands Across the World’. Kupitia wimbo huo, mtandao maarufu wa kimuziki duniani Billboard walilitangaza kundi la One 8 kama “Best Bet of 2011” kupitia orodha ya nyimbo zao bora duniani.
Mwaka huohuo Alikiba aliteuliwa na kushinda tuzo ya BEFFTA London Awards kama ‘Best International Artists’ (ACT) na kumshinda mwanamuziki 2 Face Idibia. Pia alifanikiwa kurudi na tuzo ya Sexiest Male Artist.
Historia yake
Alikiba alizaliwa Iringa Novemba 26, 1986 kutoka kwa mama yake Tombwe Njere na Saleh Omari. Yeye ni mtoto wa kwanza kati ya watoto wane katika familia yao, akifuatiwa na Abdu Saleh Kiba.
Muziki ni kati ya vitu ambavyo zimekuwa vikipendwa na mwanamuziki huyu tangu utoto wake.

Mwananchi.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga