Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

SKENDO NZIMA YA STARA THOMAS KUFUMANIWA NA MUMEWE HII HAPA



Staa wa Bongo Fleva, Stara Thomas akiwa na mumewe.
Stori: Deogratius Mongela na Chande  
HAYA ni madai mazito! Kwamba, staa wa Bongo Fleva ambaye juzi kati alinusa kwenye gospo ‘ikamshinda', Stara Thomas anadaiwa kufumaniwa na mumewe, Raumu Ally mpaka kufikishana polisi, Risasi Jumamosi halipitwagi na ‘ubuyu’. 
Kwa mujibu wa shuhuda wa kuaminika, tukio hili lilijiri hivi karibuni nyumbani kwa familia hiyo, Tabata jijini Dar es Salaam.

FUMANIZI LILIVYOTOKEA
Akilisimulia Risasi Jumamosi baada ya kuulizwa kama kweli fumanizi lilikuwepo, mume wa Stara alifunguka hivi: “Ni kweli ilitokea. Siku ya fumanizi nilikuwa nimesafiri, lakini nikarudi ghafla bila kumpa taarifa mke wangu.
“Nilikuwa nyumbani, yeye hakuwepo. Saa 9:00 usiku ndiyo nilimwona Stara akirejea tena akiwa amelewa. Aliletwa na gari mpaka nje ya nyumba.” 
NDANI YA GARI KWA NUSU SAA
“Lile gari lilisimama zaidi ya nusu nje bila kushuka mtu ndipo nikaamua kulifuata. Stara aliponiona akamwambia dereva ambaye najua ni jamaa yake, aondoe gari kwani mimi ni mume wake nitampiga.
“Nilizuia wasitoke, yule jamaa akarudi nyuma na kuniparuza kwenye mguu na tairi, nikadondoka. Niliposimama nikaokota jiwe na kulirushia gari nikavunja kioo cha mbele.” 
STARA, JAMAA POLISI
Mume huyo anaendelea kusimulia: “Baada ya hapo Stara aliondoka na yule jamaa mpaka Kituo cha Polisi Tabata ambapo walinishtaki. Niliitwa polisi kwa madai ya uharibifu wa kioo.
“Kwa vile nilikuwa nasafiri kwenda nje ya nchi (ni dereva wa malori) niliona mambo yaishie pale kituoni, nilikwenda nikachukuliwa maelezo kisha nikalipa shilingi laki saba (700,000).”
Mume wa Stara Thomas Raumu Ally. DALILI ZA KUVUNJIKA KWA HESHIMA
Habari zaidi zilidai kwamba, wawili hao wamekuwa kwenye ugomvi wa mara kwa mara.
Imeelezwa kwamba, ugomvi wao ulianza pale Raumu aliposhindwa kulipa ada ya shilingi laki tano ya mtoto wa Stara (jina tunalo) huku madai ya mchepuko nayo yakisambaa hali iliyokuwa ikishusha heshima ya familia. 
TUJIUNGE NA RAUMU 
Akifafanua kuwepo kwa sakata hilo pamoja na chanzo kizima, Raumu alisema kuwa Stara amekuwa akimfanyia vituko na mambo ya ajabu tangu aliposimamishwa kazi kwenye kampuni aliyokuwa akifanyia awali (jina kapuni) baada ya kutokea matatizo. “Mimi ni dereva wa malori, nakwenda Lusaka (Zambia) na Congo (DR), nimekuwa na mgogoro na Stara baada ya kusimamishwa kazi. Unajua ukiwa huna kazi hata fedha huna. Alitaka nimlipie ada ya laki tano mtoto wake lakini nikawa sina, ikawa maneno.” 
KUMBE KUNA MENGINE ZAIDI
“Huwezi kuamini ndugu zangu wamenitenga mimi kwa sababu wakati naanza kuishi na Stara nilibadili dini yangu ya Kiislam na kumfuata yeye kwenye ulokole (wakati huo) halafu leo hii ananiletea mambo ya ajabu! Stara amuogope Mungu.” 
WALIKUTANA HIVI 
Akizungumzia historia fupi ya uhusiano wao, Raumu alisema walikutana kwa mara ya kwanza, Stara alikuwa akisoma Shule ya Sekondari ya Mzizima, Dar, miaka ya 90.
Stara Thomas. MAP3NZI MOTOMOTO
Map3nzi yao yalikuwa motomoto lakini baadaye walipotezana kisha kuja kuonana tena miaka ya hivi karibuni huku kila mmoja akiwa na maisha yake.
Kutokana na namna walivyopendana kupita kiasi kipindi cha awali, wawili hao walirejesha uhusiano ambapo mwanaume huyo alihamia nyumbani kwa Stara, Tabata baada ya staa huyo kuachana na mumewe wa ndoa aliyezaa naye watoto wawili. 
STARA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Stara ili kujibu tuhuma hizo ambapo alipopatikana mahojiano yalikuwa hivi:
Mwandishi: Haloo Stara…
Stara: Haloo.
Mwandishi: Unamfahamu Raumu?
Stara: Kwanza wewe nani? 
Mwandishi: Mimi ni mwandishi wa Global Publishers.
Stara: Ndiyo namjua Raumu. 
Mwandishi: Ni nani kwako? 
Stara: Ukitaka kujua kuhusu Raumu, njoo nyumbani tuongee.
Mwandishi: Nataka unijibu kuhusiana na tuhuma za yeye kukufumania.
Stara: Njoo nyumbani wewe na Raumu tuongee tuyamalize huku.
Hata hivyo, mwandishi wetu alitinga nyumbani kwa staa huyo lakini hakumpata hadi gazeti hili linakwenda mitamboni.

Nyuma ya Pazia Sakata la Traffiki Walionaswa waki Dendeka


Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, chini ya Kamanda Mohammed Mpinga, limekuwa mstari wa mbele katika kusimamia maadili ya askari wake na kuwa mfano wa kuigwa lakini kuna baadhi wanalichafua, Ijumaa limenyetishiwa kamchezo kamili.
Polisi wa usalama barabarani wakidendeka.
HABARI KAMILI
Habari kamili ikufikie kwamba nyuma ya picha ya askari wawili, mwanamke na mwanaume wa usalama barabarani (matrafiki) wanaodaiwa kuacha kazi ya kuongoza magari na kwenda kufanya uchafu kichakani kuna utata mkubwa.
PICHA INASEMA
Picha hiyo inamuonesha trafiki mwanamke akiwa amepakatwa mapajani na trafiki mwanaume aliyekalia kitu kwa chini ili kupata balansi ya kumbeba mwenzake huku wawili hao ‘wakifanya yao’ wakiwa na sare za kazi.
TUJIUNGE NA VYANZO
Baada ya picha hiyo kusambaa kwa kasi ya moto wa kifuu kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii na kugeuka habari ya mjini, watu walikuwa na maoni tofauti huku baadhi wakipiga simu kwenye chumba chetu cha habari wakitaka kujua ukweli juu ya uwepo wa tukio hilo.
SIMU YA KWANZA
Simu ya kwanza iliyopigwa ilidai kwamba matrafiki hao ni maarufu katika Barabara ya Bagamoyo ambapo mara nyingi huongoza magari maeneo ya Tegeta jijini Dar.
Kamanda Mohammed Mpinga.
“Huyo mwanaume ni jamaa mmoja mpole sana anajulikana Tegeta na ana gari aina ya Baloon (Toyota).
“Huyo mwanamke, kwanza ni mke wa mtu lakini yupo bomba (mzuri) kinoma. Hata madereva daladala wanamjua maana amejaliwa, akitembea lazima atingishe,” kilidai chanzo hicho na kuongeza:
“Hapo ni maeneo ya Tegeta kwa sababu ukiangalia vizuri kwenye picha hiyo utaona nguzo ya umeme mkubwa wa Zanzibar.”
WHATSAPP
Wakati tukio likiwa ‘hot’, picha hiyo ilitumwa kwenye chumba chetu cha habari kwa WhatsApp huku ikiwa na maelezo kwamba tukio hilo lilijiri hivi karibuni mkoani Dodoma bila kufafanua maeneo gani kwa kuwa Dodoma ni kubwa. 
NI KANDA YA ZIWA?
Chanzo kingine kilichozungumza na gazeti hili kilidai kwamba tukio hilo siyo la Dar wala Dodoma ni maeneo ya Kanda ya Ziwa.
“Hilo tukio ni la Kanda ya Ziwa. Itakuwa ni kwenye moja ya Mikoa ya Kanda ya Ziwa (kati ya Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Geita),” kilidai chanzo hicho.
IMETENGENEZWA?
Baadhi ya wadau wa jeshi hilo walidai kwamba kuna uwezekano picha hiyo ni ya kutengeneza (photo shop) kwa kuwa haikujulikana aliyeipiga na kwamba iliwezekanaje kuwapiga ili hali wakijua ni kinyume na maadili.
“Unajua kinachonifanya nihisi kama imetengenezwa ni namna walivyojiachia. Kwa vyovyote kuna kitu cha ziada kimefanyika kwenye hiyo picha,” alisema mmoja wa wachangiaji mtandaoni.
MTAALAM: HAIJATENGENEZWA
Ili kuondoa utata huo wa kutengenezwa au kutokutengenezwa, gazeti hili lilimwonesha picha hiyo, mtaalam wetu wa kompyuta (IT), Nicolaus Trac ambaye alithibitisha kuwa siyo ya kutengenezwa.
“Ni vigumu kuwa ni ya kutengenezwa kwa sababu kuu tatu.
“Moja, mandhari ni moja, ingekuwa ya kutengeneza kila mmoja angeonekana tofauti lakini mazingira yanaonesha imepigwa eneo moja.
“Pili, angalia mikono yao ilivyovaana au kuingiliana. Sidhani kama kuna mtaalam angeweza kuweka mikunjo hiyo ya mikono na vidole bila kukosea sehemu.
“Tatu, angalia huyo mwanamke alivyomkalia mwanaume, inaonesha kabisa kumkalia kwake kumesababisha mkunjo katika suruali kwenye paja la mguu wa kulia,” alifafanua Nicolaus.
PETE YAIBUA MAMBO
Mbali na kukemea tabia hiyo na ukosefu wa maadili hasa kwa mtumishi wa serikali, wapo baadhi ya watu mitandaoni walikuwa wakimshambulia trafiki mwanamke kwani picha ilimuonesha akiwa na pete ya ndoa kidoleni.
“Mimi sijui kama huyo trafiki ni mumewe lakini namuona ana pete ya ndoa maana yake kuna harufu ya mchepuko. “Lakini hata kama ni mumewe, kwa nini wafanye mambo ya chumbani hadharani tena na sare za kazi? Kama walikuwa wamezidiwa sana si wangeenda nyumbani?” Alihoji mwanamke mmoja aliyetumiwa picha hiyo kwenye WhatsApp.
KAMANDA MPINGA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilimfowadia Kamanda Mpinga picha hiyo kwa njia ya WhatsApp ambapo alikiri kuwa nayo na kwamba  wanaifanyia kazi kabla ya kuchukua hatua kali kwa wahusika.
Katika mahojiano ya Kamanda Mpinga na Global TV Online hivi karibuni, kamanda huyo alisisitiza kwamba kikosi chake kinaongoza kwa maadili na kwamba inapotokea tukio kama hilo hutolewa adhabu kali.

MPIGA CHABO WAKUBWA WAKIWA GESTI VYUMBANI AKAMATWA MWANZA.


NI aibu kubwa! Mpigachabo maarufu nchini, Andrea Masangu (29) amenaswa akiwa kwenye uvungu wa kitanda akiwapiga chabo wanandoa, Ijumaa Wikienda lina mkasa wote mkononi.


Tukio hilo lilitokea Januari 10, mwaka huu, ndani ya Gesti ya Riverside, Stendi ya Nyegezi jijini hapa ambapo kijana huyo aliingia kwa kuruhusiwa na mhudumu wa gesti hiyo katika mtego makini uliotegwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global

NI aibu kubwa! Mpigachabo maarufu nchini, Andrea Masangu (29) amenaswa akiwa kwenye uvungu wa kitanda akiwapiga chabo wanandoa, Ijumaa Wikienda lina mkasa wote mkononi.

Tukio hilo lilitokea Januari 10, mwaka huu, ndani ya Gesti ya Riverside, Stendi ya Nyegezi jijini hapa ambapo kijana huyo aliingia kwa kuruhusiwa na mhudumu wa gesti hiyo katika mtego makini uliotegwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers na mwishowe kujikuta akiumbuka.
OFM WAPOKEA MASHTAKA
Wiki moja nyuma, mtu mmoja alipiga simu kwa OFM jijini Dar akidai yeye ni msomaji wa Magazeti Pendwa ya Global. Akasema ameamua kupiga simu ili kumshtakia Andrea akidai amekuwa na tabia iliyoota sugu ya kupiga chabo wapenzi wanapokuwa gesti.

“Mimi naitwa…(akataja jina lake), napiga simu kutoka jijini Mwanza. Kuna bwana mmoja anaitwa Andrea, amekuwa na tabia ya kuwachungulia (kuwapiga chabo) wapendanao wanapokuwa gesti.
“Mbaya zaidi, huyu jamaa nasikia huu mtindo anao siku nyingi sana. Amekuwa akienda hata nje ya Mkoa wa Mwanza kwa ajili hiyo,” alisema mtoa habari huyo.
Akaongeza: “Kuna watu wanasema kuwa hata Tabora, Dodoma wanamjua kwa tabia hiyo. Hebu OFM njooni Mwanza.
Ijumaa Wikienda: Usipate tabu, hukohuko Mwanza kuna OFM wametokea hapa makao makuu. Nawapa namba yako ili mshirikiane.
Mtoa Habari: Mtakuwa mmefanya jambo la maana sana.

KAZI YAANZA
Ndani ya dakika tano tu, OFM waliopo Mwanza wakapewa namba za mnyetishaji wetu, kazi ikaanza.
OFM Mwanza, walimtafuta mtoa habari huyo na kukaa naye meza moja ambapo walipanga mipango.
Miongoni mwa mipango hiyo ilikuwa ni pamoja na kutoa taarifa kwenye kituo cha polisi jijini Mwanza ambapo maafande walijipanga.
SIKU YA TUKIO
Siku ya tukio, Andrea alikwenda kwenye gesti hiyo na kumuuliza mhudumu kama kuna wateja wa ‘shot’ taimu’ wataingia, akajibiwa wapo njiani.
Akaomba alipe shilingi elfu mbili (2,000) ili atangulie kuingia yeye kwenye chumba ambacho mhudumu huyo atahakikisha anawaingiza wapendanao hao.
OFM WAJULISHWA, WAINGIA
OFM walijulishwa kuwa mpiga chabo huyo amewasili na tayari ameingia chini ya kitanda kwenye gesti
hiyo, nao wakamchukua OFM mwanamke na kutinga naye sanjari na Polisi wa Dawati la Jinsia Jiji la Mwanza.
OFM WAMCHEZEA MCHEZO
Ndani ya chumba hicho, wapendanao (mke na mume) hao walifikia kitandani. Lakini ili kujiridhisha kama kweli Andrea alikuwa uvunguni, OFM mwanaume alijifanya ameangusha pesa chini, alipoinama kuiokota akamuona kiaina lakini hakuonesha kushtuka.
Ndipo OFM hao ‘wapendanao’ walianza kuchojoa nguo za juu na kuzitupa chini kana kwamba walikuwa tayari ‘mchezoni’ ili kumshawishi Andrea aendelee kuamini na kufurahia dhamira yake chafu.
OFM NJE YA GESTI
Nini kilibaki hapo kama si OFM waliokuwa chumbani kuwajulisha kwa simu wenzao waliokuwa nje na polisi?
Chumba kilivamiwa, Andrea akajikuta yuko chini ya mikono ya sheria akionekana ameingilia faragha.
ETI AKAJITETEA!
Baada ya kutolewa chini ya kitanda, Andrea aliwekwa mtu kati na kuhojiwa kulikoni kuwa mpiga chabo wa kiwango kile?
Andrea alianza kwa kuomba msamaha na kuahidi kuacha kabisa tabia hiyo. Alikiri amekuwa akichungulia watu wengi sana wanaofika katika gesti za jijini Mwanza.
“Jamani nimekoma, ni shetani tu, naacha kabisa mambo haya ‘haki  ya Mungu’ kuanzia leo sifanyi tena. 
“Kweli nimewachungulia watu wengi sana na sijapata faida yoyote, sijui shetani gani aliniingia,” alilalama Andrea na kuongeza kuwa hayupo peke yake bali ana marafiki zake wengi ambao hufanya kama anavyofanya yeye.
Soo hilo liliisha kwa Mshauri Nasaha wa Taasisi ya Farijika, Aisha Mtumwa kumrekebisha kisaikolojia Andrea sambamba na kumpa onyo kwamba akirudia tena atatupwa rumande kwa kosa la kuingilia faragha ya watu.

NILIMFUMA MKE WANGU AKINYATIA KUINGIA KWENYE CHUMBA CHA MDOGO WANGU WA KIUME AKIWA NUSU UCH!


Kumbe ilikuwa ni tabia yake kwenda kwa mdogo wangu huyo wa kiume ambaye ni mtoto wa shangazi yangu, na kula uroda wakati mimi sipo, nilipata tetesi hizo kutoka kwa housegirl wetu lakini sikuweza kuamini. siku hiyo nilirudi kimya kimya na kujifungia chumba kimoja ambacho kilikuwa hakitumiki, na wote hawakujua kama nilikuwa nipo.

Mara ilipofika ,majira ya saa nne hivi usiku, nilimuona mke wangu ananyata huku akiwa amevaa nguo za ajabu sana, alipita chumba cha house girl na kisha kuzama kwenye chumba cha ndugu yangu huyo wa kiume. nilitoa simu yangu niliyokuwa nayo na kumpiga picha kwa ushahidi zaidi, alipoingia tu na mimi nikaingia alishindwa kuamini na gafla alianza kuomba msamaha, nilimuuliza mke wangu kwani umefanya nini alishindwa kunijibu huku akiendelea kulia na kuomba msamha, nilitoka na kwenda chumbani kwangu kulala, yule mdogo wangu wa kiume alifungasha usiku ule ule na kuondoka na mke wangu hakuweza kulala, iliniuma sana sikuweza kuamini kwani nilimuamini sana mke wangu.Kesho yake sikuweza kuvumilia nilichukua uamuzi wa kumrudisha kwao , kwani ningeweza kumfanya kitu kibaya sana kama ningeendelea kumuona.

AVUA NGUO NA KUBAKI NA "CHUP!" TU BAADA YA KUPANDWA NA FURAHA YA KUMFUMANIA SHEMEJI YAKE GUEST.




AMA kweli dunia uwanja wa fujo! Mrembo aliyetajwa kwa jina la Baby amefanya kituko cha aina yake kwa kusaula nguo mbele ya hadhara baada ya shemeji yake maarufu kwa jina la Baba K kufumaniwa.
FUMANIZI LAIVU
Tukio hilo la aina yake lililovuta wengi lilijiri kwenye gesti moja (jina tunalo), maeneo ya Temeke jijini Dar hivi karibuni baada ya jamaa mmoja kumwekea mtego rafiki yake aliyekuwa akimtongoza mkewe na kumfumania laivu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, mara baada ya fumanizi hilo, mrembo huyo ambaye ni shemeji wa mwanaume aliyefumaniwa alionesha maajabu alipoamua kuvua nguo bila kusitasita.
“Alianza kuvua kidogokidogo, baadaye akaamua kuvua zote na kubakia na nguo ya ndani tu. Kwa kweli iliwashangaza wengi pale kwenye eneo la fumanizi. Halafu unajua fumanizi lenyewe lilikuwa ndani ya chumba, dada yake alikuwa huko, yeye nje,” alisema mmoja wa mashuhuda.
Imeelezwa kuwa, baada ya mwanamke huyo kuvua nguo  alianza kushangilia kwa nguvu huku akirukaruka kwa furaha na kusema:
“Heee! Mwanaume kapatikana leo, kwa furaha namwaga lazi, eti shemeji. Shemeji gani unamwacha mkeo unakwenda kwa vidampa?”
AKATA MAUNO
Ilielezwa kuwa furaha ya mwanadada huyo haikuishia katika kuvua nguo na kusema hivyo tu, kwani aliendelea kusheherekea kwa kukata mauno huku na kule kama anayetamba.
Ilisemekana kwamba wakati ‘akifanya yake’ midume na watoto walikuwa wakifaidi sinema ya bure huku wengine wakiona aibu na kujichomoa zao eneo la tukio.
“Labda anamshukuru Mungu kwa kufanikisha fumanizi la shemeji yake kwa kuwa alihusika kwenye kusuka mchezo mzima,” alisema shuhuda mwingine.
MSHANGAO
Kitendo hicho cha kusaula nguo zote na kushangilia kiliwashangaza baadhi ya watu ambao walikuwepo eneo hilo la tukio na wengi wao wakajiuliza kulikoni shemeji mtu apitilize furaha kiasi hicho kisa tu mume wa dada yake kafumaniwa?
Wakizungumza na Amani, mashuhuda hao walisema kwa vyovyote kuna la ziada nyuma ya pazia ndiyo maana mwanadada huyo alifurahi kupita kiasi.
“Kwa vyovyote kuna kitu, si bure. Mbona huyu dada kapagawa kuliko hata aliyefumania? Mh! Yetu macho,” alisema mmoja wao huku mwingine akidakia:
“Hapa dada mtu anatakiwa kuwa makini sana na huyu dada si ajabu anachochea ili ndoa ivunjike achukue nafasi. Hawa ndiyo akina dada wa mjini bwana.”
BOFYA HAPA KUMSIKIA
Amani lilipomvaa mrembo huyo na kumuuliza kwa nini alikuwa amepagawa na kusaula nguo, mwanadada huyo alijibu kwa mkato kuwa alifurahishwa mno na fumanizi hilo ingawa alikiri aliyefumaniwa anaumia huko alipo.
“Hahahahaaa…Huyu shemeji yangu amezidi, afadhali leo amefumaniwa nimefurahi sana,” alisema dada huyo huku akikatiza mtaani akiwa na kufuli pekee.
TURUDI KWENYE FUMANIZI
Katika fumanizi hilo ambalo lilikuwa la aina yake ilielezwa kuwa shemeji mtu alikuwa akimsumbua mke wa rafiki yake ndipo mke huyo akaamua kumweleza mumewe ambaye walimwekea mtego na kufanikisha kumnasa laivu.
Hata hivyo, mfumaniaji na mfumaniwa, wote walikubaliana ambapo jamaa aliyefumaniwa alipewa kibano na onyo kali iwe mwanzo na mwisho kusarandia wake za watu.
Ilidaiwa kuwa, baada ya makubaliano hayo, mambo yote yaliishia hapo bila kufika kituo chochote cha polisi.
MAFUMANIZI YA SIKU HIZI
Uchunguzi wa Amani umebaini kuwa, miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mafumanizi ya makusudi. Katika kila wafumaniwa kumi, saba ni mitego tofauti na zamani ambapo ilikuwa ya kushtukiza.
Hata hivyo, uchunguzi inaonesha kuwa, wengi wanaofumaniwa ni wanaume wenye tabia ya kutongoza wake za watu au wake za marafiki zao wa karibu.    

GPL

YOUNG DEE AKAUNUSHA KUHUSU SKENDO YA KUFUMANIWA NA LULU WAKILA RAHA ZA UKUBWANI NDANI YA GARI



Juzi kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds FM chini ya bwana Sudi Brown ama Gossip Cop kulikuwa na fununu kali iliyokuwa inamuhusu mwanadada wa Bongo Movies na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya Young D 'Young Dar es Salaam' kama mwenyewe anavyojiita baada ya wawili hao kukutwa kwenye gari wakifanya lile tendo linaloruhusiwa kufanywa mara baada ya mdada na mkaka kufunga ndoa.
Young D
                                                                                              

Kwa mujibu wa Sudi Brown 'Gossip Cop' wawili hao walikutwa maeneo ya Mbezi Beach ndani ya gari aina ya Hyundai ya mwanadada Lulu na polisi wa doria wakivunja amri hiyo iliyokatazwa na vitabu vyote vitakatifu kwa maana ya biblia, Quran na vitabu vingine vya dini ulimwenguni.

Habari zainasema baada ya wawili hao kukutwa eneo hilo na polisi walipelekwa pembeni gizani na kuongea na Polisi kabla ya wao kutokomea wasipojulikana na gari hilo.

Alipopigiwa simu mwanadada LULU alipokea na kukata muda mfupi na baadaye Young D alipopigiwa simu alitoa majiu ya utata kama alivyoongea mwenyewe kupitia kwenye kipindi cha U-heard cha Clouds Fm.
GPL

Mke anaswa Akijivinjari na Hawara Ndani ya Chumba cha Mumewe, Angalia Yaliyomkuta Mgoni huyo!!!




TIMBWILI zito limeibuka baada ya mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Samora kumnasa ‘live’ mkewe Hadija akimsaliti kwa kuvunja amri ya 7 (usizini) na hawara ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, tena kwenye chumba chao, Ijumaa lina ishu kamili.

Mshangao: mtuhumiwa akikodoa macho baada ya kunaswa live na mke wa mtu chumbani kwa mwenye mali.
Habari kutoka chanzo cha uhakika kilitonya kuwa Samora na Hadija ni wanandoa waliooana Bomani pale Magomeni, Dar, mwaka 2009 na katika ndoa yao wamebahatika kupata mtoto mmoja wa kiume.
Tukio hilo la fumanizi lilijiri maeneo ya Kinondoni-Kwamsisiri, Dar nyumbani kwa wanandoa hao, majira ya saa 1:00 usiku, Julai 29, mwaka huu.
Aibu: mtuhumiwa akijaribu kuficha sura yake baada ya fumanizi hilo.
NDOA YATUMBUKIA NYONGO
Habari zilieleza kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, ndoa ya wawili hao ilitumbukia nyongo na kuingia kwenye mgogoro ambapo pamoja na kuweka mambo sawa, waliendelea kukwaruzana mara kwa mara.
Mshangao: Nisameheni jamani!
CHANZO NI NINI?
Ilidaiwa kuwa chanzo cha wawili hao kuhitilafiana ni kutokana na mwanaume kumtuhumu mkewe kutoa tunda nje ya ndoa.
Ikasemekana kuwa baadaye wapambe walimfuata Samora na kumtonya kuwa mkewe amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na kidume mwingine nje ya ndoa yao ndiyo maana amekuwa akimletea nyodo ‘mapichapicha’.
Iliendelea kudaiwa kuwa baada ya ndoa kutibuka, Samora alikuwa mnyonge na mwenye msongo wa mawazo hivyo ikabidi aikimbie nyumba kwa muda na kwenda kwa wazazi wake.
Ilisemekana kuwa, Samora alirejea nyumbani huku akifanya uchunguzi wa nguvu akiwatumia majirani kumpatia taarifa kuhusu kila mwanaume aliyeingia na kutoka nyumbani kwake yeye akiwa hayupo.
Bwana Samora akiwa na mkewe Hadija siku ya harusi yao.
KUMBE NI RWEKAZA
Uchunguzi wa Samora ulibaini kuwa, Hadija alikuwa ‘akibanjuka’ nje ya ndoa na mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Rwekaza ambaye ni mfanyakazi serikalini.
Habari za kina zilisema kuwa, Samora alitonywa kwamba jamaa alikuwa akitimba na gari aina ya Suzuki Swift 1.3 na siku nyingine alikuwa akilala hadi asubuhi bila tone la soni kuwa Hadija ni mke wa mtu.
Samora na Hadija wakiwa na wapambe wao siku ya harusi.
SAMORA AJIPANGA
Baada ya kupata uhakika huo ndipo Samora akajipanga kwa kuwatafuta vijana wa mtaani ili Rwekaza atakapofika nyumbani hapo kulala na mkewe wamvamie na kumfanyizia.
Mshikemshike: Samora (wa tatu kushoto) na wapambe wake wakitaka kumshushia kichapo mtuhumiwa.
RWEKAZA MTEGONI
Bila kufahamu kuwa anasubiriwa kwa hamu majira yaa saa 1:00 usiku, Rwekaza huyooo, akatinga nyumbani hapo na moja kwa moja akafikia chumbani kama kawaida yake.
Wakiwa chumbani, ilidaiwa kuwa waliendelea na mambo yao huku Rwekaza akiwa tumbo wazi na suruali yake amefungua zipu huku Hadija akiwa amesaula na kubaki na ‘kufuli’, kisha akajifunga khanga moja.
Hasira: Samora (kushoto) akimkunja mwizi wake baada ya kumfumania.
FUMANIZI KABANG’
Katika fumanizi hilo, Samora alitinga chumbani humo akiwa ameambatana na kundi la vijana kibao ambao walikuwa na lengo moja tu, kumfanyia kitu mbaya Rwekaza.
Wakiwa chumbani, kuliibuka bonge la timbwili baada ya Samora kumshuhudia mwenza wake aliyekula kiapo cha kutotengana naye akisaliti ‘laivu’ penzi lao.
Baada ya kuona machafuko makubwa ya hali ya hewa chumbani, mwanahabari wetu aliwataarifa polisi katika Kituo cha Kwamsisiri ambao walifika maeneo hayo na kufanya kazi kubwa na nzuri ya kuepusha balaa au mauaji kwa kuwa Samora alikuwa na hasira kali.
Albamu ikionyesha picha walizopiga Samora na mkewe Hadija wakati wakisaini kitabu cha ndoa.
KWELI NI MKE WA NDOA?
Ili kuthibitisha kuwa ni mkewe wa ndoa, Samora alizama kabatini na kuchomoa cheti cha ndoa na picha walizopiga siku ya ndoa yao zikiwaonesha wakiwa na tabasamu la ‘mimi na wewe milele’ kabla ya shetani ‘kufanya yake’ kwenye unganiko lao.
Wananchi wakiwa nje ya nyumba alipofumaniwa bwana Rwekaza.
MAJIRANI
Kwa mujibu wa majirani, tukio hilo liliwasikitisha wengi huku wakiamini kabisa kuwa ni nadra matukio ya mafumanizi kutokea katika kipindi cha mfungo.
“Jamani hata Mwezi Mtukufu? Ni aibu sana kwa mke kuingiza mwanaume mwingine kwenye chumba cha mumewe. Kweli hili fumanizi ni kiboko,” alisikika mmoja wa majirani hao walioshuhudia tukio hilo muda mfupi baada ya kufuturu.
Gari la mtuhumiwa aina ya Suzuki Swift 1.3 likiwa nje ya nyumba alipofumaniwa.
SAKATA LINAENDELEA
Hadi gazeti hili linaondoka eneo la tukio wahusika wote walikuwa kituoni hapo hivyo tunaendelea kulifuatilia sakata hilo kwa karibu sana na pia kuwapata wahusika wazungumzie kilichojiri.

CHANZO: GPL

Mwanaume Akatwa Miguu baada ya Kufumaniwa na Mke wa Mtu



Na Mwandishi Wetu, Kilosa
ALI Omar, mkazi wa Kijiji cha Mabana, wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro anashikiliwa na polisi kwa kosa la kumkata miguu Said  Iddi kwa kumtuhumu kumfumania na mkewe aliyejulikana kwa jina la mama Ali, mkanda mzima upo mikononi mwa Amani.


Mke wa mtu sumu: Said  Iddi akiwa chini baada ya kukatwa miguu na Ali Omar.
Tukio hilo la kikatili lilijiri Julai 15, mwaka huu wakati Said na mama Ali walipokuwa ndani ya nyumba ya Ali iliyopo kijijini hapo.
MANENO YA SHUHUDA
Akizungumza na mwandishi wetu, shuhuda mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja alisema Said alifumaniwa ndani ya nyumba asubuhi akiwa na mke wa Ali baada ya kuwekewa mtego ambao ulimnasa vizuri.
“Ali alipewa habari na kijana mmoja aitwaye God kwamba mkewe si mwaminifu katika ndoa, akamwongezea kuwa anatoka kimapenzi na Said. Ndipo Ali na mnyetishaji wake huyo walipopanga kumfumania jamaa,” alisema shuhuda.
Chini ya ulinzi: Mwenye mali, Ali Omar (kati) akiwa chini ya ulinzi baada ya kumkata Said.
Aliongeza kudai kuwa, Said ni msimamizi wa mashamba ya Ali kijijini hapo na kwamba God ni mtoto wa mwenye nyumba ambayo Ali amepanga kijijini hapo.
MPANGO WA FUMANIZI
Habari zinapasha kuwa mara baada ya mnyetishaji kutoa taarifa za usaliti huo, Ali alimtafuta  ‘baunsa’ ambaye jina lake halikuweza kujulikana mara moja na wakaweka mtego kwa kujificha karibu na nyumba hiyo ambayo Said angeingia ili kuivunja amri ya sita ya Mungu.
Umbea kazi: Kijana aitwaye God (kulia) aliyetoa taarifa kwa Ali naye akiwa chini ya ulinzi.
Katika kufanikisha mtego huo, mmbeya huyo alipewa jukumu la kuhakikisha nyendo za Said na mama Ali siku hiyo zinarekodiwa mpaka kuingia ndani ya nyumba hiyo na kumtaarifu Ali ambaye siku hiyo alimuaga mkewe kwamba amesafiri.

SAID ATINGA NYUMBANI KWA ALI
Habari zinasema mtoboa siri huyo alimwambia Said kuwa Ali amesafiri na ndipo jamaa akafunga safari kwenda kwa mama Ali kwa nia ya kujivinjari licha ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ukifikia katikati.
Mwanamke hutulii?: Mke wa Ali Omar naye akipelekwa polisi baada ya tukio hilo.
Habari zinadai mara baada ya kufika kwa Ali, Said aliingia ndani ya nyumba bila kujua kwamba mwenye mke alikuwa amejificha jirani akisubiri mtego unase.
Inasemekana Said akiwa ndani, Ali na baunsa wake waliibuka kwa kutaarifiwa na God na kumnasa jamaa huyo huku akidai ni mgoni wake. Alimuuliza maswali kadhaa, yakiwemo haya:
“Umekuja kufanya nini ndani ya nyumba yangu? Kwa nini umekaa na mke wangu?”
Habari zinasema Said alijibu hakuona ubaya kwa kuwa yeye ni mwangalizi wa mashamba ya mwanaume huyo hivyo anaweza kuingia ndani kwake wakati wowote.
Said  Iddi akiwa amezungukwa na wananchi baada ya kukatwa miguu.
MWENYE MKE ATIBUKA NA MAJIBU, AMWAGA DAMU
Jibu hilo lilidaiwa kumtibua Ali na ndipo yeye na baunsa wake wapomfunga kamba miguuni Said na kuanza kumkata kwa panga mguu mmoja kisha kuugeukia wa pili.
Said alipiga mayowe yaliyowafanya wanakijiji kukimbilia eneo la tukio kwa lengo la kujua kulikoni ambapo walimkuta Said akiwa anavuja damu na sehemu ya nyuma ya miguu ikiwa nyanga’nyang’a.
Said akipelekwa kwenye difenda.
MWENYE MKE AKIMBIA, ANASWA
Ali, God na baunsa walikimbia eneo hilo. Baadhi ya wanawake walitumia khanga zao kuifunga miguu ya Said kwa lengo la kujaribu kuzuia damu isiendelee kumwagika. Said alikuwa akilia sana.
“Wanakijiji walichukizwa sana na ukatili uliofanywa na Ali, hivyo wakaanza kumsaka na kumkamata kichakani akiwa amejificha pamoja na God. Alipewa mkong’oto kwa lengo la kutaka kumuua, lakini viongozi wa kijiji walisihi asiuawe bali afikishwe kwenye kituo cha polisi,” alisema shuhuda.
...Akiingizwa ndani ya difenda.
MKE, MUME, MMBEYA WAFIKISHWA POLISI
Polisi wa Kituo cha Dumila waliitwa na kumchukua Said, Ali na God kwa kutumia gari aina ya Land Rover lenye namba za usajili T 750 AAJ. Mke wa Ali yeye alipelekwa polisi kwa pikipiki.
Walipofika kituoni, Said alipewa fomu ya matibabu ya polisi (PF 3) na kupelekwa Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa matibabu.
“Pale hospitali Said alishonwa miguu yote lakini madaktari wakaamua ahamishiwe katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi,” alisema shuhuda huyo.
Bwana Said akiwa ndani ya difenda.
ANAWEZA ASITEMBEE TENA
Akaongeza: Daktari mmoja alisema haamini kama jamaa (Said) atatembea tena kwa sababu zana iliyotumika kumkata ilifika hadi kwenye mishipa ya nyuma ambayo ndiyo humfanya binadamu aweze kusimama na kutembea.
Said akishonwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa.
BAUNSA ASAKWA
Afisa mmoja wa polisi kituoni hapo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini kwa kuwa si msemaji, alisema wanaendelea kumsaka baunsa aliyeshirikiana na Ali kumkata miguu Said.
...Said akizidi kupatiwa huduma.




 SOURCE: GPL

Mke Amfuma Mumewe na "Shostito" wake Guest House, Amshushia Kipondo Heavy!!

-->





Kweli Mke wa Mtu Sumu na Mume wa Mtu maziwa, baada ya tetesi za muda mrefu kwamba shoga yake ndiye anayemtibulia ndoa yake hatimaye ukweli umejidhihirisha baada ya Mke kumfuma Mumewe wakiwa na Besti wake huyo ambaye mbali na kusoma pamoja hadi Field walifanya pamoja lakini bado akamtenda mwenzie visivyo.
Baada ya Fumanizi hilo mke aliamua kuwapigia mashoga wengine waliokuwa karibu ili washirikiane kumshushia kipondo mwizo huyo.

Baada ya Fumanizi, Walazimishwa kufanya Mapenzi Hadharani.

Ama kweli mke wa mtu sumu, Siku za hivi karibuni huko, Nigeria karibu na cho kikuu cha Anambra, ilitoka hukumu ya aina yake baada ya mume kumfuma mkewe akivunja amri na mpenzi wa nje. Baad ya fumanizi hilo mume mtu akiwa na wenzake walimtoa jamaa huyo na mkewe hadi uwanjani huku wakiwalazimisha waendelee na kitendo chao hadharani.

Hata hivyo mume hakuweza kukaa na kuangalia badala yake alirudi nyumbani na kutupa vitu vya mwanamke huyo nje.


Video hii pia ilikuwepo you tube lakini ilionfolewa baada ya kuonekana inapingana na Terms of Service(Tos)


Sista Aliyefumaniwa Atozwa Faini ya Laki Saba

MAHAKAMA ya Mwanzo mjini hapa, imemtia hatiani aliyekuwa mtawa wa Shirika la Kitawa la Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Sista Yasinta Sindani, kwa kufumaniwa na mume wa mtu na kuamriwa kumlipa fidia ya Sh 700,000 mlalamikaji.
Katika kesi ya msingi ya madai, mlalamikaji Asteria Mgabo alimtaka Sista Yasinta amlipe Sh milioni 3 baada ya kumfumania na mumewe wa ndoa, Martin Msangawale (39) ambaye pia ni mkazi wa mjini hapa.
-->
Sista huyo ambaye ni daktari katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa, kwa sasa anaishi nje ya nyumba ya utawa eneo la Kantalamba.
Katika hati ya awali ya madai, inadaiwa mshitakiwa alifumaniwa na Asteria akiwa na mumewe Msangawale wakiwa kwenye nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Chipa iliyopo eneo la Katandala mjini hapa, Desemba 24 mwaka jana majira ya saa 7 usiku ikiwa ni siku ya mkesha wa Sikukuu ya Krismas.
Akisoma hukumu hiyo juzi, hakimu wa mahakama hiyo, Jaffar Mkinga alisema kuwa ushahidi uliotolewa na mlalamikaji ulikuwa mzito wenye kuondoa shaka zote kuwa mdaiwa alitenda kosa hilo tofauti na utetezi uliotolewa na mdai kuwa ulikuwa dhaifu.
Awali katika utetezi wake mdaiwa aliiambia mahakama hiyo kuwa kwanza alikuwa hajui kuwa Martin alikuwa mume wa mtu na kukiri mbele ya mahakama hiyo kuwa alimweleza kuwa hana mke hivyo alimwomba amuoe.
Lakini Hakimu Mkinga alipinga utetezi huo kwa sababu usiku huo wa mkesha wa Krismas mwaka jana, saa saba na robo usiku, mlalamikaji akiongozana na mwenyekiti wa mtaa wakiwa na mashahidi wengine watatu, walimkuta mdaiwa na Martin wakitoka katika moja ya vyumba katika nyumba ya kulala wageni ya Chipa, akasainishwa.

“Kama hukufahamu kuwa Martin alikuwa hana mke ilikuwaje ukakubali kusaini karatasi hiyo ya fumanizi iliyoandaliwa na mwenyekiti huyo?” alihoji hakimu, akamhukumu kulipa sh 700,000.


source: mpekuz
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga