Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

MAKAH@BA MWANZA WAVAMIWA NA OFM WAKIWA WANAJIUZA


Issa mnally/Mchanganyiko
Baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa kuna maeneo jijini Mwanza yanatisha kwa biashara ya ngono, Operesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers hivi karibuni imetua na kufanikiwa kufumua dangaro maarufu.

Makahaba hao wakiwa katika mawindo yao ya kila siku. Awali, dawati la OFM lilipokea sms kutoka kwa msomaji wake aliyeomba hifadhi ya jina lake iliyosomeka hivi: “Jamani nyie tunawaaminia kwa kufichua maovu, tumeona kazi nyingi nzuri mlizofanya Dar sasa tunaomba mje huku Mwanza maana kuna maeneo kama vile Liberty, Market Street, Deluxe na Villa Park, Kirumba yanatisha kwa uchangudoa.” 
Baada ya kupokea meseji hiyo, mwishoni mwa wiki iliyopita kamanda wa OFM akiwa na wenzake walitingia jijini humo na katika zungukazunguka yao, walifanikiwa kunasa eneo maalum linalosifika kwa biashara hiyo haramu.
Ilikuwaje?
...Wakisubilia wateja.Mishale ya saa 8 usiku mapaparazi wetu walitonywa juu wa kuwepo mabinti waliojikusanya katika maeneo ya Liberty (Mwanza mjini) huku wakitumia nyumba moja iliyopo karibu na hapo kufanyia ufuska wao. 
Bila kuchelewa, timu ya OFM ilifika na kuwakuta mabinti hao wakiwemo wake za watu wakiwa wamevaa kihasara ikionekana wazi walikuwa ‘sokoni’.
Kufuatia hali hiyo, maparazi wetu walianza kuwafotoa picha kitendo kilichowafanya watimue mbio kuelekea kusikojulikana.
Kamanda wa OFM akitua jijini Mwanza. Hata hivyo, baada ya timuatimua hiyo, inadaiwa wengi waligundua kuwa OFM wako Mwanza na wengi waliokuwa wakifanya ufuska eneo hilo walihama wakihofia kunaswa. 
Uchunguzi uliofanwa na gazeti hili umebaini kuwa, kama ilivyo maeneo mengine, Mwanza pia wapo wake za watu na wanafunzi ambao nyakati za usiku huingia viwanja na kujiuza ili kupata pesa za kujikimu.OFM inaahidi kuendelea kufichua maovu mkoani humu ili kuhakikisha maadili yanachukua mkondo wake.


HALI YA KIKONGWE ALICHAPWA AKIHUSISHWA NA USHIRIKINA BADO NI MBAYA


KIKONGWE Hilda Johnfan Pili (79) aliyepigwa mawe kutokana na imani za kishirikina katika Kijiji cha Kilagano, Peramiho mkoani Ruvuma hivi karibuni, bado hali yake ni mbaya kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata.
Kikongwe akiwa hoi baada ya kupigwa mawe kutokana na imani za kishirikina.
Kikongwe huyo na Maurus Zenda (46) anayedaiwa kuwa ni mwanaye kiukoo, kwa pamoja walijeruhiwa vibaya baada ya kupigwa na baadhi ya ndugu zake kwa kuhisiwa kuhusika katika upotevu wa mtoto Adamu Mselewa (4).
Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia wa ukoo huo, hali ya bibi huyo bado ni mbaya na wanajitahidi kwa hali na mali kuokoa maisha yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma alikolazwa.
“Bado hali ni mbaya, bibi bado analalamika maumivu, tunaendelea na matibabu huku tukisubiri madaktari watatueleza nini kuhusu maendeleo yake, ikishindikana hapa tutamhamisha hospitali, afadhali kidogo Maurus,” alisema mwanafamilia huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Mtoto wa kikongwe huyo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Mihayo Msekhela,  waliwakamata watuhumiwa 10 kutokana na tukio hilo, ambao ni Ambros Mselewa (24) ambaye ni baba mzazi wa mtoto aliyepotea, Maria Zenda (45), Lameck Zenda (22),  Pautas Komba (24), Fredy Mende (24), Gerord Ngonyani (27), Odilo Mwingira (21), Shadrack Ngonyani (22), Hilda Zenda(36) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Muunganozomba.
Msikhela alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa moja asubuhi baada ya baba mzazi wa mtoto huyo, Ambros Mselewa akiwa pamoja na watu wengine walipoanza kuwashambulia watu hao wakimtaka kijana wao aliyepotea kimauzauza tangu Februari 3, mwaka huu.

NIKIMFUMANIA MUME WANGU NTAMSAMEHE, KWA JINSI NNAVYOMPENDA.


Wiki hii kupitia ukurasa huu tunaye mwanadada anayefanya vizuri kwenye ulimwengu wa filamu anayefahamika sana kwa jina la Sandra lakini jina lake halisi ni Salama Salmini.Ni mama wa watoto wawili na anaishi na mume wake. Mwandishi Wetu Mayasa Mariwata hivi karibuni alimbana kwa maswali 10 na bila hiyana alitoa ushirikiano katika kuyajibu, shuka naye…
Mkongwe katika tasnia ya filamu Bongo,Salama Salmini 'Sandra'.
TQ: Ni kitu gani kilichokufanya udumu kwenye ndoa yako mpaka sasa jambo ambalo wasanii wengi linawashinda?Sandra: Unajua mwanamke mjinga anaivunja ndoa yake mwenyewe, mimi siyo mjinga hivyo nailinda kwa kadiri ninavyoweza. Uvumilivu, kupendana kwa dhati na kuheshimiana ndiyo siri kubwa.
TQ: Unapokuwa nyumbani kwako huwa unapendelea kuvaa mavazi ya aina gani, hususan ukiwa chumbani na mumeo?Sandra: Nikiwa nyumbani kwa kuwa naishi na wanangu huwa napenda kujifunga kanga na kuvaa madira lakini nikiwa chumbani, huko ni full kujiachia.
TQ: Inadaiwa wewe ni kati ya mastaa wasiopenda kufanya kazi za nyumbani na mara nyingi unamuachia majukumu hausigeli ikiwemo kumpikia mumeo, hili likoje?
Sandra: Sipendi kabisa mume wangu apikiwe chakula na hausigeli, mimi ni mwanamke ninayejua majukumu yangu, kwa hiyo hausigeli huwa ananisaidia tu.
TQ: Hivi siku ikitokea umemfumania mumeo utafanyaje?
Sandra: Kwa kweli naomba Mungu hilo lisitokee maana sijui maumivu nitakayoyapata, kwanza nitamsamehe sababu nampenda sana mume wangu.
TQ: Umeshawahi kuchepuka? Kuwa mkweli Sandra.
Sandra: Sijawahi kufanya hicho kitu wala sifikirii. Nifuate nini wakati kila kitu nakipata kwa mume wangu jamani? Sina tamaa za kijinga mimi.TQ: Hili la wasanii kuibiana mabwana halikutii hofu?
Sandra: Mimi sihofii hilo kabisa maana najiamini mno, kama mtu ni mal@ya, mal@ya tu hata umchunge vipi akiwataka atatembea nao.
TQ: Ni sehemu gani ambayo inakupa mzuka zaidi kwenye jumba la mah@ba?
Sandra: Ninapokuwa hayo maeneo kila kona ya mwili wangu huwa imejaa msisimko, ila napendelea zaidi ‘rom@nce’.TQ: Siku za wikiendi unapendelea kufanya nini?
Sandra: Napenda kutoka na familia yangu kwenda ufukweni kuogelea na kubadilishana mawazo na mume wangu.
TQ: Utapenda watoto wako warithi fani yako ya uigizaji?
Sandra: Sifikirii wanangu waje kuwa wasanii, kikubwa nawaombea mafanikio wawe watu bora zaidi kwenye taifa.TQ: Hivi baada ya kuolewa kwenda viwanja ndo’ basi?
Sandra: Naiheshimu sana ndoa yangu, sioni sababu ya kwenda kukesha klabu, huwa napenda kutulia chumbani na mume wangu na kutazama muvi.
GPL.

SNURA AKANA KUZAA MTOTO WA PILI.


Msanii anayefanya muziki na filamu Bongo, Snura Mushi ameeleza kushangazwa kwake na taarifa zinazozidi kuenea kuwa amejifungua, jambo ambalo anadai eti siyo kweli.
Msanii anayefanya muziki na filamu Bongo, Snura Mushi.
Madai ya staa huyo kujifungua kwa siri yameenea na hata wasanii wenzake wanajua hivyo lakini mwenyewe amekuwa akikanusha na kuwaacha mashabiki wake njia panda.Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni, Snura alisema yeye ana mtoto mmoja mkubwa lakini madai ya kwamba amejifungua hivi karibu hayana ukweli.
“Mimi sina mtoto mdogo, mwanangu ni yule mnayemjua, hao wanaosema nimezaa mbona wananizalisha?” alihoji Snura ambaye baada ya muda mrefu kupotea, juzikati aliibukia kwenye Ukumbi wa Escape One ulipo Msasani, jijini Dar.

FULL STORY YA MAPIGANO YA AL SHABAB NA VIKOSI VYA ULINZI VYA TANZANIA HUKO TANGA



Na Mwandishi Wetu, Tanga
NI kama kumekucha! Siku chache tu baada ya Gazeti la Ijumaa (ndugu na hili) kuandika ukurasa wake wa mbele habari yenye kichwa; Kiongozi wa kikundi cha kigaidi kinachoua polisi na kuiba silaha kwenye vituo nchini...NI HUYU, kundi jingine limeibuka na kuandika mkanda wa video wakizungumzia uhalifu.
Moja ya kikosi cha kigaida cha Al Shabaab.
Cha ajabu, sanjari na kundi hilo linalodai liko Tanga, Tanga hukohuko kwenye Kitongoji cha Amboni, Ijumaa iliyopita kulizuka mapigano kati ya polisi, askari wa JWTZ wakipambana na kundi lililodhaniwa ni la kigaidi likiwa limepiga makazi ndani ya mapango ya kihistoria ya  Amboni, Uwazi lina full story.
Katika mapigano hayo hadi juzi Jumapili, askari mmoja wa JWTZ aliuawa huku wanajeshi watatu na askari polisi wawili wakijeruhiwa na kulazwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo.
MASHUHUDA WA MAPIGANO
Kabla Uwazi halijatiririka na video hiyo, lilizungumza na wananchi wenye makazi yao kwenye Kitongoji cha Amboni ambako mapigano ya askari na wahalifu yalitokea.
Mzee Ibrahimu Ally, yeye anasema: “Siku ya tukio (Ijumaa asubuhi) mimi nilikuwa nimepumzika ndani kwangu lakini ghafla nikasikia mlio wa risasi kama mara mbili hivi.
“Mke wangu alikuwa anafua, akaja mbio ndani akisema ni majambazi. Nilimwambia funga mlango haraka sana, akaufunga. Lakini cha ajabu milio ya risasi ikawa inaongezeka kadiri muda ulivyokwenda.
“Ilifika mahali nikajua si majambazi bali tumevamiwa na majeshi ya nje ya nchi. Kwani sasa risasi zilikuwa zikirindima kila muda. Hali ikawa tete kwa kweli. Hata hapa ninapoongea na wewe siamini kama ile milio ya risasi haitajirudia tena.” 
Kundi la wahalifu wanaodaiwa kujificha na kushambulia Polisi katika mapango ya Amboni.
WAZIKIMBIA NYUMBA
Mwanahawa Mudale yeye alisema: “Ilibidi tuhame majumba kwenda kujificha, tatizo ni ile milio ya mabomu na risasi na baadaye tukaona chopa (helikopta) ikitembea angani. Awali tulijua ni vita ya nchi na nchi, kumbe walikuwa askari wetu.”
SIKU MBILI HAKUNA KULALA
Baadhi ya mashuhuda wanasema kutokana na milio ya risasi kwa siku ya Ijumaa hadi Jumamosi asubuhi, hakuna mwananchi aliyepata usingizi.
“Mimi na familia yangu hatujalala jamani. Risasi na mabomu yasikieni hivihivi tu. Kuna wakati tulikuwa tukiona miale ya moto kutokea kwenye eneo la mapango. Wakati mwingine badala ya moto tuliona moshi mkubwa.
“Kumbe wanajeshi wetu nao walishafika kupambana na hao watu,” alisema Simeon Patrick, mkazi wa Kitongoji cha Karasha, Amboni.
INAVYODAIWA
Habari zilizosambaa juzi, zinadaiwa kundi hilo lililopambana na askari ni la kigaidi ambapo safari yao kubwa ilikuwa kwenda kufanya ugaidi wa kumwaga damu nchi jirani ya Kenya.
Moja ya Zana ya kivita ya Polisi ikiwa kazini kubambana na matukio ya uhalifu.
Wale jamaa nasikia walikuwa wakipeleka vifaa nchini Kenya eneo la mwambao ili waje wafanye uhalifu baadaye.
“Sasa wakiwa katika hatua za mwisho mwisho baada ya kupeleka silaha za kivita, wakashtukiwa. Ikabidi waache silala zao eneo walipozificha na wao waje Tanga kujificha kwenye mapango.
“Lengo lao, watulie mpaka hali kule Kenya itakapokuwa imepoa ndipo wajitokeze. Sasa kilichotokea ni kwamba, wakati wanaishi mapangoni ilibidi waanze kutoka kutafuta chakula kwa kufanya uhalifu mdogomdogo ndipo siku moja jamaa yao mmoja akakamatwa kwa uhalifu.
“Yule jamaa ndiye aliyewapeleka polisi walipo wenzake na kutokea kwa mapigano makali kama yale,” alisema mtoa habari mmoja huku akiomba jina lake lihifadhiwe.
WANACHOAMINI WANANCHI, TOFAUTI NA POLISI
Uwazi lilibahatika kuzungumza na baadhi ya wananchi wa jijini Tanga ambapo karibu wote walikuwa na mtazamo mmoja tu.
“Kutuambia wale ni majambazi si sawasawa. Majambazi wetu tunawajua, polisi wanawatosha sana, sasa hawa wametokea wapi mpaka JWTZ washirikishwe?” alihoji Paulina Mathias, mkazi wa Chumbageni, Tanga.
Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja.
Kusema ukweli serikali ituambie moja. Lakini wale si majambazi. Kwanza mpaka leo hii (juzi) hawajamkamata hata mmoja zaidi ya kujeruhi askari wetu na kumuua mmoja. Wale ni magaidi, lazima tuwe makini sana,” alisema Ally, mkazi wa Duga Maforoni, Tanga.
KUHUSU VIDEO MPYA
Tukiachana na mapigano ya Amboni, sasa turudi kwenye video mpya ya watu waliojiita ni watetezi wa haki dhidi ya udhalimu.
Video hii ipo ndani ya mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo wanaonekana watu wawili wakiwa wamevaa mavazi ya kininja ili wasijulikane.
Watu hao wanasema wanapinga jamii yao kukamatwa na kuuawa mara kwa mara wakidai jeshi linawaonea hivyo kutangaza kupambana na askari.
Video hiyo haipishani sana na ile iliyotangulia kuandikwa kwenye gazeti ndugu na hili la Ijumaa.
KAULI YA JESHI LA POLISI
Akizungumza na Uwazi jijini Tanga muda mfupi baada ya kutulia kwa mapambano ya Amboni, Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja aliwataka wananchi kutulia na kuendelea na shughuli zao za kawaida huku akisisitiza:
“Askari walifika mapangoni, kundi lile ni la majambazi. Lilianza kufanya mashambulizi ya risasi na katika majibizano,  askari sita walijeruhiwa na kuwahishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo,” amesema Kamishna Chagonja.      
GPL

VIDEO YA WASANII TUNDA NA STANI WAKIFANYA MAP3NZI YAVUJA....


Aibu! Mrembo anayeuza nyago (video queen) kwenye video kibao za wasanii wa Bongo Fleva, Tunda Sabasitana na mchekeshaji maarufu Bongo, Stan Bakora wamepiga picha za ng0n0 kisha kusambaa hadi kulifikia deski la Ijumaa Wikienda. 

Mrembo anayeuza nyago (video queen) kwenye video kibao za wasanii wa Bongo Fleva, Tunda Sabasitana na mchekeshaji maarufu Bongo, Stan Bakora wakijiachia.
Picha hizo chafu zilitua mezani kwetu wikiendi iliyopita ikiwa ni siku mahususi kwa wapendanao.
Picha hizo zinawaonesha wawili hao wakiwa kwenye ‘bedi’ huku wakifanya yao.

Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa Stan na Tunda, wawili hao wemekuwa kwenye ‘malovee’ siku nyingi na kupiga picha za ngono kwao si ishu maana wote hawana mshipa wa aibu kwa kuwa ni wasanii.

Ilisemekana kwamba tangu Stan aanze kuigiza amekuwa akifanya mambo ya aibu tofauti na jinsi anavyoonekana.
 
Source: GPL

SKENDO NZIMA YA STARA THOMAS KUFUMANIWA NA MUMEWE HII HAPA



Staa wa Bongo Fleva, Stara Thomas akiwa na mumewe.
Stori: Deogratius Mongela na Chande  
HAYA ni madai mazito! Kwamba, staa wa Bongo Fleva ambaye juzi kati alinusa kwenye gospo ‘ikamshinda', Stara Thomas anadaiwa kufumaniwa na mumewe, Raumu Ally mpaka kufikishana polisi, Risasi Jumamosi halipitwagi na ‘ubuyu’. 
Kwa mujibu wa shuhuda wa kuaminika, tukio hili lilijiri hivi karibuni nyumbani kwa familia hiyo, Tabata jijini Dar es Salaam.

FUMANIZI LILIVYOTOKEA
Akilisimulia Risasi Jumamosi baada ya kuulizwa kama kweli fumanizi lilikuwepo, mume wa Stara alifunguka hivi: “Ni kweli ilitokea. Siku ya fumanizi nilikuwa nimesafiri, lakini nikarudi ghafla bila kumpa taarifa mke wangu.
“Nilikuwa nyumbani, yeye hakuwepo. Saa 9:00 usiku ndiyo nilimwona Stara akirejea tena akiwa amelewa. Aliletwa na gari mpaka nje ya nyumba.” 
NDANI YA GARI KWA NUSU SAA
“Lile gari lilisimama zaidi ya nusu nje bila kushuka mtu ndipo nikaamua kulifuata. Stara aliponiona akamwambia dereva ambaye najua ni jamaa yake, aondoe gari kwani mimi ni mume wake nitampiga.
“Nilizuia wasitoke, yule jamaa akarudi nyuma na kuniparuza kwenye mguu na tairi, nikadondoka. Niliposimama nikaokota jiwe na kulirushia gari nikavunja kioo cha mbele.” 
STARA, JAMAA POLISI
Mume huyo anaendelea kusimulia: “Baada ya hapo Stara aliondoka na yule jamaa mpaka Kituo cha Polisi Tabata ambapo walinishtaki. Niliitwa polisi kwa madai ya uharibifu wa kioo.
“Kwa vile nilikuwa nasafiri kwenda nje ya nchi (ni dereva wa malori) niliona mambo yaishie pale kituoni, nilikwenda nikachukuliwa maelezo kisha nikalipa shilingi laki saba (700,000).”
Mume wa Stara Thomas Raumu Ally. DALILI ZA KUVUNJIKA KWA HESHIMA
Habari zaidi zilidai kwamba, wawili hao wamekuwa kwenye ugomvi wa mara kwa mara.
Imeelezwa kwamba, ugomvi wao ulianza pale Raumu aliposhindwa kulipa ada ya shilingi laki tano ya mtoto wa Stara (jina tunalo) huku madai ya mchepuko nayo yakisambaa hali iliyokuwa ikishusha heshima ya familia. 
TUJIUNGE NA RAUMU 
Akifafanua kuwepo kwa sakata hilo pamoja na chanzo kizima, Raumu alisema kuwa Stara amekuwa akimfanyia vituko na mambo ya ajabu tangu aliposimamishwa kazi kwenye kampuni aliyokuwa akifanyia awali (jina kapuni) baada ya kutokea matatizo. “Mimi ni dereva wa malori, nakwenda Lusaka (Zambia) na Congo (DR), nimekuwa na mgogoro na Stara baada ya kusimamishwa kazi. Unajua ukiwa huna kazi hata fedha huna. Alitaka nimlipie ada ya laki tano mtoto wake lakini nikawa sina, ikawa maneno.” 
KUMBE KUNA MENGINE ZAIDI
“Huwezi kuamini ndugu zangu wamenitenga mimi kwa sababu wakati naanza kuishi na Stara nilibadili dini yangu ya Kiislam na kumfuata yeye kwenye ulokole (wakati huo) halafu leo hii ananiletea mambo ya ajabu! Stara amuogope Mungu.” 
WALIKUTANA HIVI 
Akizungumzia historia fupi ya uhusiano wao, Raumu alisema walikutana kwa mara ya kwanza, Stara alikuwa akisoma Shule ya Sekondari ya Mzizima, Dar, miaka ya 90.
Stara Thomas. MAP3NZI MOTOMOTO
Map3nzi yao yalikuwa motomoto lakini baadaye walipotezana kisha kuja kuonana tena miaka ya hivi karibuni huku kila mmoja akiwa na maisha yake.
Kutokana na namna walivyopendana kupita kiasi kipindi cha awali, wawili hao walirejesha uhusiano ambapo mwanaume huyo alihamia nyumbani kwa Stara, Tabata baada ya staa huyo kuachana na mumewe wa ndoa aliyezaa naye watoto wawili. 
STARA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Stara ili kujibu tuhuma hizo ambapo alipopatikana mahojiano yalikuwa hivi:
Mwandishi: Haloo Stara…
Stara: Haloo.
Mwandishi: Unamfahamu Raumu?
Stara: Kwanza wewe nani? 
Mwandishi: Mimi ni mwandishi wa Global Publishers.
Stara: Ndiyo namjua Raumu. 
Mwandishi: Ni nani kwako? 
Stara: Ukitaka kujua kuhusu Raumu, njoo nyumbani tuongee.
Mwandishi: Nataka unijibu kuhusiana na tuhuma za yeye kukufumania.
Stara: Njoo nyumbani wewe na Raumu tuongee tuyamalize huku.
Hata hivyo, mwandishi wetu alitinga nyumbani kwa staa huyo lakini hakumpata hadi gazeti hili linakwenda mitamboni.

SIKU 3 ZA SEGEREA ZILIVYOMTIA DOA MREMBO HUYU WA BONGO MOVIES


Mwigizaji wa toka kitambo, Davina Yahaya ‘Davina’, amesema kamwe hatokuja kusahau mateso aliyowahi kuyapata akiwa Gereza la Segerea ambapo alikaa kwa siku tatu.
Akipiga stori na GPL, Davina alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa mwaka 2012 ambapo ilikuwa ni tatizo la kifamilia lililosababisha kutupiwa huko japokuwa hakuweza kuliweka hadharani kwakuwa bado lipo mikononi mwa sheria.
“Huwa natokwa machozi na kamwe sitokuja kusahau mateso niliyoyapata Segerea. Nilikuwa kwa siku tatu lakini niliona kama mwezi, hali ya hewa, sehemu ya kulala zilikuwa mbaya sana, wingi wa watu na sikupata hata nafasi ya kulala zaidi ya kukesha nikilia,” alisema Davina.

WEMA AMCHAMBA KING LAWRANCE KWA KUVUJISHA PICHA ZAKE NA MEMU WA ZARI THE BOSS LADY


Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’.
KIMENUKA! Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ amemporomoshea matusi mazito shemeji wa Zarina Hassan ‘Zari’, King Lauwrance akidai amemuudhi sana kwa kitendo cha kuvujisha picha inayomuonesha akiponda raha nchini Afrika Kusini ‘Sauz’ na mume wa Zari, Ivan Semwanga, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Wema na staa wa Bongo Fleva, Omari Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ walikwenda Sauz kurekodi video ya wimbo wa msanii huyo ambao jina lake bado halijafahamika mara moja ndipo baadae picha ya Ivan, Wema na King Lawrence ilipovuja na kuzua gumzo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichokuwa Sauz, baada ya Wema na Ommy kutua nchini humo na ‘project’ hiyo ya video, King Lawrance alidaiwa kuandaa mpango kabambe wa kuhakikisha kwa namna yoyote wanaonana na Wema kisha kupiga naye picha ambayo akiivujisha mtandaoni kila mtu ataamini wamefanya malipizi kwa zilipendwa wa Wema, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambaye amemnyakua Zari, mke wa Ivan.
“Ilikuwa ni mpango wa malipizi, King na Ivan walikuwa wanaumia moyoni kumuona Diamond anatoka na Zari wakati wao wana fedha kuliko Diamond hivyo waliposikia mtoto wa kike (Wema) yupo Sauz wakasema watadili naye hadi kieleweke, iwe ni kwa kufanikisha zoezi la kutoka naye kimapenzi au hata kupiga picha ambazo zikisambaa mitandaoni, watu watajua kwamba wamefanya malipizi,” kilisema chanzo chetu.

MAPYA YAIBUKA KESI YA MUME KUMCHINJA MKEWE KAMA KUKU GUEST



Na Makongoro Oging’/Uwazi
SIKU chache zimepita tangu Remy Joseph,
35, (pichani) kudaiwa kumuua kwa
kumchinja na kisu mkewe, Josephine Mushi
kwenye Hoteli ya Friends Corner iliyopo
Manzese jijini Dar, mengine yamebainika,
Uwazi limechimba zaidi.
Taarifa kutoka vyanzo vya habari hotelini
hapo zinadai kuwa, saa tano asubuhi ya
Januari 23, mwaka huu, mwanamume huyo
alifika kwenye hoteli hiyo na kufanya
sherehe ya kuzaliwa kwake ‘bethidei’
ambapo alikuwa akitimiza miaka 35.
Mmoja wa wahudumu wa hoteli hiyo
ambaye hakupenda jina lake liandikwe
gazetini alisema siku hiyo mtuhumiwa huyo
alifika akiwa na mwanamke mweupe (jina
halikupatikana) ambaye wahudumu wote
walijua ndiye mke wake kutokana na kuwa
mstari wa mbele katika shamrashamra
hiyo.“Sisi tulimuona ni kijana mstaarabu na
haya ya mauaji yasingetokea, lakini kumbe
alikuwa akisherehekea huku akijua atamuua
mkewe siku si nyingi mbele tena kwenye
hoteli hiihii, kwa kweli imetushangaza
sana,” alisema mhudumu huyo.
Uwazi lilimtafuta mkurugenzi wa hoteli hiyo
aliyejitambulisha kwa jina moja la Massawe
ambapo alikiri kupata taarifa ya sherehe
hiyo kutoka kwa wahudumu wake lakini
hakujua alichodhamiria mtuhumiwa huyo
mpaka mauaji yalipofanyika na kubainika
kuwa, kumbe ni yeye aliyekuwa ameandaa
sherehe
Joseph alikutwa na polisi katika chumba
kimoja cha hoteli hiyo akiwa na kisu
mkononi muda mfupi baada ya kumchinja
mkewe wake na yeye kutaka kujiua lakini
akashindwa.
Ilidaiwa kuwa, Joseph alipanga hotelini hapo
Januari 28, mwaka huu huku akiwa na
mkewe huyo lakini siku ya pili wahudumu
waliona damu zikitiririka kutoka chumbani
kupitia mlangoni. Waliita polisi na
walipofika walibaini kufanyika kwa mauaji
hayo ya kinyama.
Mtuhumiwa bado yupo Hospitali ya Taifa
Muhimbili kwa matibabu chini ya ulinzi
mkali wa polisi huku mkewe akizikwa Moshi,
Februari Mosi mwaka huu

WALIOFARIKI KUTOKANA NA EBOLA NI 8,795 - WHO.

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limetoa takwimu mpya za ugonjwa wa Ebola ambapo mpaka sasa watu 8,795 wamefariki huku 22,057 duniani kote wakiwa wameambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
Katika takwimu hizo, nchi ya Sierra Leone ina jumla ya watu 10,518 wenye virusi vya Ebola, Liberia watu 8,622 na Guinea 2,917.
Nchi nyingine ambazo maambukizi yake yapo chini ni Nigeria yenye maambukizi ya watu 20 huku vifo vya watu nane vikiripotiwa, Mali maambukizi ya watu nane huku waliokufa wakiwa sita. Marekani yenye maambukizi ya watu wanne huku mmoja akifariki.
Senegal, Hispania na Uingereza kila moja ina mtu mmoja…
SHIRIKA la Afya Duniani (WHO), limetoa takwimu mpya za ugonjwa wa Ebola ambapo mpaka sasa watu 8,795 wamefariki huku 22,057 duniani kote wakiwa wameambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
Katika takwimu hizo, nchi ya Sierra Leone ina jumla ya watu 10,518 wenye virusi vya Ebola, Liberia watu 8,622 na Guinea 2,917.
Nchi nyingine ambazo maambukizi yake yapo chini ni Nigeria yenye maambukizi ya watu 20 huku vifo vya watu nane vikiripotiwa, Mali maambukizi ya watu nane huku waliokufa wakiwa sita. Marekani yenye maambukizi ya watu wanne huku mmoja akifariki.
Senegal, Hispania na Uingereza kila moja ina mtu mmoja aliyeambukizwa huku zikiwa hazina vifo.
Liberia ndiyo nchi inayoongoza kwa vifo ambapo watu 3,686 wamefariki, huku Sierra Leone ikiwa na vifo 3,199 wakati Guinea ikiripotiwa kuwa na vifo 1,910.



Maambukizi ya ugonjwa wa Ebola yamepungua kwa sasa tangu yalipoanza mwezi Machi 2014 huku baadhi ya wataalamu wakieleza kuwa ugonjwa huo unaweza kuwa umetokomezwa kabisa ifikapo Mwezi Juni mwaka huu.

ALICHOKISEMA LULU KUHUSIANA NA MISS TANZANIA KUSHINDA TAJI LA MISS WORLD


MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael 'Lulu' amendika katika Instagram kuwa mshiriki wa Tanzania kwenye Miss World, Happiness Watimanywa akishinda atabadilisha jina na kuitwa…
Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael 'Lulu'.

MZAZI WA BINTI AANZISHA VARANGATI BAADA YA KUFUMANIWA MWANAE AKICHEZEWE KWENYE SCENE YA MAHABA


Baba mmoja ambaye jina halikupatikana mara ameshusha kichapo kwa wasanii ambao ni maprodyuza waliokuwa wakimchezesha mwanaye filamu bila ridhaa yake.
Baba huyo akizuiwa ili asiendelee kushusha kichapo hicho.
Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilijiri juzikati, maeneo  ya Mwananyamala-Komakoma jijini Dar ambapo awali binti huyo ambaye ni msanii chipukizi wa kuigiza aitwaye Jeniffer alidaiwa kupigwa mkwara na baba yake kuwa asijishughulishe na masuala ya muvi na badala yake ajikite kwenye masomo yake kufuatia tasnia hiyo kuhusishwa na skendo za ng0no.
Ilidaiwa kwamba, Jeniffer alikaidi amri ya mzee wake huyo na kwenda kinyemela kurekodi vipande kadhaa vya muvi ya kikundi chao ambapo taarifa zilimfikia baba yake huyo na kuamua kutimba lokesheni.
Baba huyo akijiandaa kumvaa prodyuza huyo.
Ilisemekana kwamba, katika hali iliyompandisha zaidi hasira, mzee huyo alipofika maeneo hayo alimkuta mwanaye katikati ya ‘scene’ ya mahaba aliyokuwa akiigiza na msanii anayetamba kwenye Tamthiliya ya Siri ya Mtungi, Daudi Michael almaarufu Duma.
Baada kushuhudia bintiye ‘akigaragazwa’ kimahaba, mzazi huyo alimvaa msanii Duma na kumshutumu kumharibia binti yake ambapo alimpa kibano pamoja na maprodyusza wenzake kabla ya kuamuliwa na wasanii wengine waliokuwepo eneo hilo.
Watu waliokwepo kwenye sakata hilo wakiamulizia.
Ilidaiwa kwamba, alipoona amewakungung’uta vya kutosha, baba huyo aliondoka na bintiye akiahidi kwenda ‘kumsulubu’ nyumbani kwa kuwa amekuwa sikio la kufa.
Kwa upande wake, Duma alibaki na majeraha mgongoni ambayo hadi waandishi wetu wanafika eneo la tukio yalikuwa yakitoka damu.
Duma alipoulizwa kuhusiana na mzee huyo, alikana kumfahamu na kudai kuwa alipewa mamlaka ya kumtumia binti huyo kwenye muvi na kaka wa msichana huyo.
Baba huyo akiondoka na binti yake.
“Nilimuomba Jeniffer kwa kaka yake na alikubali nishuti naye, sasa sijui nitafanyaje maana tulishashuti scene kibao halafu Jeniffer kashindwa kumalizia,” alisema Duma.

MISS TANZANIA KUTOPOKONYWA ZAWADI BAADA YA KUJIVUA TAJI

Mkurugenzi wa LINO International Agency ambao ni waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga amesema miongoni mwa maswali aliyokutana nayo kwa wingi jana kwenye ‘Kikaangoni’ ya EATV, ni pamoja na swala la Sitti Mtemvu kama atanyang’anywa zawadi alizopewa ili akabidhiwe aliyevishwa taji hilo baada ya yeye kujivua.“Kwanza hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania mtu kujivua taji, na kwenye kanuni zetu haikuelezwa wazi wazi kwamba mtu akivua taji tunachukua zawadi tunamkabidhi mtu mwingine ama hivyo,” Lundenga ameiambia E-Newz ya EATV.Lundenga amesema kuwa Sitti hatanyang’anywa zawadi kwasababu hakuvuliwa taji bali alijivua mwenyewe.

“lakini bado tuna majadiliano na wadau wetu masponsors tuangalie namna ya kufanya, kama kuna zawadi zimebaki atapewa lakini zawadi ambazo amepewa nafikiri hataweza kurudisha kwasababu hakuvuliwa, kama tungemvua kwa makosa angeweza kurudisha lakini hatujamvua kajivua mwenyewe”.

Zawadi iliyotolewa mwaka huu kwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 ni shilingi milioni 18

PENNY APIGA KELELE ZA UCHUNGU BARABARANI



Prizenta wa Kituo cha Radio E-FM cha jijini Dar, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ anadaiwa kukumbwa na mauzauza yaliyodaiwa ni mapepo na kujikuta akipiga makelele barabarani.


Habari kutoka kwa shuhuda wetu zilidai kwamba, ishu hiyo ilijiri maeneo ya Makongo jijini Dar es Salaam, juzikati wakati staa huyo akielekea msibani ambapo rafiki yake kipenz aitwaye Skitter alifariki dunia.

Chanzo hicho kilidai kwamba Penny alikuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kawaida, alipofika maeneo hayo aliegesha gari pembeni na kuanza kupiga kelele akilia kwa uchungu hivyo kuwaacha watu waliomshuhudia wakiwa midomo wazi wakitaka kujua kilichompata mtangazaji huyo. Mpashaji wetu huyo alizidi kueleza kwamba baada ya kama  dakika kumi, Penny aliondoa gari na kuendelea na safari.

Paparazi wetu aliponyetishiwa ishu hiyo alimtafuta Penny na kumuuliza kuhusu tukio hilo ambapo alisema alikuwa akienda kwenye msiba wa rafiki yake, alipokaribia kufika alipata uchungu ndiyo akatokewa na hali hiyo

WEMA SEPETU ATHIBITHISHA KUACHANA NA DIAMOND PLATNUMZ


MISS Tanzania 2006/07 ambaye ni staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’, amevunja ukimya kwa kuamua kuanika kisa cha yeye kummwaga aliyekuwa mwandani wake, nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Miss Tanzania 2006/07 ambaye ni staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akipozi..
Akizungumza na Amani katika mahojiano maalum jijini Dar, juzikati, Wema alianza kwa kufunguka kwamba, kuna watu wamekuwa wakizungumzia ishu ya yeye kumtema Diamond huku kisa wakiwa hawakijui na wengine wamehamishia sababu kwa nyota wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’, jambo ambalo si kweli.
Wema alimwaga ‘ubuyu’ kwamba, yeye ameamua kumpa likizo ndefu Diamond ili kila mmoja aweze kufanya mambo yake ya maana kwa uhuru mkubwa hasa baada ya jamaa huyo kunukuliwa na magazeti pendwa akisema hana mpango wa kuoa jambo ambalo lilimkatisha tamaa na kumwacha njia panda.
SAFARI YAKE CHINA NAYO TATIZO
Kuhusu suala la kusema amempa likizo ndefu ili kila mtu afanye mambo yake,
Wema alirejea safari yake ya China hivi karibuni ambapo Diamond hakutaka asafiri ila akalazimisha. Hapo aliona anatakiwa kuwa huru zaidi.
Wema Isaac Sepetu  akipozi kimahaba na 'Diamond Platinumz'.
MWISHO WA LIKIZO
Wema alipotakiwa kutaja mwisho wa likizo hiyo endapo ni ya siku 28  kama ilivyo
kwa sheria ya kazi ya Tanzania, aligoma kusema chochote huku akisisitiza amempa likizo Diamond.
AMZUNGUMZIA ZARI
Staa huyo asiyekaukiwa na matukio, alikwenda mbele zaidi kwa kumzungumzia Zari ambapo alisema kuna wanaodai mwanamuziki huyo tajiri yuko kimapenzi na Diamond, lakini yeye haoni ukweli wowote kwani anajua wawili hao wana ‘projekti’ ambayo ni mawazo ya muda mrefu.
BOFYA HAPA KUMSIKIA WEMA
“Kwanza naomba watu wajue kuwa, projekti ya Diamond na Zari ninaijua na bahati nzuri Zari ni shoga‘ngu tangu kitambo hivyo yote yanayofanyika mimi nayatambua hatua kwa hatua pamoja na kwamba sijaongea na Diamond siku nyingi,” alisema Wema.
Diamond akiwa na Wema Isaac Sepetu siku ya bethidei yake.
DIAMOND AULIZWA KAMA ANAITAMBUA LIKIZO NDEFU
Baada ya mazungumzo na Wema, mwanahabari wetu alimtafuta Diamond kwa lengo la kutaka kumfahamisha kama anafahamu kwamba amepewa likizo ndefu.
“Dah! Nashindwa niseme nini hapo! Lakini ujue maisha kila mfa maji siku zote haishi kutapatapa, kiukweli mimi hapo naona Wema anatoa majibu ya kisiasa tu.
“Nashindwa kujibu kila linalosemwa na watu ila kuna kipindi mtu hutakiwi kujibu kila kitu. Kuna mambo mengine yanatakiwa uyaache yapite tu.
“Mimi nimeachwa na Wema, Zari ni rafiki yangu tu, acheni projekti iendelee,” alisema Diamond huku akichekacheka kwa ishara ya furaha akijiandaa kuachia ngoma kali mpya iitwayo ‘Nitampata Wapi’ leo.
Hii ni picha ya mwisho ya wawili hao kuonekana pamoja.
KWENYE WHATSAPP
Wakati Diamond akisema hayo, baadaye kwenye maelezo yake mafupi (profile) ya WhatsApp aliweka picha ya Zari huku akiambatanisha na maneno yaliyosomeka:
“Unapokosa usisikitike, Mwenyezi Mungu kakuandalia kizuri zaidi.”
Wema na Diamond wamekuwa na kasumba ya kuachana na kurudiana hivyo kuna kila dalili wawili hao wakarudiana tena.

KUMBE SHERRY ALIMTAJA MAINDA KABLA SAFARI YAKE YA MWISHO....


MSANII aliyefariki dunia hivi karibuni mjini Morogoro, Sherry Magali, anadaiwa kuwa alikuwa akilitaja jina la Ruth Suka ‘Mainda’ kila mara hadi alipofikwa na umauti.
Marehemu Sherry Magali enzi za uhai wake.
Chanzo chetu makini kilichokuwa karibu na msanii huyo wa filamu, kinasema Sherry alianza kugoma kula akidai hadi amuone msanii mwenzake huyo ambaye alikuwa jijini Dar es Salaam anakoishi.
Msanii wa 'Bongo Movie' Ruth Suka (Mainda) akiwa katika pozi.
Mpashaji huyo alisema hata siku aliyofariki pia alilitaja jina hilo, kitendo kilichowaumiza sana baadhi ya ndugu na marafiki. Mainda ambaye alikuwa ni rafiki wa marehemu, alikiri kusikia jambo hilo na anasikitika kwamba siku aliyopanga kwenda, ndiyo ambayo mwenzake alifariki.

GARI LAPINDUKA KATIKA HARAKATI ZA KUWAKIMBIA ASKARI



Baadhi ya wakazi wa mji wa Moshi wakiangalia kwa mshangao gari aina ya Toyota Spacio lenye namba za usajili T111 BHW likiwa limepinduka chini juu mbele ya ofisi za TFA barabara ya Boma, Moshi jirani kabisa na mnara wa saa.Dereva wa gari hilo anadaiwa alikuwa akijaribu kuwakimbia askari wa kikosi cha barabarani kwa mwendo wa kasi kabla ya kugonga gari jingine na hatimaye kupinduka hakuna aliepoteza maisha kwenye tukio hilo la ajali.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga