Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » » » MISS TANZANIA KUTOPOKONYWA ZAWADI BAADA YA KUJIVUA TAJI

Mkurugenzi wa LINO International Agency ambao ni waandaaji wa mashindano ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga amesema miongoni mwa maswali aliyokutana nayo kwa wingi jana kwenye ‘Kikaangoni’ ya EATV, ni pamoja na swala la Sitti Mtemvu kama atanyang’anywa zawadi alizopewa ili akabidhiwe aliyevishwa taji hilo baada ya yeye kujivua.“Kwanza hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania mtu kujivua taji, na kwenye kanuni zetu haikuelezwa wazi wazi kwamba mtu akivua taji tunachukua zawadi tunamkabidhi mtu mwingine ama hivyo,” Lundenga ameiambia E-Newz ya EATV.Lundenga amesema kuwa Sitti hatanyang’anywa zawadi kwasababu hakuvuliwa taji bali alijivua mwenyewe.

“lakini bado tuna majadiliano na wadau wetu masponsors tuangalie namna ya kufanya, kama kuna zawadi zimebaki atapewa lakini zawadi ambazo amepewa nafikiri hataweza kurudisha kwasababu hakuvuliwa, kama tungemvua kwa makosa angeweza kurudisha lakini hatujamvua kajivua mwenyewe”.

Zawadi iliyotolewa mwaka huu kwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 ni shilingi milioni 18

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga