Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

BANDAWE BADO ANAMKUBALI ROSE NDAUKA, JAPO WAMESHA ACHANA.


MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Malick Bandawe ambaye sasa anatamba na wimbo wake wa Tucheze amefunguka kwa mara ya kwanza kuwa tangu atengane na mzazi mwenziye, Rose Ndauka bado hajatokea wa kumtetemesha.
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Malick Bandawe.
Akizungumza na Ijumaa juzikati, Malick alisema kuwa huko nyuma alipomuona Rose alimtetemesha na kuamua kuingia mzimamzima mpaka kufikia hatua ya kupata naye mtoto lakini mpaka sasa hajatokea kama yeye.

Rose Ndauka.
“Unajua mambo yanapotokea lazima kukubaliana nayo na huwezi kulazimisha. Tangu uhusiano wetu usambaratike, hajatokea kama Rose,” alisema Malick.

MUME WA ROSE NDAUKA AMWACHA MSANII HUO AISHI ATAKAVYO



BAADA ya msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka kuonekana akijiachia viwanja mbalimbali tofauti na alivyokuwa akiishi awali, mzazi mwenzake, Malick Bandawe, ameibuka na kumfungukia kuwa aachwe ajirushe.
Malick Bandawe.
Malick alifungua kinywa kufuatia madai kwamba alipokuwa akiishi na Rose alikuwa akimpa sheria kali na kumkataza kwenda ‘out’ ndiyo maana alikuwa hajiachii kama ilivyo sasa na hiyo ni moja ya sababu zilizosababisha uhusiano wao kuvunjika.
“Mimi siyo mkali wala sina sheria hizo ninazoambiwa ila nilikuwa nachukua muda mwingi sana kuzungumza na Rose na ninaamini amejifunza mengi sana mazuri ambayo akiyazingatia yatamsaidia maishani.
Msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka.
“Sababu za Rose kujiachia hivyo ni kutokana na maisha ambayo tulikuwa tunaishi hivyo anahitaji muda atatulia na atakuwa sawa na hapo ndipo atakapoanza kuyafanyia kazi yale mazuri aliyoyapata kutoka kwangu, sitegemei yeye kufanya mabaya ila nategemea afanye mazuri kwa ajili ya mtoto wetu,”alisema Malick.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga