Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » » » WEMA AMCHAMBA KING LAWRANCE KWA KUVUJISHA PICHA ZAKE NA MEMU WA ZARI THE BOSS LADY


Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’.
KIMENUKA! Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ amemporomoshea matusi mazito shemeji wa Zarina Hassan ‘Zari’, King Lauwrance akidai amemuudhi sana kwa kitendo cha kuvujisha picha inayomuonesha akiponda raha nchini Afrika Kusini ‘Sauz’ na mume wa Zari, Ivan Semwanga, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Wema na staa wa Bongo Fleva, Omari Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ walikwenda Sauz kurekodi video ya wimbo wa msanii huyo ambao jina lake bado halijafahamika mara moja ndipo baadae picha ya Ivan, Wema na King Lawrence ilipovuja na kuzua gumzo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kilichokuwa Sauz, baada ya Wema na Ommy kutua nchini humo na ‘project’ hiyo ya video, King Lawrance alidaiwa kuandaa mpango kabambe wa kuhakikisha kwa namna yoyote wanaonana na Wema kisha kupiga naye picha ambayo akiivujisha mtandaoni kila mtu ataamini wamefanya malipizi kwa zilipendwa wa Wema, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambaye amemnyakua Zari, mke wa Ivan.
“Ilikuwa ni mpango wa malipizi, King na Ivan walikuwa wanaumia moyoni kumuona Diamond anatoka na Zari wakati wao wana fedha kuliko Diamond hivyo waliposikia mtoto wa kike (Wema) yupo Sauz wakasema watadili naye hadi kieleweke, iwe ni kwa kufanikisha zoezi la kutoka naye kimapenzi au hata kupiga picha ambazo zikisambaa mitandaoni, watu watajua kwamba wamefanya malipizi,” kilisema chanzo chetu.

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga