Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » Rais wa Madagascar awasili Nchini, Kujadili kuhusu mgogoro wa amani wa kisiwa hicho.


Dar es Salaam. Rais wa Serikali ya Mpito ya Madagascar, Andry Rajoelina amewasili nchini kwa ziara ya kikazi na jana alitarajiwa kuwa na mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete.
Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Rais Rajoelina alilakiwa na Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC-Troika) ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).
Katika nafasi yake ya Mwenyekiti wa asasi hiyo, Rais Kikwete ndiye aliyepewa jukumu na viongozi wenzake wa nchi wanachama wa SADC, kutafuta suluhisho la mgogoro wa kisiasa katika Kisiwa cha Madagascar.
Viongozi hao wawili walikutana Ikulu, kuzungumzia hali ya kisiasa nchini Madagascar ambapo Rais Kikwete alimweleza Rais Rajoelina matokeo ya kikao cha wakuu wa nchi wanachama wa SADC-Troika, kilichofanyika chini ya uenyekiti wake, Jumamosi usiku, mjini Pretoria, Afrika Kusini.


CHANZO:MWANANCHI

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga