Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » ANGALIA KEKI YA KUSUTWA ALIYOPEWA PENNY, KISA KIKIWA NI MABWANA WA WATU


KATIKA staili ya aina yake ya kuuaga mwaka na kuukaribisha 2014, mtangazaji Peniela Mungilwa ‘Penny’, ambaye ni zilipendwa wa Nasib Abdul ‘Diamond’ alipewa zawadi ikiwemo keki yenye maandishi ya kumsuta.
Peniela Mungilwa ‘Penny’.
Tukio hilo la aina yake lilitokea Jumatano hii nyumbani kwake Mwananyamala Mwinjuma alikohamia hivi karibuni, baada ya watu wanaosadikika kuwa ni wadau wa Wema Sepetu, kufika hapo wakiwa na ‘mzigo’ huo uliojumuisha pia kadi, shampeni na maua.
Mmoja wa wapangaji wa nyumba anayoishi Penny, aliliambia gazeti hili kuwa msafara wa magari matatu ulifika hapo na kugonga mlango wakimuulizia mtangazaji huyo wa kituo cha televisheni cha Channel Ten.
“Walivyofika sisi tulijua labda leo ni bethidei ya Penny, maana tuliwaona wakiwa na maua, keki, shampeni na kadi, walipomuulizia tukawaambia ametoka, wakaacha mzigo huo wakisema apewe atakaporudi,” alisema shuhuda huyo.
Juu ya Keki iliyopelekwa kwa mtangazaji huyo kulikuwa na maandishi yaliyomsuta na kumtaka kuachana na tabia ya kuchukua mabwana wa rafiki zake pamoja na dada zake, hali inayoonyesha kuwa waliompelekea ujumbe huo ni wabaya wake.
Juhudi za kumtafuta Penny kuzungumzia tukio hilo hazikuweza kuzaa matunda hadi gazeti hili linakwenda mtamboni.

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga