Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » BOTI YA KILIMANJARO 2 ILIYONUSURIKA KUZAMA KATIKA MKONDO WA NUNGWI PEMBA YAWASILI ZANZIBAR SALAMA.


Kwa mujibu wa Abiria waliohojiwa wanasema Boti ya Kilimanjaro II ikitokea Pemba kuelekea Unguja imepigwa na dhoruba leo Jan 5 2014 kwenye saa nne asubuhi na kuponea kuzama ilipokua kwenye eneo hatari la Nungwi ambapo ilizama kidogo mbele na kunyanyuka hivyo watu wa mbele wote wakaachwa lakini pamoja na kuwatupa hao watu kwenye maji Nahodha akafanya uamuzi mwingine mgumu.
clip_image001Aliona akisimama ili kuwaokoa wale watu boti yote ingezama pale hivyo akaamua kuendelea na safari lakini kabla ya kuondoka watu kadhaa ndani ya boti wakajitolea kuwatupia life jacket wale waliotupwa kwenye maji ambapo shuhuda anasema kama mtu hajui kuogelea anaweza kupoteza maisha kwa sababu hawakua wamejiandaa kwenye tukio hili la ghafla na sio wote wamepata vifaa hivyo vya kujiokoa.
clip_image001[6]Shuhuda mmoja anasema ‘yani boti ilizama ghafla mbele hivyo watu wakatupwa kwenye maji kwenye hii sehemu ambayo kuna mkondo wa maji, upepo ulikua mkali sana yani unaona watu wanajaribu kujiokoa mabegi na vitu vingine vinaonekana juu ya maji’
Hali ilivyo ndani ya boti ambayo imeendelea na safari ni watu kujawa na huzuni na wengine wamebaki wanalia tu.
KAULI YA POLISI KUHUSU TAARIFA YA ABIRIA 10 WALIOTUPWA MAJINI
Kuhusu taarifa za watu 10 kurushwa baharini wakati upepo mkali ulipotokea, Polisi wanasema ‘hakuna mtu yeyote aliedondoka baharini na hizi taarifa ni kwa mujibu wa Captain wa boti hii N. Abubakar’

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga