Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

Diamond Azidi Kuwakera Mashabiki wake Majuu, Ashindwa kutokea katika Shoo Uingereza.


Mwanamuziki Diamond Platnumz kwa mara nyingine tena usiku wa kuamkia jana alisababisha vurugu kubwa nchini Uingereza baada ya kushindwa kutumbuiza katika ukumbi wa LaFace Club uliopo jijini London.

Hii ni mara ya pili kwa Diamond kusababisha vurugu nchi za ughaibuni baada ya Septemba 1, kusababisha vurugu katika mji wa Stuttgart nchini Ujerumani aliposhindwa kufika kwa wakati ukumbini.
Akizungumza na gazeti hili, shuhuda wa tukio ambaye ni Mtanzania anayefanya shughuli zake nchini Uingereza, Flora Lyimo alionyesha wazi kukerwa na tukio hilo ambalo alieleza kuwa huenda likaharibu sifa ya nyota huyo ughaibuni.
Lyimo ambaye alihudhuria shoo hiyo alisema Diamond alisubiriwa na zaidi ya watu 200 tangu saa sita usiku bila nyota huyo kutokea na ilipofika saa 10:00 alfajiri, ndipo walipoanzisha vurugu kudai kurudishiwa pesa zao.
Shoo hiyo ambayo ilitozwa kiingilio cha pauni 20 sawa na fedha za Tanzania Sh54,280 iliishia kwa dosari ya aina yake baada ya polisi kulazimika kuingilia kati kusimamia urudishwaji wa fedha hizo.
Alisema waliamuru watu warudishiwe fedha zao, hivyo walipanga mstari na kurudishiwa fedha zao, kila mmoja akiamuriwa kuondoka eneo hilo huku wenye klabu hiyo wakinyang’anywa leseni.
“Ni jambo la ajabu na aibu kwa msanii ambaye Watanzania tunamtegemea atuwakilishe nje ya nchi anakubali vipi kutangazwa kwenye shoo kama hajalipwa pesa zake, watu wanamchukulia kama tapeli kwani yeye mwenyewe amewatangazia mashabiki wake halafu hajatokea.
“Wengi tunapata shaka kama hajashirikiana na huyo promota kwani hata huo ukumbi ambao shoo ilitakiwa kufanyika hauna jukwaa maalumu ambalo msanii anaweza kutumbuiza binafsi nilishangaa haikuwa eneo sahihi, lakini nikasema ngoja niende kumuunga mkono Mtanzania mwenzangu,”alisema Lyimo.
Hata hivyo, pesa zilizopatikana hazikutosha kuwarudishia watu wote ikizingatiwa kuwa wengi walikata tiketi kabla ya siku ya shoo, hapo ndipo vurugu zilipotokea na polisi kulazimika kumshikilia promota wa shoo hiyo ambaye alifahamika kwa jina la Victor.
“Polisi wengi sana waliofika hapa ukumbini kwa ajili ya kulinda usalama, walichokifanya ni kumchukua promota aliyeandaa shoo hii na kumweka chini ya ulinzi kwa kosa la utapeli, kwa sharti kwamba mpaka watakapompata Diamond, lakini mpaka sasa bado haijajulikana alipo,” alisema Lyimo.
Lyimo alionyesha wasiwasi wake na kueleza kuwa kutokana na mfululizo wa matukio hayo huenda Diamond akazuiliwa kufanya shoo katika nchi za Ulaya, kutokana na kuanza kupoteza imani kwa mashabiki wake.

MAKUBWA MISS BUM BUM WA BRAZIL ATOA PICHA AKIONESHA MAKALIO YAKE


You know those ladies who contest in that pageant where they check who has the best butt? Yeah well, they just released new sexy photos. The pageant released new lingerie pics of the contestants to say thank you for reaching one million votes in the competition. 

Online voting will determine 15 finalists from the 27 ladies vying for this year's title. The finale will hold in Sao Paulo, Brazil in November. Check out the pics after the cut...


LULU NA JOTI WAKINUKISHA BALAA


Mastaa wawili Bongo waliokuwa watangazaji wa Shindano la Kuibua Vipaji vya Kuigiza, Tanzania Movie Talents (TMT), Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Lucas Mhuvile ‘Joti’ wamezua balaa na kuwaacha hoi mashabiki waliohudhuria fainali za shindano hilo kufuatia aina ya viwalo walivyokuwa wamepigilia.
Staa wa Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiingia ukumbini na kigauni kilichoacha sehemu kubwa ya kifua wazi.
Mpango mzima ulijiri kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar, wikiendi iliyopita ambapo katika kuonesha ubunifu, mchekeshaji Joti, alitupia vazi la jinsi zote ambalo upande mmoja lilionekana ni sketi ya kike na mwingine suruali ya kiume.
Kama hiyo haitoshi, mwili wake aliugawa katika nafsi hizo mbili kwani licha ya sketi, pia mguu wake wa kushoto alivaa kiatu cha kike, kama ambavyo kichwani kwake, alisuka nywele upande mmoja kama mdada.Kitendo hicho kilionekana kama kuwapa bichwa wanaume wenye kufanya mapenzi ya jinsia moja, kwani waliona ni kitu cha kawaida kwa mwanaume kuvaa mavazi ya kike.
Staa wa vichekesho Bongo, Lucas Mhuvile ‘Joti’ akitumbuiza jukwaani ndani ya ukumbi wa Mlimani City.
Kwa upande wake, Lulu alivaa kivazi kilichoonesha sehemu kubwa ya mwili wake, kikiwa kimeziba matiti kwa mbali na kusababisha wanaume wakware kutokwa na udenda.
Katika fainali hizo za kumsaka mwenye kipaji cha kuigiza ukumbini hapo, mshiriki kutoka kusini mkoani Lindi, Mwanaafa Libuyu ndiye aliyeibuka mshindi na kuondoka na cheki ya Sh. milioni 50.
LULU AINGIA UKUMBINI
Shushushu wetu alimshuhudia Lulu akizama ukumbini humo akiwa amevalia gauni hilo lililoacha wazi sehemu ya mwili wake hivyo kujichafua mbele ya mamia ya mashabiki waliohudhuria.
“Yaani Lulu huwa anaonekana kama hajali vile, hebu muone nguo aliyovaa, imemuacha wazi sana, karibu mwili mzima uko wazi na anatangaza kwa kujiamini mpaka dah! Ni balaa!” alisikika mmoja wa wahudhuriaji hao.
‘Joti’ akizidi kuwaonyesha vimbwanga vya 'kikomedi' watazamaji waliohudhuria fainali za TMT ndani ya Ukumbi wa Mlimani City.
Kwa upande wake, Lulu alionekana kujiamini kupita kiasi bila kujali macho ya watu kwani alifanya kazi yake vizuri na hakuwa na wasiwasi wowote kufuatia nguo aliyokuwa ameivaa mwanzo.
JOTI NAYE
Kufuatia kipaji alichonacho, Joti, kila mtu hakuamini pale alipopanda stejini kutumbuiza kwa staili ya aina yake kufuatia vazi lake alilokuwa amevalia yaani nusu mwanaume na kuwafanya watu washindwe kukaa na kuishia kuangalia shoo aliyokuwa akiitoa kwa mashabiki.
“Ama kweli watu wana vipaji vyao, yaani kwa wakati mmoja Joti ameweza kuigiza kama mwanamke na mwanaume. Ukiachana na hayo, hadi nguo nayo imeshonwa hivyo! Dah! Fundi alifanya kazi tena nampongeza sana Joti maana nilijua anakuja kuigiza,” alisikika mhudhuriaji mwingine.
Mshiriki wa TMT kutoka kusini mkoani Lindi, Mwanaafa Libuyu akishangilia ushindi alioupata.
Katika maelezo yake, Joti alisema sababu ya kufanya vile ni sapraizi tu kwa mashabiki wake kwani huenda walijua atakuja kama ambavyo huwa anafanya sehemu mbalimbali.
“Nimeamua kuja kivingine, hii staili ni ya kawaida tu, sema watu wameshangaa kuniona vile, ndiyo maana Lulu alisema ni sapraizi kwa mashabiki, ni kweli nimewafurahisha sana na huwa wanashindwa kunielewa kwa jinsi ninavyobadilikabadilika,” alisema Joti.
Mwanaafa Libuyu akikabidhiwa zawadi.
Joti hakuishia hapo kwani baada ya mshindi kutangazwa tu, alitoa shoo ya nguvu huku watu wakimzunguka na kumuimbia kwa kufurahishwa jinsi alivyokuwa akicheza.
Kabla ya shindano hilo, Lulu na Joti waliwahi kudaiwa wanatoka lakini kwa pamoja walikanusha vikali skendo hiyo na kuweka hadharani kuwa uhusiano wao ni wa kikazi tu.

DIAMOND APIGWA MARURUFUKU KUKANYAGA UJERUMANI


Stori: Sifael Paul na mitandao
Kufuatia vurugu zilizoibuka ukumbini alfajiri ya Jumapili iliyopita baada ya msanii Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kucheleweshwa kupanda stejini kwenye Ukumbi wa Sindelfingen uliopo Mji wa Stuttgart, Ujerumani, mwanamuziki huyo anadaiwa kupigwa marufuku kutia maguu nchini humo.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
SHUHUDA WETU
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini mjini humo, ambacho pia kilikuwepo ukumbini wakati vurugu zilipoibuka, uchunguzi wa awali umeonesha kwamba, gharama ya vitu vilivyoharibiwa inakadiriwa kuwa zaidi ya Euro 128,322 sawa na Sh. milioni 280.
Viti vya ukumbi wa Sindelfingen uliopo Mji wa Stuttgart, Ujerumani vilivyoharibiwa na mashabiki waliopoteza uvumilivu kusubiri shoo ya Diamond Platinum.
“Tukio la vurugu za Diamond limeripotiwa kwenye magazeti tofauti mjini hapa lakini kubwa ni hasira ambayo mashabiki wa Diamond wameionesha waziwazi.
“Kwa mfano Gazeti la Stuttgarter la leo (Jumatatu) la mjini hapa limeandika:
Gari la polisi likiwasili eneo la tukio kutoa Msaada.
‘MASHABIKI WANA HASIRA NA DIAMOND’.
Kwenye habari zao waliwahoji watu waliofurika ukumbini hapo.
“Wengi walikuwa wakilalamika kwamba walikata tiketi mapema kwa euro 25 (zaidi ya Sh. elfu 55) kwa kichwa. Yaani kuanzia saa 4:00 watu walikuwa tayari wanamsubiri Diamond.
MUDA WAYOYOMA
“Kuna muda DJ alitangaza kwamba angepanda stejini kuanzia saa 6:00 usiku hivyo watu wakapunguza hasira. Cha ajabu saa saba ilikatika, nane ikapita, tisa ndipo mtiti ukaanza.
Mashabiki wakilizingira gari la Diamond.
“Sasa hebu fikiria mtu umetoa buku 55 yako halafu hadi saa tisa usiku mtu haonekani! Hapo ndipo tatizo lilipoanzia!” yamesomeka hivyo magazeti ya hapa.Ilisemekana kwamba ilipofika saa 10:00 alfajiri ndipo Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake, raia wa Nigeria anayejiita Kamabritts.
CHUPA ZARUSHWA
Mashabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki huyo na promota wake.Ilidaiwa kwamba kilichowakera zaidi mashabiki hao ni vyombo vibovu vilivyofungwa ukumbini humo kitu ambacho kiliwafanya kuvunjavunja viti, meza, jukwaa na vyombo vya muziki kisha kusababisha watu kujeruhiwa na hasara kubwa ya mamilioni ya shilingi.
Mapolisi wakilinda gari la diamond dhidi ya mshabiki waliokuwa na gadhabu.
MAJERUHI WAONGEZEKA
Baadhi ya vyombo vya habari mjini humo, juzi (Jumatatu) viliripoti kuongezeka kwa majeruhi wakiwemo MaDJ wawili ambao hali zao bado ni tete hospitalini kwa sasa.
Katika vurugu hizo, DJ mwanamke aliyetajwa kwa jina la DJ Flor alizimia hivyo akakimbizwa hospitalini huku mashabiki wakimpa kipigo DJ Drazee.
KAULI YA POLISI
Polisi eneo la Sindelfingen, Stuttgart nchini Ujerumani walisema tukio hilo ni la aibu hivyo uchunguzi wa kina unaendelea ambapo promota huyo na Diamond watalazimika kulipa vitu hivyo na kwamba hawatawaruhusu kufanya tena shoo eneo hilo na kwingineko nchini humo.
Magari ya wagonjwa yakiwa tayari kuhudumia majeruhi eneo la tukio.
Vyombo vya habari vya Ujerumani viliandika kuwa polisi wamesema walitenga askari 18 wa kutuliza ghasia ambapo walifyatua mabomu ya machozi ili kumuokoa Diamond.Walisema kwamba kitendo cha msanii kuchelewa kufika jukwaani nchini humo ni kitu cha hatari mno kwani mashabiki wanaheshimu muda wao.
PROMOTA ASAKWA
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni polisi walikuwa wakimsaka promota huyo, Kamabritts ili wamalizane na Diamond aruhusiwe kuondoka nchini humo na asirudie tena jambo kama hilo.
MCHEZO NYUMA YA PAZIA
Duru za kiuchunguzi zinaonesha kwamba, shoo nyingi za wasanii kutoka Afrika zinazofanywa kwenye kumbi mbalimbali katika baadhi ya nchi za Ulaya, hucheleweshwa makusudi ili vinywaji viuzike.
'Mzee wa Mdogomdogo', Diamond Platinum taratiiiibu akiondoka eneo la tukio huku gari likishambuliwa na washabiki wenye gadhabu.
Ilidaiwa kwamba, katika tukio hilo baya, kulikuwa na tatizo la kiusimamizi kwani mbali na promota, menejimenti ya Diamond ilipaswa kuwa na ratiba kamili na siyo kumsikiliza promota ambaye anawaza zaidi kuingiza kipato kuliko heshima ya msanii hivyo jamaa huyo kuwa staa wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kusababisha vurugu Ulaya.
LAWAMA KWA MENEJA WA UJERUMANI
Kuna maelezo kwamba, Diamond huwa ana mameneja wengi kwenye kila nchi anayokwenda hivyo huyo meneja wa Ujerumani alistahili lawama zote kwani alipaswa kujua kinachoendelea ukumbini.
BABU TALE ANASEMAJE?
Kuhusu hilo, Risasi Jumatano lilimtafuta meneja wa Diamond ambaye hakusafiri na msanii huyo, Babu Tale na kuulizwa kulikoni yaliyomkuta Diamond Ujerumani ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Kweli inasikitisha lakini haukuwa mpango wa Diamond. Ninachojua alikuwa akimsikiliza promota.
Ni changamoto kubwa lakini tunaomba radhi kwa mashabiki wetu wa Ujerumani. Next time wampokee vizuri.“Lakini kwa upande mwingine unajua ni jambo kubwa na niseme tu kuwa ukilitazama tukio hili kibiashara ni kama limemkuza zaidi kujulikana duniani. Umeona ameripotiwa na vyombo vingi vya habari. Mitandao ya kijamii ndiyo usiseme. Yote kwa yote tumejifunza na tunaomba radhi. Tusiangalie tulipoangukia, tuangalie tulipojikwaa.”
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga