Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » BABA AMBAKA BINTI YAKE WA MIAKA 12 KWA WIKI 2 MFULULIZO



Stori: Hamida Hassan na Gladness  
BINTI mwenye umri wa miaka 12 aliyejitambulisha kwa jina moja la Irine, mkazi wa Mbagala-Charambe, Dar amesimulia tukio la kusikitisha akidai kubakwa na baba yake mzazi kwa muda wa takribani miezi miwili.
Akilisimulia Risasi Jumamosi mkasa huo wa kusikitisha hivi karibuni nyumbani kwao maeneo hayo, binti huyo alisema kuwa baba yake aliyemtaja kwa jina moja la Israel alikuwa akimfanyia unyama huo mara tatu kwa siku (dozi) pale mama yake anapokuwa hayupo nyumbani. 
“Baba amekuwa akinibaka wakati wa alfajiri kwa zaidi ya miezi miwili sasa hasa mama anapoamka na kwenda kazini na usiku tulipokuwa tukilala wakati mama hajarudi, wakati mwingine ilikuwa ni wakati mama akiwa anaoga bafuni,”
alisema Irine. Binti huyo aliendelea kusimulia kwamba baba yake huyo alikuwa akimwingilia kwa kumlazimisha na pale alipokuwa akikataa alikuwa akimpiga vibao na wakati mwingine waya wa umeme.
“Nilipokuwa nikimuuliza baba kwa nini ananifanyia unyama huo aliniambia hana kazi ndiyo maana ananifanyia hivyo na alikuwa akipenda kuniuliza kama nafurahia au nasikia raha pale tunapokuwa kwenye tendo, nikijaribu kulia ananipiga na kuniuliza nataka watu wamsikie hivyo navumilia maumivu,” alisema Irine kwa uchungu. 
MAMA MZAZI AFUNGUKA 
Akizungumzia mkasa huo, mama mzazi wa Irine alifunguka kwa uchungu na kusema kuwa amekaa na mwanaume huyo kwa muda wa miaka 12 lakini hajawahi kumuonesha tabia hiyo.“Ninachojua baba yake ni mkorofi kwani huwa ananipiga mara kwa mara na amekuwa hapendi kufanya kazi, nilikuwa nikimuhudumia kwa kila kitu kuanzia chakula hadi malazi,” alisema.
Kamanda Kihenya. Mama Irine alisema habari za kuwa anatembea na mwanaye alianza kuambiwa na mtoto mwenyewe lakini hakutilia maanani kwa sababu alipombana alikataa.“Wikiendi iliyopita niliambiwa na jirani yangu kuwa nifuatilie nyendo za mtoto kwani amekuwa akilia sana muda ninapokuwa sipo nyumbani, nilipomuuliza mwanangu akafunguka kila kitu,” alisema na kuongeza: 
“Baada ya kuniambia, nilimbana mume wangu akawa hana jibu na nilipomlazimisha tukampime mtoto alikataa na kusema niende mwenyewe.“Nilikwenda kumpima na kugundua kuwa ameshaharibiwa vibaya sehemu za siri ndipo nikaenda polisi Mbagala-Kizuiani na kufungua jalada la kesi namba MB/RB/1171/15 –UBAKAJI.” 
Aliongeza kuwa alipomaliza kufungua kesi alipanga na askari baba Irine akamatwe na ndipo akarudi nyumbani bila kumweleza mumewe lakini alikuta tayari ametonywa na watoto wake.
“Nahisi mtoto wangu wa kiume ndiye alimtonya mume wangu kwani tuliporudi hatukumkuta, hata hivyo polisi wanamsaka ili wamfikishwe kwenye vyombo vya sheria.


About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga