Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » » Msanii JB Ala shavu


Na Denis Mtima
MWIGIZAJI Bora wa Kiume Bongo, Jacob Steven ‘JB’ amefuatwa na mastaa Wazungu kutoka Ulaya nchini Norway.
Hivi karibuni, Ijumaa Wikienda lilimnasa JB akipigwa na baridi usiku wa manane kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar ambapo alipoulizwa kulikoni alisema kuna waigizaji kutoka Norway wanaokuja kumfuata hivyo anawasubiri.
Alisema: “Kuna waigizaji Wazungu kutoka Norway wanakuja kunifuata, nimekuwa nikiwasiliana nao kwa muda mrefu, mwanzoni nilisita kwa kuwa nilikuwa siwajui. Baadaye nilijiwa na mawazo kwamba kwa nini nisiwatafute mtandaoni? Kweli nilipoingia mtandaoni na kutafuta majina yao niliwapata.
“Wapo wawili, majina yao ni Bard Yuvis Akir na Vega Uvisakir, waliniambia wanakuja kunichukua nikafanye nao kazi za filamu kwao, nikimaliza Tamasha la Matumaini tutarekodi filamu moja hapa nchini ndiyo tuondoke.”
wakati mazungumzo yakiendelea, JB aliitwa kwenye mlango wa kutokea uwanja wa ndege na kuwapokea wageni wake kisha kutimua eneo hilo.

Source:- Global Publishers

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga