Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » » Mwanafunzi Akutwa Amekufa Huku Akiwa "UCHI" chumbani kwake.

-->

Miracle Enzi za Uhai wake


Mwanafunzi kutoka Ebony State University, Aliyefahamika kwa jina la Miracle Eze amefariki dunia huku akiwa hana nguo hata moja (uchi) ndani ya chumba chake katika Campus ya Iseheke Chuoni hapo.

Siku moja kabla ya kufikwa na umauti, Miracle alienda chumbani kwa rafiki yake huku akilia machozi na kumweleza ni jinsi gani kuna mtu anamtishia maisha sababu ya kutomkubali kama mpenzi wake na anahisi atamfanyia kitu kibaya kama alivyomuahidi.

Asubuhi yake wenzake walipopita mlangoni kwake na kugonga hawakujibiwa, kwa kuwa walikuwa na haraka ya kuwahi masomo walihisi atakuwa anasali chumbani humo, lakini hadi wanatoka darasani binti huyo alikuwa hajaonekana na ndipo walipoamua kumpigia simu yake ya kiganjani ambayo ilikuwa inaita tu bila majibu.

Walisogea mlangoni na kuisikia simu ikiita, baadhi ya wavulana waliamua kupanda kwa dirishani kuchungulia ndani na ndipo walipomuona akiwa katika hali hiyo, taarifa zikatolewa Polisi ambao walifika na kuuchukua mwili huo huku Juhudi za kubaini chanzo cha kifo chake zikianza.

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga