Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

» » » » Unamkumbuka Rehema?!!, Sasa anakula bata na Mtoto wa Balozi Huko China!!


Na Hamida Hassan
MLIMBWENDE aliyewahi kung’ara katika Shindano la Miss Kiswahili 2009, Rehema Fabian anadaiwa kuangukia kimapenzi kwa mtoto wa Balozi wa Nigeria nchini China aliyemtaja kwa jina moja la Allen anayetaka kufunga naye ndoa.
Rehema akijiachia na mtoto wa Balozi wa Nigeria nchini China aitwaye Allen.
Akichati na Risasi Mchanganyiko, kwa njia ya mtandao, Rehema alikiri kuwa na mwanaume huyo ambaye ni mtu mzima na kweli ni mtoto wa balozi huyo.
Rehema akiwa na Allen.
“Nimechoshwa na masharobaro hivyo nimeamua kutulia na mwanaume huyo kwa sababu nimempenda na yeye anaonekana kunipenda,” aliandika Rehema.
...Wakizidi kujinafasi.
Rehema ambaye kwa muda mrefu amekuwa nchini humo, alisema kwamba amekuwa akipata wanaume wanaomtumia na kumuacha lakini safari hii amepata mtu sahihi.
...Pozi la kamera.
“Tumepanga kuja Tanzania kwa ajili ya kukamilisha mipango ya ndoa, hivyo nitarajieni huko muda si mrefu,” aliandika Rehema na kuongeza kwamba atafanya bonge la sherehe.

Source: GPL

About Unknown

Habari karibu katika Blog hii, Tafadhali Like Page Yetu na Toa Maoni yako kuhusiana na kile unachokiona humu.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga