Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

This is Why Ndoa ya Diamond Platnumz na Wema Sepetu Itadumu


Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz aka Dangote ni miongoni mwa wasanii wanaofanya vizuri katika music industry ndani na nje ya Tzee, yote ni kujituma kwake kwa kutoa hit songs za nguvu kama ‘Moyo Wangu’, ‘Ukimuona’, ‘Mbagala’, ‘Number One’ and so many songz zimempelekea kufika hapo halipo, mapenzi ya Dangote na Wema Sepetu aka Madam Wema yalianza pale jina la Diamond lilipoanza ku-make headline kwenye media kutokana na ngoma zake nyingi kukubalika, since that day mapenzi yao yalishamili kwa kasi sana ingawa walikuwa wana mvutano wa kutoaminiana na kusababisha Diamond Platnumz kuachana na Wema Sepetu na kumchukua Peniel Mungilwa aka Penny, but they could not last long mapenzi yakarudi tena kwa Wema Sepetu yote kutokana na Diamond kumuona Madam Wema ni msaada kwake, na kuna tetesi kuwa Wema Sepetu ananyota kali sana ya mafanikio kiasi cha kumfanya Dangote kuona umuhimu wa kufunga ndoa, na hivi ndivyo vitu vitano vinavyofanya ndoa ya Diamond Platnumz na Wema Sepetu kudumu kwa muda mrefu kama ndoa hiyo ikitokea.
Kutosikiliza maneno ya watu
tumeona ndoa nyingi sana za mastaa zinavunjika not only Tzee even abroad mfano kwa Bob Junior na Halima, Ezden na Dida yote ni kusikiliza sana maneno ya watu kuliko hisia zao wenyewe.
Diamond-Platnumz-59
Kusaidiana
Tukiangalia kwa Jay Z na Beyonce wanasaidiana sana kwenye kazi yao ili wazidi kuendelea ku-make mkwanja, so kwa Dangote na Wema wakiwa wanasaidiana watadumu na kufika mbali sana katika ndoa yao.
Super-couples-jay-z-beyonce-Diamond-Platnumz-Wema-Sepetu
Elimu
ukweli utabaki kuwa kweli Diamond Platnumz hana elimu ya kutosha kumzidi Wema Sepetu ila  ana mkwanja than Wema kitu kinachowafanya wazidi kujifunza kutoka kwa kila mmoja.
rp_diamond-wema.jpg
Kutambuana kitabia
kitu kitakachowafanya wazidi kudumu kwenye ndoa yao kila mmoja kumtambua mwenza wake coz wameshaumizana sana, kujivuna kwa sana na sasa watakua wanajua ni kitu gani wanapaswa wasifanye ili kutoumizana.
Diamond-Platnumz-62
Wote ni mastaa
Hii itawasaidia sana katika kuendeleza mshikamano wao katika ndoa kwa kujilinda kutokana na hadhi waliyonayo right now.
Wema-Sepetu-Diamond-Platnumz-Sasa-copyright-www-vibe-co-tz

Angalia Picha za Ajali Aliyopata Msanii Baba Levo



Mchana wa saa tisa October 10 2014 Baba Levo ambae ni msanii wa bongofleva aliipigia simu millardayo.com na kutoa taarifa za ajali aliyoipata saa saba mchana akitokea Tabora kuelekea Mpanda ambako alikua anakwenda kwa ajili ya kutumbuiza.
Baba Levo anasema alizitoa hizo taarifa saa tisa mchana sababu ndio aliweza kupata angalau network ya mtandao wa simu kwani kwa saa mbili zilizopita alishindwa kupiga simu baada ya kupata ajali porini kutokana na uzembe wa dereva wa Coaster aliehama upande wake na kuhamia upande wa pili kukwepa barabara mbovu.
Kina Baba Levo walikua kwenye Basi kubwa lililogongana uso kwa uso na Coaster hii ambapo Baba Levo alikua amekaa pale mbele pembeni kabisa ya dereva kwenye kile kigodoro ambapo msanii huyu ilibidi akae hapo sababu kiti chake kiliuzwa ticket kwa watu wawili hivyo aliamua kuiachia siti yake kwa mama wa Kiarabu baada ya kujikuta wote wamepangwa siti moja.
Baba 5Baba Levo anasema japo taarifa za vifo hazijathibitishwa, kuna watu kama Wanne ambao aliwaona wamepoteza maisha kwenye eneo la ajali kwa kupasuka vichwa na viungo muhimu vya mwili.
Baada ya ajali hii kutokea, dakika zaidi ya 150 baadae ndio walipata msaada na Baba Levo kwenda Hospitali kucheki afya yake ambapo alisafishwa vidonda alivyoumizwa na vioo vilivyomrukia mwilini kama inavyoonekana kwenye picha za hili basi hapa chini.
Baba 4

Lady Gaga Akatiza Mtaani Makalio wazi.


Sio Bongo Tu Wasanii Wanatafuta Kiki Kwa nguvu Mbali Hata Huko Marekani Wasanii Wanatafuta kiki Kila siku ili Majina yao yabakie midomoni mwa Watu , Mwanamuziki Mkubwa Lady Gaga Ambae amezoeleka kwa kuwa na vituko vingi awapo jukwaani sasa amehamishia vituko mtaani baada ya kunaswa akitembea akiwa amevaa T-shirt tu bila nguo chini kitu kilichofanya watu kumshangaa kila anapopita....

Warembo wanavyojua kujiachia na Instagram



Instagram ni zaidi ya uionavyo, watu wanajua kula raha asikwambie Mtu jionee mwenyewe...maisha mazuri hadi unashawishika kutaka kujua zaidi wanafanya nini...ntajaribu kuwatafuta hawa watupe siri ya mafanikio yao.

 1. Vera Sidika anapenda clubs yaani mdada yeye ni full ku party. What I like from her she has a talent ni mchoraji balaa anaonekana msomi pia alisema karudi shule big up @queenveebossette naomba tuongee zaidi kuhusu vipaji vyako naamini watu watabaki vinywa wazi.. 

2. Starlisha huyu naye ni mrembo wa instagram yeye anapenda kula sehemu nzuri, kupiga picha akiendesha magari mazuri na selfie za kumwaga. Mungu ni mkubwa kapunguza mabifu, sikuhizi yeye ni mshauri na mhamasishaji wa masuala mbali mbali ya maendeleo, hii inampa heshima safi sana @chaggabarbie naomba nijue siri ya utulivu wako, inapendeza sana. 
3. Huddah kama hayuko airport, hotelini basi swimming pool @huddahthebosschick unapenda kuogelea we mtoto, umekaa kibiashara tu mara photo shoot, lebel yako ya mavazi iko hewan na mengine atleast unaonekana unafanya kazi. Hizo bikini ukiziweka sokoni utauza sana. Hongera 

4. Masogange, picha nyingi yuko kitandani, kama sio kitandani bafuni kama sio nje ya nyumba then anarudi kitandani anajipiga mapicha weee hadi analala. Hongera nawe @officialagnes Mungu kakupendelea sana. 

Kuna wengine humu nashindwa kuwaelezea kwakweli...sitaki kujua sana maisha binafsi ya mtu ila natamani kujifunza au tujifunze kupitia hao "mastaa" Hakuna asiyependa kupiga mapicha all the time kalala, anaogelea, kwenye mahoteli makubwa na maboti anaenjoy maisha kama mnaweza kupiga mapicha hayo jamani tuonesheni na kazi zenu nasi tutamani kufikia huko??..

Picha za Trafiki aliyetimuliwa akiwa kavaa kiraia, Ni Sheeedah.


Wezee Nimekutana na Hiyo Picha Instagram, Yule Polisi wa Kike Traffic Watu wamechimba Mpaka Wamepata Picha zake Akiwa Bila sare za Kazini....

Baadhi ya Comment ni Hizi Hapa :

-mwambie alete CV mi ntamwajiri

-Aje kwangu atalelewa kuliko alivyokuwa huko!Contact pls 

-Kajazia Sana hata Ingekuwa Mimi Ningekula Mzigo, hiyo ni ajali kazini

Nyuma ya Pazia Sakata la Traffiki Walionaswa waki Dendeka


Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, chini ya Kamanda Mohammed Mpinga, limekuwa mstari wa mbele katika kusimamia maadili ya askari wake na kuwa mfano wa kuigwa lakini kuna baadhi wanalichafua, Ijumaa limenyetishiwa kamchezo kamili.
Polisi wa usalama barabarani wakidendeka.
HABARI KAMILI
Habari kamili ikufikie kwamba nyuma ya picha ya askari wawili, mwanamke na mwanaume wa usalama barabarani (matrafiki) wanaodaiwa kuacha kazi ya kuongoza magari na kwenda kufanya uchafu kichakani kuna utata mkubwa.
PICHA INASEMA
Picha hiyo inamuonesha trafiki mwanamke akiwa amepakatwa mapajani na trafiki mwanaume aliyekalia kitu kwa chini ili kupata balansi ya kumbeba mwenzake huku wawili hao ‘wakifanya yao’ wakiwa na sare za kazi.
TUJIUNGE NA VYANZO
Baada ya picha hiyo kusambaa kwa kasi ya moto wa kifuu kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii na kugeuka habari ya mjini, watu walikuwa na maoni tofauti huku baadhi wakipiga simu kwenye chumba chetu cha habari wakitaka kujua ukweli juu ya uwepo wa tukio hilo.
SIMU YA KWANZA
Simu ya kwanza iliyopigwa ilidai kwamba matrafiki hao ni maarufu katika Barabara ya Bagamoyo ambapo mara nyingi huongoza magari maeneo ya Tegeta jijini Dar.
Kamanda Mohammed Mpinga.
“Huyo mwanaume ni jamaa mmoja mpole sana anajulikana Tegeta na ana gari aina ya Baloon (Toyota).
“Huyo mwanamke, kwanza ni mke wa mtu lakini yupo bomba (mzuri) kinoma. Hata madereva daladala wanamjua maana amejaliwa, akitembea lazima atingishe,” kilidai chanzo hicho na kuongeza:
“Hapo ni maeneo ya Tegeta kwa sababu ukiangalia vizuri kwenye picha hiyo utaona nguzo ya umeme mkubwa wa Zanzibar.”
WHATSAPP
Wakati tukio likiwa ‘hot’, picha hiyo ilitumwa kwenye chumba chetu cha habari kwa WhatsApp huku ikiwa na maelezo kwamba tukio hilo lilijiri hivi karibuni mkoani Dodoma bila kufafanua maeneo gani kwa kuwa Dodoma ni kubwa. 
NI KANDA YA ZIWA?
Chanzo kingine kilichozungumza na gazeti hili kilidai kwamba tukio hilo siyo la Dar wala Dodoma ni maeneo ya Kanda ya Ziwa.
“Hilo tukio ni la Kanda ya Ziwa. Itakuwa ni kwenye moja ya Mikoa ya Kanda ya Ziwa (kati ya Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Geita),” kilidai chanzo hicho.
IMETENGENEZWA?
Baadhi ya wadau wa jeshi hilo walidai kwamba kuna uwezekano picha hiyo ni ya kutengeneza (photo shop) kwa kuwa haikujulikana aliyeipiga na kwamba iliwezekanaje kuwapiga ili hali wakijua ni kinyume na maadili.
“Unajua kinachonifanya nihisi kama imetengenezwa ni namna walivyojiachia. Kwa vyovyote kuna kitu cha ziada kimefanyika kwenye hiyo picha,” alisema mmoja wa wachangiaji mtandaoni.
MTAALAM: HAIJATENGENEZWA
Ili kuondoa utata huo wa kutengenezwa au kutokutengenezwa, gazeti hili lilimwonesha picha hiyo, mtaalam wetu wa kompyuta (IT), Nicolaus Trac ambaye alithibitisha kuwa siyo ya kutengenezwa.
“Ni vigumu kuwa ni ya kutengenezwa kwa sababu kuu tatu.
“Moja, mandhari ni moja, ingekuwa ya kutengeneza kila mmoja angeonekana tofauti lakini mazingira yanaonesha imepigwa eneo moja.
“Pili, angalia mikono yao ilivyovaana au kuingiliana. Sidhani kama kuna mtaalam angeweza kuweka mikunjo hiyo ya mikono na vidole bila kukosea sehemu.
“Tatu, angalia huyo mwanamke alivyomkalia mwanaume, inaonesha kabisa kumkalia kwake kumesababisha mkunjo katika suruali kwenye paja la mguu wa kulia,” alifafanua Nicolaus.
PETE YAIBUA MAMBO
Mbali na kukemea tabia hiyo na ukosefu wa maadili hasa kwa mtumishi wa serikali, wapo baadhi ya watu mitandaoni walikuwa wakimshambulia trafiki mwanamke kwani picha ilimuonesha akiwa na pete ya ndoa kidoleni.
“Mimi sijui kama huyo trafiki ni mumewe lakini namuona ana pete ya ndoa maana yake kuna harufu ya mchepuko. “Lakini hata kama ni mumewe, kwa nini wafanye mambo ya chumbani hadharani tena na sare za kazi? Kama walikuwa wamezidiwa sana si wangeenda nyumbani?” Alihoji mwanamke mmoja aliyetumiwa picha hiyo kwenye WhatsApp.
KAMANDA MPINGA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilimfowadia Kamanda Mpinga picha hiyo kwa njia ya WhatsApp ambapo alikiri kuwa nayo na kwamba  wanaifanyia kazi kabla ya kuchukua hatua kali kwa wahusika.
Katika mahojiano ya Kamanda Mpinga na Global TV Online hivi karibuni, kamanda huyo alisisitiza kwamba kikosi chake kinaongoza kwa maadili na kwamba inapotokea tukio kama hilo hutolewa adhabu kali.

Jambazi Muuawa watu Arusha Auliwa na Polisi


Jambazi mmoja aliefahamika kwa jina la Ramathan Abdallah alimaarufu kwa jina la Ramadhani Ndonga (37) mkazi wa Moivo ameuwawa baada ya kupigwa risasi katika majibizano na askari wa jeshi la polisi.
Akizungumzia tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Arusha Liberatus Sabas Alisema kuwa tukio hilo limetokea October 10 mwaka huu majira ya saa nane na dakika nne usiku katika kijiji cha Moivo kilichopo ndani ya kitongoji cha Enaboishu wilayani Arumeru.
Alisema kuwa marehemu Ramadhan Abdallh aliuwa anatafutwa kwa muda mrefu na jeshi la polisi kwa kuhusika na matukio mbalimbali ya uhalifu ambayo yameshawahi kutokea ndani ya mkoa huu pamoja na katika maeneo mbalimbali ya nchi hiii.
Alibainisha kuwa kuuwawa kwa jambazi hili kumetokana na juhudi na kutumia mbinu za kisasa za kiupelelezi na kufika nyumbani kwa mtuhumiwa (marehemu) ambapo askari polisi walimwamuru ajisalimishe lakini alikaidi amri na kuanza kuwarushia risasi hali ambayo ilisababisha askari kujibu mashambulizi na kumsababishia umauti kumfika.
“Mara baada yakupiga jambazi huyo polisi walianza kumpekuwa mwili wa marehemu na alipatiana akiwa ba bastola aina ya Glock 19 yenye namba RLU976 iliotengenezwa nchini Austria ikiwa na magazine yenye risasi (14) ambapo alikuwa ameishika mkononi pamoja na maganda matano yarisasi na mbali na hapo polisi pia walifanya upekuzi katika chumba cha jambazi hilo na kukuta magazine ingine moja yenye risasi (15) na magazine zingine mbili zenye uwezo wa kubeba risasi thelathini kila moja ,Radio call moja yeye nembo ya ITSS/UNICTR pamoja na pikipiki aina ya toyo power king rangi nyekundu yenye namba za usajili T507 BSU pamoja na kofia ngumu”alisema Sabas
Aidha alibainisha kuwa pia katika upekuzi huo wa ndani ya nyumba ya jambazi hilo pia walifanikiwa kupata pingu moja ,plate namba ingine ya pikipiki yenye namba za usajili T 805 CVD ambapo alibainisha kuwa jambazi hili lilikuwa likibadilisha plate namba ya pikipiki kila mara pamoja na chomba maalumu cha kuwekea magazine pamoja na kufanyia tageti kabla yakupiga risasi (Glock Fab Defense moja),kifaa cha kusafishia bastola pamoja na koti kubwa jeusi.
Kamanda Sabas alitaja baadhi ya matukio ambayo jambazi hili lilishayafanya kuwa ni pamoja na tukio lililotekea Augast 6 majira ya saa tatu na nusu usiku maeneo ya kwa iddi ambapo mtuhumiwa akiwa na mwenzake ambaye ajakamatwa walimpiga risasi ya shingo mwanamke aliyefahamika kwa jina la Shamimu Rashid aliyekuwa mkazi wa sakina wakati akijiandaa kuingina nyumbani kwake ,huku tukio lingine likiwa limetokea Augast 21 saa 19:00 maeneo ya olasiti ambapo jambazi huyo akiwa na mwenzake kwenye pikipiki walimjeruhi kwa kumpiga risasi ya domo na kutokea kichwani mototo aitwaye Christen NIckson mwenye umri wa miaka mitatu na nusu na kisha kufanikiwa kumpora TSH 2000 na baadae majeruhi kufariki dunia akiwa anapatiwa matibabu.
Kamanda sabas alitumia nafasi hiyo kuwapongeza askari wake kwa kufanya kazi nzuri pamoja na kuwahaidi wananchi kuendelea kufanya uchunguzi na kuwabaini wahalifu wote na kuwachukulia sheria kali.
“arusha sio sehemu ya kuifadhi wahalifu ivyo tutajitaidi kwa hali na mali kuhakikisha tunawamaliza majambazi wote pamoja na wahalifu wote na napenda kuwaaambia wahalifu waache mapema maana sasa ivi tumejipanga vilivyo ,pia napenda kuchukuwa nafasi hii kuwaomba wananchi pia waendelee kuwafichua wahalifu popote pale ili tuwaangamize kabisa”alisema Sabas



Mmoja wa wananchi ambaye alijitokeza kushuhudia maiti ya jambazi hilo Aliyejitambulisha kwa jina la Alaija Saro akiongea na libeneke blog hili alilipongeza jeshi la polisi kwa kuweza kumuangamiza jambazi hilo kwani limekuwa likiwatia mashaka watu wengi na kuwanyima raha kwa jinsi walivyokuwa wanauwa watu.

Gardner wa Lady Jay Dee Anaswa na Kabinti Night


LICHA ya kutothibitishwa juu ya kuwepo au kutokuwepo kwa ndoa yake na mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Jide’, mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash ‘Kepteini’ amenaswa na kabinti akiwa kwenye pozi tata za kimahaba hivyo baadhi ya watu kuhoji anasaliti ndoa? Risasi Jumamosi lilifuatilia hatua kwa hatua.
Mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash ‘Kepteini’ akiwa katika pozi la kimahaba na binti huyo.
OFM KAZINI, TUJIUNGE COCO
Tukio hilo lililojaa viulizo kibao bila majibu, lilifuatiliwa na Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers hatua kwa hatua ambapo lilijiri Jumatano iliyopita kwenye Ufukwe wa Coco uliopo Oysterbay jijini Dar kulipokuwa tamasha la wazi la kuibua vipaji vya wasaniii mbalimbali.
Awali, vijana mbalimbali walipanda katika onesho hilo na kuonesha vipaji huku binti huyo jina halikupatikana mara moja, alionekana na rafiki yake ambapo wote walikuwa ni washiriki katika onesho hilo.
GARDNER AMUIBUKIA
Wakati mtangazaji huyo akiwa katika mizunguko yake ufukweni hapo, ghafla jicho lake lilitua kwa binti huyo na kumfuata kisha kumnong’oneza kitu (haikujulikana alimwambia nini).
Gardner na mrembo wakiwa pamoja.
Huku wapenda ‘ubuyu’ wakimfuatilia kwa ukaribu, ndani ya muda mfupi, binti huyo alionekana kuelewa mazungumzo ya Gardner kwa kutingisha kichwa kuashiria ujumbe umemfika vizuri.
WACHEPUKA
Baada ya Gardner na mrembo huyo kusikilizana, wanahabari wetu waliwashuhudia wawili hao wakishikana mikono na kuondoka eneo hilo kwenda kununua vinywaji kisha wakajitenga sehemu wakinywa vinyaji huku Gadner akiwa amemkubatia kwa nyumba mtoto huyo mzuri na mwembamba kama Jide.
WAHAMA PAMOJA
Mashushushu wetu waliwashuhudia wawili hao wakipiga misele pamoja katika maeneo mbalimbali ya ufukwe huo huku mtoto wa kike akiachia tabasamu zito huku jamaa akiwa amemzungushia mkono kiunoni, wakizungumza maneno yalioonesha kuwa wapo kwenye urafiki mzuri.
Akimnong'oneza jambo.
WAPENDA UBUYU SASA!
Wakati Gardner akiwa bize akifanya yake huku akiwa ameongeza umakini, baadhi ya watu ambao ni wepesi kufuatilia mambo ya watu (wapenda ubuyu/umbeya), walianza kuibua minong’ono kwamba kulikoni mtangazaji huyo ambaye amekuwa mzito kutamka kwamba hawako pamoja na Jide, ajiachie kiasi hicho na mrembo huyo.
“Jamani huyu si ni Gardner? Vipi tena mbona anaambatanaambatana na huyu mtoto? Kwa vyovyote ni wazi kabisa kuna kitu kinaendelea kati yao, maana muda wote wapo beneti.“Duh! Sijui Jide akiwaona katika pozi kama hizi atajisikiaje kama kweli hawajaachana,” alisikika mmoja wa wapenda ubuyu.
Baada ya wanahabari wetu kupata walakini na kutaka kuthibitisha hilo, walianza kumfuatilia hatua kwa hatua mpaka waone mwisho wa mchezo utakavyokuwa baada ya kuona dalili hizo, kwa kuwa kadiri muda ulivyozidi kwenda ndivyo mambo yalipozidi kujianika hadharani huku wakijitahidi kukwepa kamera lakini waligonga mwamba.
WABADILISHANA VINYWAJI
Kuonesha kwamba urafiki wao si wakubahatisha, kuna wakati Gardner na mrembo huyo walibadilishana vinywaji jambo ambalo lilifanyika chini ya wapambe wa Gardner ambao walikuwa wakimzingira ili mapaparazi wasiweze kupata picha kwa urahisi.
Akizidi kuwanaye bega kwa bega.
Hata hivyo, mapaparazi wetu walifanikiwa kuzipata picha hizo kwa kutumia mbinu za kiintelijensia kama zinavyoonekana katika ukurasa wa mbele.
WATOWEKA
Wakati mapaparazi wetu wakiendelea kuwafuatilia, ghafla Gardner alitoweka eneo hilo lililokuwa na watu wengi kisha baada ya muda mfupi binti naye akatokomea kusikojulikana.
JIDE AAMBIWA AJIONGEZE!
Kwa mujibu wa mashuhuda wa mpango huo, mke wa Gardner, Jide anapaswa kujiongeza ili kulinda mali yake la sivyo wasichana wa mjini watamzidi kete.
BOFYA HAPA KUMSIKIA GARDNER
Alipotafutwa Gander kupitia simu ya mkononi juzi, Alhamisi ili kuulizwa kuhusu mrembo huyo, mtangazaji huyo alikiri kuwepo Coco kwenye shoo hiyo lakini hakumbuki ni binti gani amuone vizuri kwenye picha.
“Ebwana ni kweli nilialikwa kwenye hiyo shoo so nilikuwepo lakini kuhusu kabinti siwezi kukumbuka labda nione picha.



“Kweli nilipiga picha na mabinti wengi so sijui ni yupi, unajua nature (asili) ya kazi yangu (utangazaji) nakutana na watu wengi na wanapenda kupiga picha na mimi,” alisema Gardner.
GPL

Meninah Akana kutoka Kimapenz na Diamond Platnums


BAADA ya kuandamwa na skendo kuwa anatoka kimapenzi na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, mkali wa Bongo Fleva, Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’ amesema yuko mbioni kumtambulisha mchumba wake.
Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’.
Akipiga stori na gazeti hili, Meninah ambaye ni zao kutoka shindano la kuibua vipaji vya kuimba, Bongo Star Search ‘BSS’ 2012 alisema;
“Nimechoshwa kila siku kusikia Diamond, sasa ni bora nimtafute mwanaume yeyote tu kisha nimtambulishe ili ijulikane siko na Diamond,” alisema Meninah ambaye yupo mbioni kuachia ngoma mpya ya Kaniganda.Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’ akipozi.
Hivi karibuni kulikuwa na tetesi kuwa Meninah anatoka kimapenzi na Diamond, pia Diamond ameshafika kwao kujaribu kutoa mahari ili amuoe.
GPL.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga