Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

WEMA AFUNGUKA KUHUSIANA NA KUMDAI DIAMOND



 Ukubwa wa stori hii ambayo jana aliizungumzia Martin Kadinda kama Meneja wa Wema Sepetu imefanya millardayo.com kutaka kuujua undani zaidi kutoka kwa Wema mwenyewe.
Kwenye exclusive Interview,Wema amesema>>’Taarifa hii imenishtua sana maana asubuhi ya jana nimekuta kwenye gazeti wameandika nikashangaa yaani hapa nimekaa kwa sababu muda mwingi siendeshi mimi akaunti yangu ya twitter,anaiendesha mtu wangu wa blog Bestizo maana nilikua nataka kutoa tamko’
spt 
 
‘Nilishasema ukurasa huu tulishaufunga na nilishasema haiwezi kujirudia tena,nashangaa watu wanarudi na maneno yale yale maana nimekaa kimya kwa kila kitu ili kuepuka haya maneno’
‘Hakuna kitu ambacho namdai Diamond,hakuna siku hata moja nimefikiria kwenda kumshtaki Diamond labda kama kungekua kuna kitu chochote,yaani labda kungekua na ukweli wa kitu chochote siwezi kupoteza muda wangu kwenda polisi,sijawahi kufanya kitu cha namna hii hizi taarifa zimenishtua sana’
‘Sijawahi kujiunga Vikoba maana sivijui,nilikua nimekaa na mtu akanambia labda Wema hujui  hawa watu wa vikoba wanajaribu kujitangaza kwa njia hii na kutengeneza hii kitu kwamba vikoba wanaweza kukopa hadi Milioni kumi kwanza mimi siwezi kukopa Milioni 10′.


WEMA NA AUNTY EZEKIEL WAFUMWA WAKICHEKA JUU YA KABURI LA MAN NGWEA



INAWEZEKANA ilikuwa utani? Au ‘waliamka’ nazo?! Kweli binadamu anaweza kuvunjika mbavu (kicheko) juu ya kaburi la mpendwa wake? Mh!

Mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel wakiangusha kicheko katika kaburi la marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’.

Lakini imetokea! Wakati dunia ikisherehekea ujio wa mwaka mpya wa 2015, mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel walionesha jambo tofauti kufuatia kutinga kwenye kaburi la aliyekuwa nyota wa Bongo Fleva, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ na kutumia muda mwingi kucheka na kutuma meseji kwa simu wakiwa juu ya kaburi hilo.

ENEO LA TUKIO

Tukio hilo lililonaswa zimazima na kamera za Risasi Jumatano, lilijiri Januari Mosi, mwaka huu kwenye kaburi la Ngwea lililopo katika Makaburi ya Kihonda mjini Morogoro.

ILIVYOKUWA

Aunt ndiye aliyeanza kutia timu kwenye makaburi hayo na kukaa. Baadhi ya ‘kruu’ ya Wema, akiwemo Petit Man nayo ilifika na kuungana na Aunt.Baada ya dakika tatu, Mama la Mama, Wema aliwasili akiwa ndani ya nguo isiyokuwa ya mtoko, akakaa upande wa pili wa kaburi. Yeye na Aunt walikaa kwa kupeana ubavu.

CHA AJABU SASA

Awali ilidaiwa kuwa, kruu hiyo ilipanga kuwa baada ya kufika kwenye kaburi hilo wangefanya dua fupi kwa ajili ya kumwombea marehemu apumzike kwa amani huko aliko.Lakini cha ajabu, kabla ya ibada hiyo, Wema, Aunt na wafuasi wao walikuwa wakipiga stori za hapa na pale na katika hali ya kushangaza zaidi, ilifika mahali wakaanza kucheka kile kicheko cha kuvunjika mbavu bila shuhuda wa tukio hili kujua nini hasa kilichokuwa kikiwachekesha!

Baadhi ya wapita njia waliokuwa wakikatiza karibu na makaburi hayo, nao walipigwa na butwaa kuwaona watu hao, walioamini ni ndugu wa marehemu, wakiangua vicheko kama hawana akili nzuri. kwa nukta kadhaa walisimama na kushangaa kabla ya kuendelea na ‘hamsini zao’.-

WEMA ATUMIA SIMU KUFICHA USO

Ni dhahiri kuwa, Wema alijishtukia kuwa kitendo cha kucheka juu ya kaburi hakikuwa na ujazo wa kiungwana hivyo haraka sana aliweka simu sehemu ya midomoni na kumfanya asionekane kwenye kamera kwamba alikuwa akicheka. Miwani ya jua aliyovaa pia ilimsaidia.

Wakati Wema akionesha ubinadamu huo, ‘mwenzangu na mimi’, Aunt yeye alijimalizia kiu yake ya kicheko mpaka pale alipoamua mwenyewe kuacha na si kwa kuogopa kamera wala malaika waliolizunguka kaburi lile (kama wapo) la mmoja wa marapa bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania.

WEMA AJIELEZA KWA RISASI

Baada ya wote kuacha kucheka na kila mmoja kuchukua nafasi ya ubinadamu, paparazi wetu alimuuliza Wema ni kwa nini walionesha kuwa na furaha juu ya kaburi la staa huyo.Wema: “Tumepita hapa ili kumuombea ndugu na rafiki yetu Mangweha hivyo hatuna lengo lingine zaidi ya hilo.“Ishu ya kupiga stori na kucheka, tusingeweza kuacha kuongea eti kisa tupo kaburini, maana kila kitu lazima kijadiliwe hata kukaa hapa tumekaa kwa sababu tunafarijika kuona kaburi la mwenzetu.”

KWA NINI WALIFANYA ZIARA KABURINI KWA NGWEA?

Awali, mastaa hao na wapambe wao walikuwa na shoo ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika Desemba 31, 2014 ndani ya Ukumbi wa Matei Lounge mjini Dodoma.Wakiwa wanarudi Dar, walipiga kituo mjini Morogoro ambapo miongoni mwa mambo waliyokuwa nayo kwenye ratiba ni kulitembelea kaburi la Ngwea na kuangusha dua fupi.

Hata hivyo, baada ya yote hayo, kundi hilo la Wema na watu wake hatimaye walifanya dua fupi ya kumuombea malazi mema Albert Mangweha.

KUMBUKUMBU MUHIMU

Mangweha alikuwa msanii wa Bongo Fleva. Akiwa na miaka 31 alifariki dunia, Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini. Chanzo cha kifo chake inadaiwa ni matumizi yaliyopitiliza ya madawa ya kulevya. Alizikwa Morogoro, Tanzania, Juni 6 2013

Powered by Blogger.

KADINDA NA AUNT EZEKIEL KULIKONI?



MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda na mwigizaji Aunt Ezekiel wamenaswa chobingo wakiwa katika pozi tata.Tukio hilo lililoibua maswali mengi yasiyokuwa na majibu lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika Klabu ya 71, Tegeta-Kibaoni jijini Dar kulipokuwa na shoo ya kuukaribisha mwaka iliyoandaliwa na Kampuni ya Endless Fame.


“Mh jamani huyu Aunt si ana mume? Halafu si ana kibuzi chake kingine? Huyu Martin naye imekuwaje tena,” alisikika jamaa mmoja ukumbini humo.

Alipoulizwa Aunt kuhusu tukio hilo, alisema wamekumbatiana kirafiki tu na si
wapenz

WEMA ALIPIGA MNADA GARI ALILOHONGWA NA DIAMOND


Lile gari jipya aina ya Nissan Murano la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alilompa aliyekuwa mwandani wake, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ limezua mapya ambapo baada ya kudai linamchefua sasa anadaiwa kuwa analiuza kwa kigezo kwamba hataki gundu mwaka huu mpya wa 2015.


KUMBE LIPO KWA DALALI
Habari za kiwango kutoka kwa mnyetishaji wetu zilidai kwamba gari hilo lipo kwa dalali wa kike maarufu ajulikanaye kwa jina moja la Tindwa kwa ajili ya kulitafutia mteja.

NI KISASI?
Ilidaiwa kwamba, Wema ameamua kufanya hivyo kwa kuwa ana kisasi na hasira kwa Diamond kwa kuwa jamaa huyo kwa sasa anadaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Uganda, Zarinah Hassani ‘Zari au The Boss Lady’.

“Watu wanadhani Wema anafurahishwa na Diamond kutupia mapicha na Zari baada ya kuwasifia juzikati.
“Ukweli ni kwamba hivi sasa Wema anakereka sana na jinsi Diamond anavyoweka mapicha yake na Zari wakiwa sehemu mbalimbali na anaona kuwa na gari ambalo amepewa zawadi na Diamond ni kujipa kero zisizokuwa na sababu hivyo ameamua kuliuza,” kilisema chanzo hicho.

HALIJAPATA MTEJA
Mpashaji wetu huyo alizidi kunyetisha kwamba pamoja na gari hilo kuwa sasa bado liko sokoni lakini halijapatia mteja wa kulinunua kitu ambacho kinazidi kumkera Madam.
“Bado gari halijapata mteja ‘so’ kitendo hicho kinamkera sana Wema kutokana na gari hilo kutouzika mapema kwa maana kila anapoliona hajisikii vizuri kabisa,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa gazeti kwani ni ‘besti’ mkubwa wa Wema.

WEMA ANASEMAJE?
Baada ya kupewa ubuyu huo, gazeti hili lilimsaka Wema ambaye alipopatikana alidai yupo bize akiandaa shoo zake za mkoani Dodoma na Morogoro.
“Ngojeni kwanza nimalize shoo zangu za mikoani. Kwa sasa nipo Dodoma nikimaliza naenda Morogoro,” alisema Wema kwa ahadi kuwa atafafanua suala hilo vizuri akitulia.

TUMEFIKAJE HAPA
Diamond alimzawadia Wema gari hilo lenye thamani ya Sh. milioni 36, siku ya bethidei ya mwanadada huyo iliyofanyika Septemba 28, mwaka jana.
Siku chache baadaye Wema alidai kummwaga jamaa huyo huku akieleza kwamba hapendi kuliona wala kulitumia gari hilo kwani lilikuwa likimzidishia chuki juu ya jamaa huyo.

.

NICK MBISH ATANGAZA KUACHA MUZIKI



Rapper Nikki Mbishi leo ametangaza kuwa ameacha muziki.

Rapper huyo ameelezea uamuzi wake wa kuachana na muziki kutokana na kutokunufaika chochote na kwamba hawezi kuendelea kuwa mtumwa mwa kiwanda cha muziki.
“I’m glad to say I’ve officially decided to quit music….Wishing all the best to the slaves and victims of Music industry,” ametweet rappe huyo. “Nitaziachia tracks zangu zote ambazo hazijatoka for free then SITOINGIA TENA STUDIO kufanya wimbo(MUZIKI BASI).”
“The Industry is designed to frustrate the cats with high degrees of talents and intelligence. Ngwea,Langa,Geez mlale pema wanangu. I will remain as a music fan…and u guys need to find me some hip hop heads to listen to…asanteni,” ameongeza.
“Bora kuwa JAMBAZI kuliko MWANAMUZIKI. Tusije kushikiana bunduki bure maana milango ya kutoka kimaisha ni mingi na muziki ni burudani na biashara sio vita. Industry full of stupid and Illiterate but rich and famous. Mpaka lini tutauza UNGA kwa kivuli cha kuwa WASANII?”





HATIMAYE WEMA AUKUBALI UHUSIANO WA DIAMOND NA ZARI


U Heard ya juzi December 29 iko hapa, Gossip Cop alihudhuria shughuli ya kutambulisha msanii mpya ambaye atakuwa kwenye Management ya Endless Fame iliyofanyika Tegeta Dar siku ya jana December 28, akapata nafasi ya kuzungumza na Wema na jinsi anavyojisikia kuhusu uhusiano wa Diamond na Zari.
Wema alisema anachukulia fresh, hana tatizo lolote na yoyote kati ya wawili hao kwa sasa ameendelea na mambo yake.
“... Aisee nawapenda… such a good couple. Wivu wa nini, I wish him all the best and ammmm… I wish him happiness …” Wema Sepetu.
Kwa bahati mbaya wakati wakijiandaa kutoka ukumbini hapo baada ya mahojiano hayo Wema alipata jeraha baada ya kubanwa kidole na mlango wa gari.

ZARI NA DIAMOND WALIVYOJIACHIA MWAKA MPYA RWANDA



Baada ya show yake ya Burundi, Diamond Platnumz amefunga safari na Zari The Boss lady wakielekea Rwanda ambako kwa mujibu wa Post ya Diamond, atakuwa huko mpaka mwaka 2015.




RAY C AJIPANGA KURUDI NA ALBUM



Ujio Mpya wa Ray C Kudondosha Alabum

WAKATI asilimia kubwa ya wasanii wa Bongo Fleva wakiachana na mpango wa kutoa albamu, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amerudi rasmi katika muziki huo na wimbo wake mpya wa ‘Mshum Mshum’ huku akitamba kudondosha albamu.

Ray C alibainisha kuwa albamu yake itakuwa na nyimbo nane, ikiwa amemchukua mwaka mmoja na nusu kuiandaa mpaka kuikamilisha mwishoni mwa mwaka huu.

“Albamu yangu ina nyimbo nane na imechukua mwaka mmoja na nusu kuimalizia, najua mmesubiri sana na wengine walidhani sitarejea tena kwenye muziki, haya sasa bidada karudi tena kwa nguvu zote na Mwenyezi Mungu kabariki wimbo wangu unafanya vizuri na nimepokea pongezi nyingi kutoka kwa mashabiki,” alisema Ray C.

Ray C aliyesifika kwa kuzungusha kiuno chake, alisema pongezi anazozipokea zinampa moyo wa kuzidi kufanya kazi nzuri zaidi.

“Eeh Mola niepushe na husda za binadamu, nifungulie milango yenye neema na baraka zote,” alisema Ray C.


Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga