Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

Msanii Maringo Saba Anywa Sumu!!

--> Msanii wa vichekesho vya "Mizengwe" kupitia kituo cha ITV amelazwa katika hospitali ya Mwananyamala baada ya kunywa sumu akiwa na nia ya kujia baada ya kumfumania mkewe akivinjari na rafiki yake wa karibu. Udaku unaelezwa kuwa maringo aliwawekea mtego siku nyingi nz arobaini yao ilikuwa imefika wiki iliyopita ambapo baada ya tukio la kuwafumania na mkewe kuamua kula kona jamaa akaona bora ajiue.

Dereva Aliyemgonga Askari na Kumuua Papo Hapo Kortini

DEREVA anayetuhumiwa kwa kesi ya kusababisha kifo cha askari wa usalama barabarani, Koplo Elikiza Nnko, Jackson Steven Simbo (pichani) amefikishwa mahakama ya Kinondoni, Dar, Machi 26,  mwaka huu na kuzua jambo kortini.
Mtuhumiwa huyo baada ya kupata dhamana alikwenda ofisini kwa maofisa wa mahakama hiyo na kubadili shati kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kuondoa nuksi ya kulala rumande kwa siku 8.
Jackson anakabiliwa na makosa matatu,   kusababisha kifo cha Koplo Elikiza, kuendesha gari kwa mwendo kasi na kuingilia msafara wa kiongozi na kushindwa kujisalimisha polisi hadi alipokamatwa. Kesi hiyo itatajwa tena Aprili 15, mwaka huu.

Source:gpl

Eti Isha Mashauzi anatumia Madawa ya Kulevya!



-->




Hatimaye mamaa Isha Mashauzi, mkurugenzi wa bendi ya mashauzi classic amefunguka na kukanusha ya kwamba anavuta bangi, badala yake amesema ya kuwa hupata faraja toka kwa vinyaji vikali na mirungi hasa akiwa anataka kupanda stejini, na kwa vile hana mume wala mtoto basi hizo ndo kampani zake kwa sasa.

Milioni 13 za Wema Sepetu zamrudisha Kajala Uraiani.


-->


Msanii wa filamu za kitanzania Kajala Masanja ameachiwa huru leo mchana baada ya Msanii mwenzie WemaSepetu, kumlipia Faini ya Shilingi Milioni 13 na kumfanya asiende kutumikia kifungo cha miaka mitano jela. Kajala ambaye alihukumiwa akiwa na mumewe ambaye yeye ameenda kutumikia kifungo cha miaka saba jela kutokana na kupatikana na hatia ya kesi iliyokuwa ikiwakabili ya utengenezaji wa fedha haramu. Katika mahojiano na kituo kimoja cha radio nchini, Wema amesema kwamba anajisikia kama shujaa fulani kwa msaidia rafiki yake huyo na ilimchukua kama masaa mawili hivi kumaliza kila kitu.

Chinua Achebe Afariki Dunia

Profesa Mahiri na mtunzi wa kitabu cha "Things Fall Apart" Chinua Achebe amefariki dunia. Mwandishi huyo maarufu toka Afrika Magharibi amefariki nchini Marekani alipokuwa akiishi baada ya kuugua kwa muda kidogo. Mpaka umauti unamfikia alikuwa akifundisha masomo ya Lugha katika chuo cha Brown, amefarikia akiwa na umri wa miaka 82.

Kuna Ulazima wa Tatoo Mpaka......

-->


Siku za hivi karibuni kumekewa na wimbi la vijana wengi kujipiga tatoo sehemu mbali mbali za miili yao. miongoni mwa sababu zikiwa ni hamasa ya ushabiki au mapenzi yao juu ya kitu fulani au mchezo fulani. Cha kushangaza sasa hali imekuwa too much kiasi kwamba watu wanajipiga tatoo hadi sehemu za siri.

2face Aoa Dubai Jana

Mwanamuziki 2face kutoka nchini Nigeria jana Jumamosi ya Tarehe 23/03 ameuaga U single boy baada ya kufunga pingu za maisha na mwanadada Annie Macaulay. Katika kuhakikisha Mpango mzima unakwenda vizuri, Milionea wa Kinageria ambaye anaishi Marekani Ayri Emami, amechangia Shilingi milioni 20 za Nigeria.

Miss Israel "MWEUSI" Wa Kwanza

-->
Mwanadada Yityish Aynaw, ni mkimbizi toka nchini Ethiopia. Ameweka Rekodi ya kipee pale alipotoa Taji hilio la Mlimbende wa mwaka wa Nchi hiyo juku akiwa na asili ya kiafrika. Inasemekana kuwa mwanadada huyo alihamia nchini humo zamani akiwa bado binti mdogo.

Kutana na Bingwa wa kujipinda

--> Kwa jina anaitwa Alesha Dixon, akiwa katika moja ya shows zake huko Uingereza, akijipinda zaid ya mpira.

Mvuto wa Kim baada ya Kujifungua


-->















 Picha hiyo ikimwonesha mwanadada Kim Kardashian na Ddada wakiwa matembezini huku akiwa na mvuto kama vile hajajifungua siku za hivi karibuni.

Mpango mzima ndani ya Dar Live

-->
Hatimaye magwiji wa hip hop ndani ya wilaya ya Temeke, Dar na Tanzania kwa ujumla, nazungumzia makundi ya wanamuziki ya TMK Halisi na TMK Family yanatarajia kufanya makamuzi ya kufa mtu ndani ya Ukumbi wa Dar siku ya Tarehe 31/03/2013...... Nisikumalizie uhondo.....

Timbulo na Skendo ya Madawa ya Kulevya

< div class="separator" style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none; clear: both; text-align: center;">

Habari ambazo bado hazijathibitishwa zinaeleza ya kuwa Msanii Ali Timbulo, maarufu kama Timbulo amekamatwa akiwa na mzigo wa madawa ya kulevya Nchini Burundi, Timbulo ambaye alikwenda nchini humo kupiga show kutokana na maombi ya wapenzi wake wa nchini humo.

Steve Nyerere Apata Ajali kisha atupwa Rumande

-->
Nyota wa filamu za Kibongo nchini, Steve Mengele, maarufu kama Steve Nyere amekutwa na mkasa wa aina yake pale alipopata ajali jumatatu ya wiki iliyopita maeneo ya kijitonyama ambapo Steve akiwa ndani ya gari yake aina ya Toyota Verosa aliligonga gari lililokuwa limesimama ghafla mbele yake aina ya Toyota Fun Cargo na kulisababisha litumbikie mtaroni. Baada ya tukio kulitokea majibizano baina ya madereva hao ambapo walipofika askari kutuliza ghasia inasemekana kulitokea kupishana kauli kati ya askari na nyota huyo ndipo alipopigwa "Tanganyika jeki" na kupelekwa kituoni,
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga