Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

WANAODHANI MAISHA MAZURI YANATOKANA NA KUJIUZA BASI NAO WAJIUZE" HUDDAH MONROE"


Mshiriki wa zamani wa BBA Huddah alikasirika Baada ya mashabiki wake wa kike instagram kumwambia kuwa anatembea na wanaume wengi ili ili apate pesa ya kuishi.

Naye akaamua kuwajibu kuwa kama wanafikiri maisha mazuri aliyonayo yanatokana na yeye kujiuza basi na wao wajiueze ili wawe na maisha kama yake.

Hii yapa Comment yake

"Honestly, I don't understand why women have to be the ones hating all the damn time . If you think my v@gina is giving me the life I live then why don't u use your vagina too to get a life instead of hating?"

DIAMOND PLATINUMZ HATAREE, APOKELEWA KAMA MFALME DAR AKITOKEA SOUTH.



Diamond baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar.
Mashabiki waliofika uwanja wa ndege kumpokea Diamond.
Diamond akipokelewa na mashabiki kwa shangwe.
MWANAMUZIKI Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ametua nchini muda huu akitokea Afrika Kusini alipokwenda kushiriki zoezi la utoaji tuzo za Channel O ambapo alijinyakulia tuzo tatu kwa mpigo. Tuzo alizonyakua staa huyo ni pamoja na Most Gifted New Comer, Most Gifted Afropop na Most Gifted East kupitia wimbo wake wa Number One.

AL SHABAB WAMFANYA IGP KIMAIYO WA KENYA AJIUZULU


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Kenya, David Kimaiyo ametangaza kustaafu leo kutokana na shinikizo dhidi yake ajiuzulu kwa kushindwa kukabiliana na usalama nchini humo.
Wakati huohuo Kenyatta amempendekeza Waziri Mkuu mpya wa usalama Joseph Nkaiseri kuchukua nafasi ya aliyekuwa Waziri wa Usalama wa nchi hiyo, Joseph Ole Lenku.
Rais Kenyatta alisema kuwa baada ya mazungumzo na Bwana Kimaiyo alikubali kustaafu majukumu yake hayo.

KWA HILI MPENZ WA WOLPER ARINGE TU...


Ni jambo la kawaida kwa binadam kujiachia hasa pale tunapokuwa katika hali fulan ya raha ama kujawa na hisia nzuri za kimahaba. Kupitia akaunti yake ya Instagram, msanii wa Bongo Movie, Mrembo Jacqueline Wolper amefunguka na kusema kuwa hlo ndio pozi analohusudu pindi anapokuwa ana chat na wake wa moyo.....

Je wewe ushawahi kujitathmin kuhusiana na pozi gani hukuhamasisha unapokuwa unawasiliana na mwenza wako...???

JANGA LA UPUNGUFU WA NGUVU NA MATUMIZ YA VIAGRA KWA WANAUME


Inasikitisha sana siku hizi wanaotumia Viagra ni vijana wadogo sana ,wengine hata ni wanafunzi wa vyuo. Na hii si Dar tu, mpaka hata mikoani..nilikua Dodoma nikawa na jamaa yangu mmoja pale anaduka la dawa...ananiambia Viagra ndio inamlipa kuliko dawa zote.

Wateja ni wanafunzi wa vyuo na waheshimiwa. Sijui kwa kweli nini kinalikumba Taifa. Hivi kweli kwa mawazo yako unaweza ikomoa papuchi wewe. Acheni ujinga jamani.
Excellence is not a destination you arrive at… It is the benchmark for your journey. Earvin “Magic” Johnson

SAKATA LA ESCROW, KUMBE LUKUVI ALITAKA KUIBA RIPOTI SAA 9 USIKU.


Dar es Salaam. Viongozi wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe na Deo Filikunjombe wamemtuhumu Waziri William Lukuvi kuwa alitaka kuiba ripoti ya kamati yao kuhusu uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow.
Sakata hilo lilihitimishwa Jumamosi wakati Bunge lilipoazimia kuwajibishwa kwa watu wote waliohusika kwenye uchotwaji wa fedha hizo, ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa taasisi za fedha zilizoruhusu kufanyika kwa miamala mikubwa kinyume na taratibu za kibenki. Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wabunge hao wawili kutoka Chadema na CCM walilieleza gazeti hili kuwa jaribio hilo lilishindikana baada ya wao na mjumbe mwalikwa, Luhanga Mpina (CCM) kuamua kukesha wakiilinda ripoti hiyo tangu ilipokuwa ikichapwa hadi ilipowasilishwa bungeni.
Hata hivyo, Lukuvi alikanusha vikali tuhuma hizo akisema kuwa aliipata ripoti hiyo siku iliposomwa na kwamba kama angehusika, asingekubaliwa kuwa mjumbe wa kamati ya maridhiano iliyoundwa mwishoni mwa kikao kupendekeza maazimio ya Bunge.
“Si kweli,” alisema waziri huyo wa nchi anayehusika na sera, utaratibu na Bunge.
“Unajua PAC walikuwa wanafanya kazi chini ya hazina. Hata Spika wa Bunge hakuiona hiyo ripoti, aliisikia tu ikisomwa bungeni. Kwanza kamati ilikuwa ikidurufu hiyo taarifa yake eneo la mbali na ili uipate ilikuwa ni lazima umrubuni Zitto.”
Aliongeza kusema: “Kama kweli nilikuwa nataka kuiba taarifa yao nisingekubali kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya maridhiano, iliyokutana kupitia upya mapendekezo ya PAC baada ya yale ya awali kuzua mvutano bungeni.”
Hata hivyo, Filikunjombe, ambaye alikuwa makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, alikwenda mbali zaidi na kudai kuwa walilazimika kumwondoa eneo la kuchapishia ripoti hiyo. “Waziri Lukuvi alitumwa saa 9:00 usiku kuiba taarifa yetu wakati tunaichapa. Taarifa ilikuwa katika ‘flash’ na tulipogundua hilo tulimfukuza. Sisi tuliamua kuilinda ripoti ili isiibwe,” alisema Filikunjombe ambaye ni mbunge wa Ludewa kwa tiketi ya CCM.
“Ile taarifa tuliichapa usiku wa kuamkia Jumatano ambayo ilikuwa siku ya kuiwasilisha bungeni. Na hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya kikao cha Bunge kuahirishwa mara tu baada ya PAC kuwasilisha taarifa yake, ili Serikali ikajipange,” aliongeza.
Mbali na kauli yake ya jana, Filikunjombe aligusia suala hilo la ulinzi wakati akishukuru wabunge kwa kushikamana katika kufikia maazimio manane ya kuwawajibisha wote waliohusika.
Katika shukrani hizo, Filikunjombe alisema walilazimika kukesha usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita kuilinda ripoti yao isiibiwe na hivyo kuwashukuru watendaji wa Bunge kwa kazi nzuri.
Hata hivyo, kabla ya kuwasilishwa kwa ripoti hiyo kulienea taarifa kuna watu waliiiba na kunyofoa kurasa zilizokuwa na nyaraka za vielelezo na baadaye kuanza kuzisambaza. Polisi ilidai baadaye kuwa ilimkamata mtu aliyekuwa akisambaza vitabu hivyo vya ripoti, lakini hadi leo hajafikishwa mahakamani wala hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na polisi kuhusu maendeleo ya mtuhumiwa huyo.
Katika sakata hilo kubwa la aina yake, Bunge limtia hatiani Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Mwanasheria Mkuu Jaji Fredrick Werema na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Eliachim Maswi na wakurugenzi wa Shirika la Umeme kwa kuhusika kwa makusudi au kwa uzembe katika kufanikisha miamala haramu kutoka kwenye akaunti hiyo.

AKODI MATARUMBETA KWENDA KUMSUTA MWIZI WA BWANA WAKE WA ESCROW


Makubwa! Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikiwa kwenye msukosuko wa fedha zilizochotwa ‘kihuni’ kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, mwanaume mmoja, mtumishi wa wizara hiyo mkoani hapa almaarufu Kigogo wa Escrow, amesababisha wanawake wawili kusutana kwa matarumbeta na kukabana wakidaiwa kumgombea kwani ana fedha ‘chafu’.
Wakina mama, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota  ( katikati ) wakisutana kwa kuibiana mabwana.
Tukio hilo la aina yake lilijiri wikiendi iliyopita katika Mtaa wa Karume mjini hapa ambapo wanawake hao, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota walisababisha pakachimbika hadi polisi walipofika na kuokoa jahazi.
Awali ilifahamika kwamba wanawake hao walikuwa wakiishi pamoja maeneo ya Kikundi, Kata ya Sultan Area mkoani hapa. Kwa mujibu wa madai ya mashuhuda waliokuwa wamefunga mtaa huo, Tabu ndiye aliyeanza ‘kuchepuka’ na kigogo huyo ambaye ni mume wa mtu aliyemnunulia gari aina ya Toyota Opa.
Madai yaliendelea kushushwa kwamba, Mwajuma ambaye ni mke wa mtu alipoona mwenzake anakula vinono, naye akajiweka.
Bendi ilikodiwa na Tabu Mohamed ili kumsuta shosti yake Mwajuma Chota.
Habari za mtaani zilidai kuwa katika kujiweka, alifanikiwa kulamba mshiko wa shilingi elfu 80 kabla ya kushtukiwa na Tabu huku naye akitaka kuhongwa gari kama mwenzake.
Ilielezwa kwamba katika kufuatilia, Tabu aligundua kuwa Mwajuma anachepuka na ‘mshefa’ wake ndipo akapanga mashambulizi ya vita vya ardhini.
Kwa hasira, Tabu alishonesha sare za ‘madila’ na kununua mizinga ya pombe kali ambapo alienda kukodi matarumbeta na watu wa kusuta.
Wakubwa kwa watoto wakishuhudia vimbwanga vya wakinamama hao.
Ilisemekana kwamba kabla ya tukio, watu walipiga pombe kisha wakamfuata nyumbani kwao, Mtaa wa Karume na kulianzisha.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda ambalo liliwasili eneo la tukio ndani ya dakika sifuri juu ya tukio hilo, Mwajuma alifunguka: “Namshangaa Tabu kuja kunifanyia vurugu wakati na yeye ni mwizi tu. Huyo bwana ni mume wa mtu.”
Kwa upande wake, Tabu alidai Mwajuma ni shosti yake lakini alimtendea kitendo kibaya cha kutembea na bwana’ke.
Mmoja wa wamama hao, Tabu Mohamed  akichukuliwa na polisi kwa kumletea fujo mwenzake, Mwajuma Chota.
Alipobanwa zaidi hasa suala la kukodisha matarumbeta na kwamba mwanaume huyo ni mume wa mtu, Tabu alidai kwamba jamaa huyo alimkataza kuzungumza na wanahabari.
Baada ya kuipata ishu hiyo, gazeti hili liliwasiliana na mke wa kigogo huyo na kumuuliza kama ana habari kwamba kuna wanawake wanamgombea mumewe ndipo akapatwa na mshtuko na kuahidi kulifanyia kazi na kama ni kweli atafungasha virago.
Makamanda wa Polisi wakiimarisha ulinzi eneo la tukio.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume, Elly Mgota alithibitisha vurugu hizo kutokea kwenye mtaa wake ambapo sakata hilo lilitinga polisi baada ya Tabu kutiwa mbaroni kwa kosa la kumfanyia fujo mwenzake.

KESI YA MADAWA ILIVYOHARIBU MIPANGO MIZURI YA CHID BENZ


Rapper Chidi Benz anayekabiliwa na kesi ya kukutwa na madawa ya kulevya, amesema kesi hiyo imeathiri kufanyika kwa video ya wimbo wake ‘Mpaka Kuchee’ aliyowashirikisha Diamond na AY.

Chidi alikuwa akiongea na Bongo5 jana kwenye uzinduzi wa video ya Wakazi ‘Wanawake wa Dar’.

“Video inakuja, bado sijaanza kufanya mazungumzo na AY wala Diamond ambao nipo nao kwenye hiyo project,” alisema. Video itafanyika hivi soon, haya matatizo ndo yameichewesha hii project.”

Kesi yake inatarajiwa kusikilizwa tena December 1. Diamond na AY waliahidi kugharamia video hiyo.

Credit Bongo5

AJALI ILIYOTOA UHAI WA MMILIKI WA MATEI LODGE NA KUMJERUHI BLOGGER WA DODOMA


Gari alilokuwemo Mattei likiwa limeharibika vibaya baada ya ajali.
Wananchi wakiwa eneo la tukio.…
Gari alilokuwemo Mattei likiwa limeharibika vibaya baada ya ajali.
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
Mmiliki wa Mattei Lodge enzi za uhai wake.
MMILIKI wa Mattei Lodge iliyopo Area D mkoani Dodoma aliyefahamika kwa jina moja tu la Mattei amefariki dunia katika ajali ya gari jana Jumapili eneo la Pandembili, Kongwa.
Chanzo cha ajali hiyo inadaiwa kuwa mwendo kasi uliopelekea gari hilo kuligonga gari lingine na kisha kupinduka.
Marehemu Mattei alikuwa na wenzake watatu katika gari ambao walijeruhiwa Akiwemo Blogger wa Dodoma Boss Ngassa.

ASKARI WA JWTZ APIGA MTUNGI MPAKA KUJIKOJELEA NA KUTUPWA MTARONI


KATIKA hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa na wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa leo amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakali na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa
Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa.
Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogondani ya basi hilo.
Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu .
Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumkutana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza
" Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare .....sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja
Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana mambi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa .
Ushauri wetu kwa askari wetu kujaribu kuheshimu nafasi hizo japo hakuna anayewakataza kunywa pombe ila watambue kuwa unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ama chonde chonde ulevi noma.


HISTORIA YA SINGA SINGA TAPELI WA IPTL AMBAYE ANALIWEKA PABAYA TAIFA



Unamjua? Anaitwa Harbinder Singh Sethi! Ni mfanyabiashara bilionea mwenye asili ya Bara la Asia na mmiliki wa mtambo wa kufua umeme wa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ambayo hivi karibuni imezua tafrani Bongo kufuatia kampuni yake kuhusishwa na uchotwaji wa fedha kiasi cha Sh. Bilioni 306 kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Singa singa ambaye ni mmiliki wa mtambo wa kufua umeme wa IPTL, Harbinder Singh Sethi! (wa pili kulia) akielekeza jambo.
Harbinder ambaye ni singasinga anatajwa pia akidaiwa kuwa mfanyabiashara tapeli kufuatia vitendo vyake mbalimbali katika kumiliki makampuni na ukwepaji wa kodi ya serikali.
HISTORIA YAKE FUPI
Harbinder anatajwa na vyanzo kwamba ni mzaliwa wa Mkoa wa Iringa. Mwaka 1977 akiwa na umri wa miaka 20 ya kuzaliwa na nduguze wawili, Nota Singh na Manjit Singh walianzisha kampuni ya ujenzi wa barabara iliyojulikana kwa jina la Ruaha Concrete Co. Ltd ikitumia SLP 498, Iringa. Ruaha ni sehemu maarufu kwenye Manispaa ya Mji wa Iringa kukiwa na vitongoji vya Ipogoro, Kibwabwa na Ndiuka. Jina la Ruaha linatokana na Mto Ruaha kupita eneo hilo.
Vyanzo vinasema, Harbinder alianza kumiliki fedha nyingi kuanzia miaka ya 80 wakati familia ya Rais wa Kenya wakati huo, Daniel Arap Moi ilipoanza kujiingiza kwenye biashara mbalimbali.
Waziri mkuu, Mh. Mizengo Pinda.
AHAMIA KENYA
Vyanzo vikadai kuwa, miaka hiyo, singasinga huyo alihamia jijini Nairobi, Kenya ambako alianza kuwa mshirika wa kibiashara na mtoto wa kwanza wa Rais Moi aitwaye Gideon Moi.
ALIANZA UMEME NCHINI KENYA
Akiwa nchini humo, vyanzo vinamtaja singasinga huyo kuwa alipata umiliki wa mtambo wa Westmont wa kuzalisha umeme wa megawati 47 jijini Mombasa.
Washirika wenzake katika mradi huo walikuwa Mukesh Gohil, Kamlesh Pattni, Gichuru na Mkurugenzi Mtendaji wa KPLC, Mutitu.
Singh pia anatajwa kuwa na miradi  74 iliyofungwa katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki kutokana na kuvurunda kama siyo kufanya vibaya.
ALIPATA MSALA KENYA
Mwaka 1997, Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Mashirika Kenya ilianika udhaifu wa Ruaha Concrete katika tenda ya ujenzi wa barabara ambako kulikuwa na ucheleweshaji, kuongezeka kwa gharama pamoja na utekelezaji hafifu uliojitokeza.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi.
Kufuatia madai hayo, ilibidi mhandisi msimamizi wa mradi huo aliyetajwa kwa jina moja la Kitololo ajiuzulu baada ya kukataa kutia saini kuwa kazi iliyozembewa imekamilika.
ARUDI BONGO
Haikujulikana mara moja ni mwaka gani alirejea Bongo, lakini ilidaiwa kuwa tayari alishawekeza nchini huku akiwa bado ana biashara zake Kenya na baadaye alirudi jumla kutokana na misala ya kule.
KWA NINI NI TAPELI?
Singh anatajwa kuwa mfanyabishara tapeli kufuatia Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kumtaja kuwa amehusika na vitendo vya ukwepaji wa kodi akitumia mbinu za ujanjaujanja.
Mfano mkubwa ni hizo bilioni 306 alizochota kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow hakuzilipia kodi na ndiyo maana Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akihutubia bunge mjini Dodoma, Ijumaa iliyopita katika mjadala huo aliamuru kodi hiyo ilipwe mara moja.
Lakini pia kwa mujibu wa TRA na Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), jamaa huyo amekuwa na tabia ya kuuza hisa kwa bei ya chini kwa makampuni mengine ili aweze kulipa kodi ndogo jambo ambalo pia ni kuonesha ni mfanyabiashara tapeli.
Jaji Werema akiteta jambo na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Kamati ya Zitto Kabwe ambaye ni mwenyekiti wa PAC, pia ilibaini kuwa, wakati yeye alijulikana kuwa ndiye mmiliki wa Kampuni ya IPTL ambayo baadaye aliiuza kwa Pan African Power Solutions Limited (PAP), uchunguzi wa PAC ukaja kubaini kuwa, mwenye PAP ndiyo huyohuyo mwenye IPTL, yaani singasinga huyo. Dah!
ALIHENYESHA BUNGE LA TANZANIA
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Bongo, Ijumaa iliyopita bunge liliendeshwa hadi saa 5:00 kasoro usiku, ishu ikiwa ni kujadili yaliyotokana na Kamati ya PAC baada ya kuchunguza wizi wa mabilioni ya shilingi kutoka Escrow kwenda IPTL kwa kupitia PAP.
Baadhi ya mawaziri na vigogo serikalini ambao wengine walimwaga machozi kutokana na kashfa waliyoipata kupitia Kampuni ya IPTL hawatamsahau singasinga huyo kwa vile amewaingiza kwenye kumbukumbu mbaya ya Taifa la Tanzania. Katika listi ya viongozi hao yumo Mizengo Pinda, Profesa Sopspeter Muhongo, Stephen Masele, Eliakim Maswi, Jaji Feredrick Werema na wengine wengi.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliliahirisha bunge hadi Januari, mwakani katika kikao cha 18 bila kumwadhibu mtu juu ya sakata hilo.

ZARI AZIDI KUJIWEKA KWA DIAMOND, USO KWA USO NA MAMA MKWE SOUTH AFRICA


Diamond Hivi Karibuni alidai kuwa yeye na the bosslady Zari hawana uhusiano wowote wa kimapenzi bali wapo kikazi, (project).


Lakini kwa kilichoonekana Usiku wa jana Afrika Kusini, ambapo mrembo Huyo alionekana kuwa karibu zaidi na Diamond Platnumz na Mama Mkwe wake wake yani Mama Diamond, Na wadau kuamini Kabisa Hakuna cha project bali kinachoelendea ni mahaba ninyonge kati ya Mrembo Zarina na Diamond Platnumz.

angalia picha zaidi hapo chini




WEMA SEPETU AZINGATIE USHAURI HUU WA SHABIKI WAKE


najua wewe ni mrembo sana ,una exposure na unapesa.sawa wanasema mwanamke bila mwanaume haiwezekani ila kwa mimi naona inawezekana jana nimekuona sehemu fulani kinondoni umelewa sana sana...hivi unadhani pombe ndio suruhisho la matatizo yako? tena unakunywa mi pombe mikali halafu wewe mwanamke .iko kizazi kitapona kweli kwa staili hiyo? nikupe siri mdogo wangu wewe ni mzuri sana una nafasi ya kuwa na mwanaume yeyote dunia hii na sio uchafu wa manzese huu unaokupaka paka vikwapa vya kila mwanamke ..

 kama ungeweza embu ondoka tanzania japo kwa miezi 6 nenda kakae zako nje ya nchi kama ulivyofanya kipindi kile ulipoachana na yule mla unga ..ukirudi utakuwa mpya wema mpya utakuwa umeweza kukaa mbali na huyo domo na utaona unaweza kuishi bila yeye
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga