Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

WATOTO 6 KWA MAMA TOFAUTI WAMFILISI DUDE, AKOSA PESA YA KUREKODI TAMTHILIYA YAKE.

HALI ya uchumi ya mwigizaji Kulwa Kikumba ‘Dude’ imemkwamisha mwigizaji huyo ashindwe kurekodi tamthiliya yake.
Kulwa Kikumba ‘Dude’.
Akizungumza na paparazi wetu, Dude alikiri kuwa uchumi umemkalia vibaya ambapo aliruhusiwa kupewa muda wa hewani katika Runinga ya East Africa lakini akashindwa kushuti kutokana na majukumu ya kifamilia kumuandama.



“Daa we acha tu, mwezi wa kwanza huu majanga matupu. Nimeshindwa, kama unavyojua nina watoto wengi mambo ya ada yamenibana kwelikweli,” alisema Dude ambaye ana jumla ya watoto sita kwa mama tofauti.

FARAJA KOTA, AFUNGUKA YA MOYONI KUHUSIANANA MUMEWE, WAZIRI NYALANDU.

MISS Tanzania 2004, Faraja Kota amefunguka kuwa kamwe hawezi kuingilia kazi za mumewe ambaye ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kwani anaamini mumewe ana akili nyingi kuliko yeye.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Akizungumza na paparazi wetu, Faraja alisema siyo rahisi kuingilia kazi za mume wake zaidi ya kuzungumza naye kidogo sana kama kuna kitu amekiona anaweza kumshauri kwa sehemu fulani lakini siyo kwa kiasi kikubwa sana.
Faraja Kota.



“Unajua mume wangu ana akili zaidi kuliko hata mimi, naweza kumshauri kidogo tu kama nitakiona kitu fulani na siyo vyote kwa sababu ninaporudi nyumbani anakuwa ni baba zaidi na siyo kama waziri,” alisema Faraja.

MIMBA ILIVYOMNYIMA "DILI" ZA HELA DAVINA WA BONGO MOVIES

STAA wa Bongo Movie, Halima Yahaya ‘Davina’ amefunguka kuwa mwaka 2013 aliutumia zaidi kwa kulea mimba hadi kujifungua hivyo kukosa madili ya kazi za uigizaji.
Halima Yahaya ‘Davina’.
Akizungumza na paparazi wetu, Davina alisema mwaka huu amejipanga kurejea upya katika sanaa kwani amegundua kuwa mashabiki wake walikuwa wamemmisi hivyo lazima apambane kutetea taito yake katika sanaa.



“Nimejipanga zaidi mwaka huu, nimedhamiria kufanya mapinduzi makubwa katika sanaa tofauti na kipindi cha nyuma, kulea siyo mchezo ilibidi sanaa ikae pembeni kidogo,” alisema Davina ambaye sasa ni mama wa mtoto mmoja, Fazal.

AMBER ROSE, JIKO LA WIZZY KHALIFA, ATUPIA ZA KIMETEGO MTANDAONI, NI SHIDAAA!!!!


Hakika ni kama anajaribu kuwatega watu kwa umbile lake matata, kwani hivi karibuni mrembo huyu aitwaye Amber Rose aliamua kuzitupia picha zake kwenye mitandao ya kijamii katika hali tu ya kushea picha hizo na watu wake! Hakika ni mkali...

Mcheki hapo chini kwa picha zaidi...


DC.

MFANYA BIASHARA APIGWA RISASI 3 NA KUFA PAPO HAPO NDANI YA GARI LAKE.

Mwili wa marehemu Ahmed Bakhshuwein baada ya kupigwa risasi.
Mfanyabiashara, Ahmed Bakhshuwein ameuawa kwa kupigwa risasi tatu kichwani akiwa kwenye gari eneo la Malindi, Mombasa karibu na Al-R azaak Stores nchini Kenya.
CREDIT: Michuzi Issa.




HALI ILIVYOKUWA WAKATI JENGO LA JMC LILIVYOPAMBA MOTO LEO MCHANA





JENGO la JMC lenye ghorofa saba lililopo eneo la Kamata mtaa wa Kasanga Kariakoo jijini Dar linaungua moto muda huu! Vyombo mbalimbali vya usalama vipo eneo la tukio vikijaribu kupambana na moto huo ambao bado unaendelea kuteketeza mali zilizomo ndani ya jengo hi

BILIONEA WA KIKE "OPRAH WINFREY" ATIMIZA MIAKA 60 LEO.


MWIGIZAJI, mmiliki wa vyombo vya habari, mtangazaji, prodyuza kutoka nchini Marekani, Oprah Gail Winfrey leo ametimiza umri wa miaka 60. Oprah ambaye amejishindia tuzo mbalimbali kupitia kipindi chake cha 'The Oprah Winfrey Show' alizaliwa Januari 29, 1954 Mississipi nchini Marekani. Oprah ni bilionea namba moja ambaye ni Mmarekani mweusi wa karne ya 20.

RIHANNA BILA "SIDIRIA" AKIMKUMBATIA JAY Z, CHEKI MAPICHA MENGINE YA TUKIO LA JUZI HAPA.


Pati ya awali ya The Roc Nation kwa ajili ya tuzo za awali za Grammy Brunch ilifanyika LA mnamo siku ya Jumamosi, January 25, 2014 huku ikihusisha nyota wengine toka Hollywood.
Uwepo wa Jay Z na Rihanna kilikuwa ni moja kati ya vitu vilivyogusa watu wengi waliofika kwenye tukio hilo kwa maswali kutokana aina ya pozi na kwa vile walivyokuwa pamoja.

Cheki hapo chini picha za tukio hilo...

 Hapa ni Rihanna na Jay Z wakichat kimtindo


Rihanna alifika kwenye tukio hilo akiwa na top moja matata huku ndani yake akiacha kuvaa bra na sketi ya toleo la Altuzzara spring 2014.


 Wageni wengine wliokfika alikuwepo watoto wa Will Smith, Jaden na Willow Smith, Ne-Yo, pia marapa T.I., J. Cole na Wale. 

MASTAA WA BONGO MOVIE WAMPONDA WEMA SEPETU BAADA YA KUNYANG'ANYWA KILA KITU NA MP#NZI WAKE KIGOGO WA SERIKALINI.


MASTAA wa kike Bongo wamecharuka na kutoa yao ya moyoni baada ya nyota mwenzao, Wema Sepetu kubwagwa na aliyekuwa mpenzi wake, anayetambulika kwa jina moja la Clement na kumnyang’anya vitu alivyompa kama zawadi wakati wa mapenzi yao.
Wema Sepetu.
Kuhusu Wema kuporwa ofisi yake ya Endless Fame Film Production, kupewa notisi ya nyumba aliyokuwa amepangiwa na kigogo huyo anayeelezwa yupo serikalini na kunyang’anywa magari siyo stori kabisa mjini.
Risasi Mchanganyiko lilifanya mahojiano na mastaa hao wikiendi iliyopita, kwa njia ya simu na kuwahoji kuhusu kitendo alichofanyiwa mwenzao ambapo walifunguka bila wasiwasi wowote.
USENGENYAJI
Wakali hao, waliopata kuzungumza na waandishi wetu kwa nyakati tofauti, baadhi wamemponda Wema kwa kutokuwa makini wakati akiwa kwenye uhusiano na kigogo huyo kwa kutaka kukabidhiwa hati za vitu alivyopewa.
Wa kwanza kuzungumza ni Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ ambaye alisema: “Mimi namshukuru Mungu kwa sababu sijapangiwa nyumba na mwanaume.  Naishi maisha yangu simpo ya furaha na amani, sipendi kuigiza maisha. Hao wasanii wanaopenda mambo makubwa wakati hawana uwezo,  nawashauri wafanye kazi, filamu zinalipa sana. Wasipende vitu vya haraka, maana siku zote vizuri huja taratibu.”
ZUWENA MOHAMED ‘SHILOLE’
“Mastaa tusijiachie sana kwa wanaume, kama ukipewa gari, upewe na kadi... tusidanganyike na tusipende kuhongwa, tutafute vya kwetu. Kama mtu anakupenda na anakusaidia kwa mapenzi mema, sawa mheshimu.”
WASTARA JUMA
“Inabidi tujitambue jamani, maana kuna watu wanatembea na mastaa makusudi ili wajulikane au kwa manufaa yao wenyewe. Tuache kuishi kwa kutegemea migongo ya wengine. Wengi hawana mapenzi ya kweli. Hata kama mmeachana, sasa kuna sababu gani ya kumnyang’anya mtu vitu ulivyompa?”
NURU NASSOR ‘NORA’
“Mimi najisikia vibaya sana... kama mtu unajiamini una kipaji, kwa nini usifanye kazi?  Mastaa tuache kujitangaza, kwa sababu tunatumika kama vyombo vya starehe tu.  Tutafute ndoa, tusitumie ustaa kufanya ufuska kwa sababu mali zinapita na mwisho wa siku tunaharibu maisha yetu.”
TAMRINA POSH ‘AMANDA’
“Utapeli ni mwingi, haya mambo ya kupewa vitu siyo vizuri kabisa, tuache.  Wanawake tuna akili fupi sana na tunajisahau tunapokuwa na wanaume wakati wenyewe wana kitu moyoni mwao, akishapata anachotaka anaanza matatizo.



“Bora nitembelee taksi au Bajaj kuliko kudhalilishwa... wanawake ni wajinga na huwa tunajidanganya kwa vitu visivyo vyetu, mwisho wa siku tunaumbuka. Tuache sifa za kijinga.”

LILE KAHABA "ALBINO" MWENYE MUONEKANO KAMA MZUNGU AZIDI KUWAPAGAWISHA WANAUME, SAFARI HII ANASWA MOROGORO.


Ama kweli sikio la kufa halisikii dawa! Mwanadada mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Fadhila Omary, mkazi wa Mbezi jijini Dar ametikisa midume na kuzua gumzo nchini baada ya kukamatwa mkoani Morogogo kwenye msako wa makahaba.
Albino akiwa mikononi mwa polisi.
KWA NINI?
Unaweza ukajiuliza kwa nini amegeuka gumzo lakini jibu ni kwamba ishu hiyo imemkuta hivi karibuni ikiwa ni miezi michache baada ya Mahakama ya Jiji la Dar ‘Sokoine Drive’ kumuonya kuwa imezichoka kesi zake za kunaswa kwenye misako mbalimbali ya makahaba.
MAMA WA WATOTO WAWILI
Fadhila ambaye ni mama wa watoto wawili, Juni 21, mwaka jana alifikishwa kwa mara ya tatu mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Jiji la Dar ‘Sokoine Drive’, Timothy Lyon baada ya kunaswa kwenye msako wa makahaba.
...Akielekea kituoni baada ya kunaswa katika msako wa makahaba.
HAKIMU MSHANGAO
Baada ya Lyon kumuona alishtuka na kumuuliza ‘hivi wewe Fadhila una matatizo gani? Mimi tangu nihamie mahakama hii kutoka Mahakama ya Wilaya ya Kisarawe, Pwani hapa sijamaliza hata mwaka lakini umeshaletwa mbele yangu mara tatu!’
Hakimu huyo alimweleza hayo Fadhila huku akionesha mshangao mkubwa.
KUMBE MKE WA MTU!
Katika utetezi wake, Fadhila alimtupia zigo la lawama mumewe, aliyezaa naye watoto wawili.
Alisema kuwa mwanaume huyo amekuwa akimpa fedha kiduchu za matumizi hali inayomfanya ajiingize kwenye biashara hiyo.
Baada ya utetezi huo, mumewe alipelekewa barua ya kuitwa mahakamani hapo ambapo alionywa juu ya kuitunza familia yake na mkewe alionywa kutopatikana tena na kesi kama hiyo kisha akapewa ushauri nasaha katika Kitengo cha Ustawi wa Jamii kilichopo mahakamani hapo.
Miongoni mwa mambo waliyoshauriwa ni kubadili mfumo wa maisha kwa  kujitafutia kipato kwa njia nyingine ya halali na kuelezwa madhara ya kuishi kwa kutegemea biashara hiyo haramu.
Baada ya kupewa somo, wote wawili waliahidi kubadilika lakini katika hali ya kushangaza ilidaiwa kuwa Fadhila baada ya kuwapa kisogo maofisa wa ustawi wa jamii, alichofanya ni kuhama mkoa na kwenda kufanyia shughuli hiyo mkoani Morogoro.
OFM KAZINI
Baada ya Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ kupata taarifa hizo ilitoa maelekezo kwenye kitengo chake cha Mtambo wa Kurekebisha Tabia (MKT).
MKT walifunga safari hadi mkoani Morogoro ‘Mji Kasoro Bahari (MKB) na kujiunga na vijana wa Kamanda Faustine Shilogile, Mkuu wa Polisi mkoani humo na kuvamia madanguro na vijiwe mbalimbali vya makahaba.
MKT na vijana wa Shilogile walipata fununu kuwa kuna kundi kubwa la makahaba eneo la Kaumba mjini humo ambapo mmoja wa mapaparazi wa MKT alitangulia eneo hilo kama mteja ndipo Fadhila na wenzake watatu wakamvaa wakitaka kumhudumia.
Wakati wakinadi biashara yao kwa MKT na kuahidi kutoa huduma kwa kadiri anavyopenda mteja (paparazi) ndipo maafande waliokuwa wamejibanza sehemu waliwavamia machangudoa hao na kuwatia nguvuni kwa ajili ya kuwafikisha mbele ya sheria.
Baadhi ya watu waliozungumza na MKT eneo hilo walisema, Fadhila amekuwa tishio kwa kuwapiga bao wenzake kutokana idadi kubwa ya wanaume wanaomgombea huku akiwa na vijana spesho wa kumlinda.
“Huyu dada, hapana chezea kabisa, sijui ana kizizi! Yaani tangu atue hapa Kaumba anawapiga bao wenzake, yaani mpaka aondoke na mteja ndiyo wenzake nyuma wapate wateja. Yaani wanamchukia sijui ana nini,” alisema mmoja wa mashuhuda hao.
Fadhila na wenzake pamoja na wanaume walionaswa wakiwahudumia walitiwa mbaroni na muda wowote watafikishwa mahakamani.



KALAMU YA MHARIRI
Uchunguzi wa OFM uliofanywa katika kila kona ya Tanzania umebaini kuwa hali ni mbaya kwani biashara haramu ya kuuza milii imeshika kasi mithili ya moto wa kifuu. Ni jukumu lako kujilinda kwani kuna hatari ya kukipoteza kizazi hiki kwa Ugonjwa wa Ukimwi.
GPL

AVULIWA NGUO NA KUBAKI NA "CHUP*" BAADA YA KUMUIBIA BUZI LAKE SIMU NA KUIFICHA KUAKO NYETI, ACHEZEA KICHAPO CHA MBWA MWIZI

Stori: Richard Bukos na Makongoro Oging'
MREMBO mmoja mkazi wa Mabibo Makutano jijini Dar es Salaam (jina lake halikupatikana) mwishoni mwa wiki iliyopita alinusurika kifo baada ya kuvamiwa na kudundwa baada ya kudaiwa kukwapua simu ya mwanaume na kuificha sehemu zake za siri.

Mrembo akiwa chini baada ya kuchezea kichapo.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, awali mrembo huyo alikuwa akila bata na mwanaume aitwaye Hashim kwenye Baa ya Jassun Inn iliyopo maeneo ya Mabibo huku mwanaume huyo akiwa ametandaza simu zake za kisasa juu ya meza.
Imedaiwa kuwa wakati wakiendelea kuponda raha, Hashim alikwenda msalani kwa lengo la kujisaidia na kuacha simu zake mezani, aliporudi hakumkuta mrembo aliyekuwa akiponda naye raha na simu yake moja haikuwepo.
...Akiwa amewekwa mtu kati na wananchi.
“Jasho lilimtoka Hashim na kuwauliza watu waliokaa jirani alikoelekea mrembo huyo,” alisema shuhuda mmojawapo wa tukio hilo na kubainisha kwamba msamaria mwema mmoja alimweleza Hashim mwelekeo wa mrembo huyo.
Bila kuchelewa Hashim aliwakusanya wapambe wake na kuanza kumtafuta mrembo huyo na wakamnasa mita kama 150 kutoka Baa ya Jassun na kumuuliza kuhusu simu iliyokuwa mezani lakini alileta ubishi.
“Walijitahidi sana kumbembeleza ili aitoe simu kwa hiyari yake lakini alikataa, ndipo Hashim na wapambe wakamwanzishia songombingo la nguvu na kufikia kumvua nguo hadharani na simu ikakutwa kwenye nguo yake ya ndani,” shuhuda wetu alisema.



Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kwamba, hadi kufikia kupatikana kwa simu hiyo, mrembo huyo alikuwa hoi kutokana na vurugu aliyofanyiwa na wapambe wa Hashim ambao walipoipata simu walimvisha nguo pamoja na wigi lake lililokuwa limemvuka.

GPL

PATA MUDA KUISOMA BARUA YA MMOJA WA "WASHKAJI" WA DIAMOND PLATINUMS AKIMPA NENO JAMAA WAKE.

KWAKO,
Nasibu Abdul ‘Diamond’. Pole na kazi na mihangaiko ya hapa na pale. Najua uko bize sana na shoo za kila kukicha. Siyo mbaya, ndiyo maisha, maana bila kazi inakuwa siyo maisha tena.
Muda mrefu sana hatuwasiliani... nasikia siku hizi unapokea simu kwa nadra sana! Hata hivyo, siyo lengo langu kuzungumzia hayo. Ni kitambo kidogo hatujakutana kwenye barua.
Naamini leo ni sahihi zaidi kukufikishia ujumbe huu. Hata kama kuna mengine niliyotaka kuzungumza nawe, lakini kuna jambo ulilofanya, limenifanya niweke mengine yote pembeni kwanza.
Diamond, siri ya mafanikio ya binadamu yapo katika utoaji. Hapo kuna mara mbili; kutoa kwa wahitaji ambao hawajiwezi au kutoa kama shukrani kwa wanaochangia mafanikio yako!
Mwaka jana katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar ulifanya Tamasha la Krismasi na Ngololo ambapo pia uliwashindanisha watoto kucheza wimbo wako wa Number One ambao ndani yake kuna kionjo cha Ngololo.
Ahadi yako kwa washindi ilikuwa ni kuwasomesha watoto hao katika shule bora kama zawadi kwao. Ilikuwa ahadi nzuri sana kwako, maana wote walikuwa wakisoma katika shule za kawaida a.k.a St. Kayumba.
Ile ilibaki kuwa ahadi tu... wengi waliamini yalikuwa maneno ya kujipaisha. Kitendo chako cha kutimiza ahadi hiyo Januari 21, mwaka huu kwa kuwapeleka hao watoto katika Shule ya Kimataifa ya Afrika Mashariki (East Africa International School), iliyopo Mikocheni, Dar kimekuongezea heshima kubwa kwenye jamii.
Hii imeonesha ni kwa namna gani umetambua na kuthamini elimu. Ni vigumu sana kwa msanii mwingine kufunika rekodi hii, hata kama mwingine akija kufanya, atakuwa ameiga kutoka kwako.
Nasikia wanafunzi hao, mmoja ameingia darasa la nne  na mwingine la tano na wote kwa pamoja umeahidi kuwasomesha mpaka watakapomaliza darasa la saba.
Hongera sana bwana mdogo. Hapo umeonyesha ukomavu wa fikra wa hali ya juu. Jambo hili liwe fundisho kwa wasanii wenzako. Kumbe mnaweza kufanya mambo makubwa kwa jamii na mkajenga heshima.
Bila shaka yoyote, utakuwa umejiongezea mashabiki luluki kwa tendo hilo ambalo pengine kuna msanii hakuwahi kulifikiria. Hapo tegemea mafanikio katika kazi yako, maana umerudisha sehemu ya pato lako kwa mashabiki wako.



Hongera sana. Nadhani nikuache ufanye kazi, lakini sasa Diamond, mbona hupokei simu za waandishi kamanda? Nasikia wifi yetu  amekubana... ni kweli? Hayo tutaongea siku nyingine ila kwa hili la kuwalipia madogo ada, chukua tano!
Yuleyule,
Mkweli daima,

MBALI NA KUPENDEZA NA KUVUTIA, BEYONCE AANIKA "NYETI" ZAKE HADHARANI ALIPOANZA KUPIGA SHOW JUKWAANI.


Bila kupoteza muda, picha zinajieleza, maana Beyonce alipata bahati ya kutumbuiza pamoja na mumewe,sasa basi katika songombingo za hapa na pale jukwaani, lol, kumbe kigua alichokivaa kinaonesha maumbile yake wazi, ni hatari


Angalia picha ya hatari zaidi hapo chini, yaani kila kitu wazi kabisa. Hii nini sasa?!! Mimi sisemi.




Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga