Habari kutoka Iringa zinasema kuwa kituo  cha polisi cha Ilula mkoani Iringa kimechomwa moto na wananchi wenye hasira  kufuatia polisi kumuua mwanamke mmoja mfanyabiashara ya mama ntilie  wakati wa msako maalum ulioendeshwa na jeshi la polisi dhidi ya  wafanyabiashara na watu wanaokunywa pombe mida ya kazi.
Inasemekana  wakati wa purukushani za kukimbia ndipo polisi mmoja alimchota mtama  huyo mama wakati anakimbia na kusababisha mama wa watu kuanguka na  kufariki dunia hapo hapo.
  


Muonekano wa mji wa Ilula mkoani Iringa baada ya wananchi kufunga barabara kuu ya mji huo.
Mabasi ya kwenda mikoani yakiwa yamepaki baada ya wananchi kufunga barabara.


 
 
 

