Feature

Udaku wa Africa

Habari za Kimataifa

Habari za Kitaifa

Mapenzi

Michezo na Burudani

Udaku wa Ulaya

DIAMOND PLATNUMZ, HISTORIA YAKE KWA UFUPI


Mkali wa Bongo fleva, Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond akipozi.

ANAITWA Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond. Alizaliwa saa kumi na moja jioni ya Oktoba 2, 1989 katika Hospitali ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Wazazi wake walimpa jina la Nasibu wakiamini ni la bahati.

Diamond aliongea hivi karibuni na safu hii ya Mjue Huyu ambapo aliweka wazi mambo mengi ya maisha yake. Diamond akiwa hajapata ufahamu, yaani bado mdogo, wazazi wake walitengana kwa sababu ambazo bado hazijawa wazi na baba yake kumuacha na mama.
Kufuatia hali hiyo, ilibidi mama yake ahamie kwa mama yake mzazi (bibi wa Diamond), Tandale Magharibi, Dar. Hapo ndipo yakawa makazi ya mama huyo na mwanaye.
Mnamo mwaka 1995, Diamond alianza elimu ya awali katika Shule ya Chakula Bora iliyopo Tandale- Uzuri. Mwaka 1996 alianza elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Tandale- Magharibi iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mwaka 2000, Diamond akiwa darasa la tano alianza kupenda muziki, hivyo akawa anakopi baadhi ya nyimbo za wasanii waliokuwa wakihiti ndani na nje ya Bongo na kuimba yeye katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam. Kwa kuliona hilo, mama yake alianza kumnunulia kanda za albamu za wasanii tofauti hata kumwandikia baadhi ya nyimbo za wasanii hao ili mwanae aweze kuzishika na kuimba kirahisi.
Diamond alizidi kuupenda muziki ikabidi mama yake awe anampeleka kwenye matamasha mbalimbali ili mwanae apate nafasi ya kuimba.
Baadhi ya ndugu walimjia juu mama huyo wakidai anamharibu mtoto badala ya kumuhimiza masomo anamwingiza kwenye muziki ambao walidhani haukuwa na faida yoyote.
'Diamond Platinumz'
“Kusema ukweli pamoja na yote hayo, hali ya maisha ilikuwa si nzuri kwa mama maana hakuwa na kazi ya maana wala vyanzo vikubwa vya fedha, hivyo ilibidi atumie kiasi kidogo alichokipata kutoka kwenye kodi ya vyumba viwili alivyopewa na bibi ili kunisomesha,” alisema Diamond.
CHUMBA KIMOJA NA MAMA
Diamond aliendelea kusema kuwa, kutokana na kupangisha vyumba viwili ilibidi yeye na mama yake kuhamia kwenye chumba cha bibi yake na maisha yakaendelea humo.
AMALIZA SHULE YA MSINGI
Mwaka 2002, Diamond alimaliza masomo ya elimu ya msingi lakini ili aende sekondari, mama yake alimwambia aachane na habari ya muziki azingatie masomo aweze kupata elimu itakayomsaidia mbele ya safari katika maisha.
AFANYA MUZIKI KWA SIRI
Nyota huyo aliendelea kusema kuwa akiwa sekondari, aliendelea kuimba muziki lakini kwa siri kubwa ili mama yake asijue.
Mwaka 2004, anasema alianza kuandika nyimbo zake mwenyewe kwa kuwa akili bado ilimwambia mafanikio yake yatapatikana huko.
AFANYA VIBARUA APATE PESA
Mwaka 2006, Diamond alimaliza elimu ya sekondari na kuanza kuimarisha ndoto yake ya kuwa mwanamuziki.
Alikuwa hana kazi ya kufanya nyumbani hivyo alianza kutafuta vibarua mbalimbali vya kumuwezesha kupata riziki ya siku. Miongoni mwa kazi hizo ni kuuza mitumba, kuweka mafuta kwenye magari (vituo vya mafuta), kupiga picha, kupigisha simu na kazi za kwenye viwanda mbalimbali.

NAY NA "AKADUMBA" NI HATAREE


Nay wa mitego hii sasa ni zidi ya Akadumba.Msanii Nay wa mitego amekuwa akiposti picha akiwa na Hot bebez tofauti tofauti na kuandika baadhi ya vipande vya wimbo wake mpya wa akadumba.

Wiki hii Nay ameposti picha ikimuonesha akiwa na mrembo bomba kisha na kuandika yafuatayo.
"Jinsi ulivyojaza nyuma kitaani napata Lawama,

Ona Sili Silali nikilala kitumbo chali..,

Unapokuwa mbali natamani kufunga safari..,
Lol Hii kweli ni Akadumba

BLUE "KAMA SIO NGOMA YA "PESA" GAME INGEKUWA BASI


Akizungumza kwenye kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV, rapper huyo alidai kuwa kama ngoma yake ‘Pesa’ ingebuma, angeachana kabisa na muziki na kuzamia Ulaya.
“Pesa kama Pesa ilikuwa ni project yangu ya mwisho,” alisema Kabayser. “Nilikuwa nimeshakata tamaa. Vitu vingi vilikuwa vinanisumbua, nilikuwa naplan kidogo niwakimbie watanzania nikatulie Uingereza. Nyumba yangu ilikuwa ipo kwenye finishing na itahitajika kama milioni 25 nimalize au 30 labda, nitaipata wapi hiyo hela, ikiwa mimi kazi yangu ni muziki? Ndioa Mungu akanisaidia nikatoa lile jiwe Pesa. Kwa mapenzi ya mwenyezi Mungu ikawa ni balaa,” aliongeza.
“Sasa baada ya kupata ile pesa ikabidi nichague nimalizie nyumba yangu au nitoe video watu wanijue kama huyu ni Mr Blue! Kwahiyo hela yangu yote nawashukuru Serengeti Fiesta naomba niseme wazi kabisa ni watu ambao wamenisaidia hilo tatizo. Kwasababu hela hiyo yote niliipata kwenye Fiesta.”
Kuhusu video ya Pesa, Blue alidai kuwa Adam Juma alishoot video ya Pesa bure, bila kumpa chochote.
“Adam Juma from nowhere, ni mtu ambaye sikuwahi kufikiria nitafanya naye video. Nilishajaribu kutaka kufanya naye lakini mipango ikawa haikamiliki. Alinipigia simu mwenyewe namshukuru sana Adam Juma na Mungu akusaidie kwa kunipa video bure kabisa! Yaani video kila kitu bureee kabisa. Mimi nasema kuishi na watu kwa upendo ndo zimefanya hivyo ninaweza kusema ni zawadi.”
Credit: Bongo5.com

DIDAH WA MITIKISIKO, NDANI YA MARK X

Raha sana mtangazaji wa kipindi cha mipasho cha TIMES FM Dida Shaibu akiwa morogoro Road na ndinga yake mpya. Lol acha auze sura mtoto wa kike na mali yake kwa jasho lake.
picha nyingine hii hapa chini

DULLY SYKES AELEZEASABABU YA KUREKODI WIMBO WA MATUSI NA MAUNDA ZORRO


Siku chache baada ya wimbo wake wa Thats The Way uliojaa matusi yasiyoweza kuandikika gazetini kuanza kusambaa kwa kasi kwenye mitandao , msanii wa kitambo wa muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amefunguka kuwa halikuwa kusudio lake kuachia wimbo huo bali ulivuja kwa bahati mbaya mitandaoni.
Akipiga stori na Showbiz juzikati, Dully alisema kuwa wimbo huo aliomshirikisha mwanadada Maunda Zorro, aliurekodi miaka nane iliyopita kwenye studio yake ya Dhahabu Records na hakupanga kuutoa lakini kwa bahati mbaya ukavuja na kuingia mitandaoni.
“Siyo mpya, ni wa kitambo sana, nilirekodi miaka nane iliyopita nashangaa kwa nini watu wanafikiri ni mpya,” alisema Dully lakini alipoulizwa hata kama ni wa zamani kwa nini alirekodi wimbo wenye maneno ya kuhamasisha ngono, hakuwa na majibu.
Licha ya utetezi wake huo, wimbo huo unaonekana kuwa mpya kwani sauti ya Dully inafanana na ya kwenye nyimbo zake mpya za hivi karibun

SHILOLE AKIPOZ NDANI YA HOTEL HUKO UBELIGIJI



Baada ya mwanadada Shilole Kuwasili uwanja wa kimataifa wa ndege wa Zeventem jijin Burssel Ubeligiji.Si ndo akaenda zake kujitafutia hoteli ya kujipumzisha. Sasa hiyo ndo picha yake ya kwanza akiwa hotelini humo.

WEMA NA PENNY MAMBO DAM DAM


Baada ya kuweka Tofauti zao pembeni na kukubali kwamba Diamond si wao tena, Warembo Wema Sepetu na Penny wamekuwa mashosti vibaya, kiasi cha kufikia kufanya mambo mengi pamoja, jiangalie mwenyewe walivyoamua kushona nguo Sare Sare.

ZARI THE BOSS LADY, DIAMOND PLATINUMZ, MAHABA NIUE TU.


Wataalamu wa mambo wamepitisha kuwa hakuna haja ya kumlaumu Diamond Platnumz kwa kuamua kupigana chini na Wema Sepetu na kuanzisha uhusiano mpya na mrembo tajiri Kutoka nchini Uganda Zarina Hassan "Zari" kwa kuwa mrembo Zari ni mzuri sana so angeweza kumdatisha Mwanaume yeyote yule na Si Diamond Tu.

IRINE UWOYA, ANA MTOTO MZURI....


Katoto hako kazuri, kama mama mtu, hope katafuata nyayo nzuri za kuingia katika game kama b mkubwa wako, though hatujajua what mama mtu ana wish mwanae afanye. ila ndo hivyo safisha macho kwa kumwona mtoto wa staa wako umpendae.

DIAMOND PLATNUMZ, AKIFANYA YAKE IRINGA TOWN.


Hivi ndivyo jinsi Msanii Diamond Platnumz alivyoweza kukonga nyoyo za mashabiki wa Iringa Town alipoenda kupiga show. Mbali na maskendo yake na Projects zake lakini Mashabiki lukuki walifurika Uwanjani.

LULU MICHAEL "HOT PHOTO"


Pata muda ku mcheki mtoto Lulu Michael akiwa katika kivazi cha aina yake, Kama una lolote la ku coment dondoka hapo chini uweke maoni yako, katokelezea au la?!

DIAMOND AKIMLA "MATE" ZARI THE BOSS LADY, NI PROJECT TU.


Kama kawaida yake Diamond Platinumz mzee wa Totoz, Dangote wa BOngo, awali alisema ni "PROJEKTI" tu inayowaweka karibu wawili hao, lakin mwisho wa siku....

JOKATE ALAMBA SHAVU


Baada ya Salama Jabir kupata shavu la kuwa na show kwenye kituo cha runinga cha Maisha Magic, sasa ni zamu ya Jokate Mwegelo. Mtangazaji huyo anatarajiwa kuongeza show yake ya tatu katika TV (baada ya The One Show ya TV1 na Top 10 Most ya Channel O), itakayoanza kuonekana kupitia Maisha Magic, December mwaka huu.

Jokate atashirikiana na mtangazaji maarufu wa Uganda, Gaetano Kagwa kuendesha kipindi hicho kiitwacho Beat the Challenge.
Beat the Challenge ni kipindi kitachokuwa kikihusisha mashindano ya familia 12 (baba, mama na watoto wao wenye umri kuanzia miaka 12 hadi 17) wataokuwa wakihusika kwenye kazi mbalimbali na kuulizwa maswali kuhusu uelewa wa masuala mbalimbali.

Show hiyo itaanza kuonekana kupitia Maisha Magic (DSTV CHANNEL 161(, Jumamosi ya December 13, saa 2 na nusu usiku. Usaili utafanyika Nairobi November 22, Supersport Studios, Tanzania ni siku hiyo hiyo New Africa Hotel Dar es Salaam na Kampala utafanyika Silver Springs Hotel Kampala,kuanzia saa tatu asubuhi.
Blogger Tips and TricksLatest Tips And TricksBlogger Tricks

Majanga